Kamis, 24 September 2009

Marekani yaonekana kusalimu amri kwa urusi. yafuta mpango wake wa kuweka makombora ya kujikinga Ulaya ya mashariki


RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI NA DMITRY MEDVEDEV WA RUSSIA


Akihutubia baraza kuu la umoja wa mataifa, rais wa Urusi Dmitri Medvedev ameueleza uamuzi wa Marekani wa kutoendelea na mradi wake wa ngao dhidi ya makombora katika bara la Ulaya kuwa ni hatua muhimu kuelekea katika mwelekeo sahihi.

Akizungumzia mzozo wa mwaka jana wa kivita kati ya Urusi na Georgia, Medvedev ameshauri kupatikana mkataba mpya wa usalama katika bara la Ulaya ili kutatua mizozo kama hiyo.

Leo Alhamis, rais Barack Obama anatarajiwa kuwa mwenyekiti wa mkutano wa baraza la usalama la umoja wa mataifa, ikiwa ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kufanya hivyo tangu kuundwa kwa baraza hilo mwaka 1946.

Kikao hicho cha leo kitalenga katika kupunguza silaha za kinuklia. Azimio lililotayarishwa na Marekani linatarajiwa kuyatolea wito mataifa kuondoa kabisa hazina zao za silaha za kinuklia kwa kutia saini na kuidhinisha mkataba unaozuwia kuenea kwa silaha hizo pamoja na mkataba unaozuwia majaribio ya silaha za kinuklia. Mkataba wa pili bado haujaidhinishwa na Marekani pamoja na mataifa mengine manane yaliyo na teknolojia ya kinuklia, ikiwa ni pamoja na India na Pakistan.

Ukoloni unaanza kurudi kiaina aina


Korea Kusini yaomba kulima Tanzania

Korea Kusini imesema imekubaliana na serikali ya Tanzania kutumia eneo kubwa la nchi hiyo kwa ajili ya kuendesha shughuli za kilimo, ikiwa ni hatua ya mpya katika mfululizo wa mikataba baina ya mataifa tajiri na masikini.

Maafisa wa serikali ya Korea Kusini wanasema kilomita za mraba 1,000 zitaendelezwa, ambapo nusu ya mazao yatakayopatikana yatakuwa kwa ajili ya matumizi ya wananchi wa Korea na nusu kwa ajili ya wakulima wa eneo hilo.

Hata hivyo serikali ya Tanzania imesema bado swala hilo lipo katika hatua ya majadiliano.

Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Waziri wa kilimo, chakula na ushirika, Stephen Wasira, alisema ni kweli serikali imepokea maombi kutoka Korea Kusini lakini bado hakuna mkataba uliosainiwa.

"Walituarifu, walituambia wakati tukiwa pale. Siwezi kusema kwa sasa hivi, kama ni jema au si jema. Kwasababu kitu hii bado hata details zake hazijawa worked out", alisema Bw Wasira.

Bw Wasira aliongeza kuwa: "Lakini kwamba tunakaribisha investors kwenye agriculture, ni policy iko very clear, sasa unawakaribisha kwa conditions gani? Hizo ndiyo zinatakiwa ziwe worked out na mwekezaji pamoja na serikali ya Tanzania", alibainisha Bw Wasira.

Nchi kama China, Saudi Arabia, Korea Kusini na Kuwait zina upungufu wa ardhi yenye rutba na zimekuwa zikitafuta kuwekeza katika sekta ya kilimo Afrika.

Kampuni inayomilikiwa na serikali ijulikanayo kama Korea Rural Community Corporation imesema mkataba wa ushirikiano utasainiwa nchini Tanzania mwezi ujao.

Mkataba huo wa Tanzania na Korea Kusini umeafikiwa wiki mbili baada ya Waziri mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda, kuzuru Seoul ambako nchi zote mbili zimeahidi kuimarisha ushirikiano.

Korea Kusini pia ilisaini mkataba mwaka jana kuweza kukodisha eneo kubwa la Madagascar

Lakini hatma ya makubaliano ya Madagascar - ambayo yangetoa fursa kwa eneo kubwa kwenye kisiwa hicho kutumika kulima mazao kwa manufaa ya Korea Kusini, haijulikani.

Serikali ya Madagascar iling'olewa katika mapinduzi mapema mwaka huu na viongozi wapya wamesema watasitisha mpango huo, ambao ulielezwa kuwa sehemu ya machafuko ya kisiasa nchini humo.

Njia nyeupeeeee kupata tiba ya UKIMWI


Chanjo imejaribiwa kwa wanawake na wanaume wasioathirika nchini Thailand

Watafiti wanasema kwa mara ya kwanza chanjo ya UKIMWI iliyofanyiwa majaribio imeweza kupunguza uwezekano wa kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo.

Chanjo hiyo ambayo ni mchanganyiko wa chanjo mbili zilizofanyiwa majaribio hapo awali, iligaiwa kwa watu 16,000 nchini Thailand.

Watafiti hao wamesema imepunguza kwa takriban theluthi ya hatari ya kuambukiza ukimwi, virusi vinavyosababisha ukimwi.

Imesifiwa kuwa ni hatua muhimu hasa katika nyanja ya kisayansi, licha ya kuwa chanjo hiyo bado ina safari ndefu ya kutumika duniani kote.

Utafiti huu ulifanywa na jeshi la Marekani na serikali ya Thailand kwa zaidi ya miaka saba kwa watu waliojitolea.

Watu hao waliojitolea walikuwa wanawake na wanaume wa kati ya umri wa miaka 18 hadi 30 katika maeneo yaliyoathirika sana na ugonjwa huo huko Thailand.

Rabu, 23 September 2009

Obama alihutubia Baraza kuu la Umoja wa mataifa.


Asema Marekani haiwezi kutatua matatizo ya dunia peke yake.


Baraza kuu la umoja wa mataifa limeanza kikao chake cha kila mwaka mjini New York leo, huku macho yote akikodolewa Rais wa Marekani Barack Obama aliyelihutubia baraza hilo kwa mara ya kwanza muda mfupi uliopita.

Katika hotuba yake Rais Obama alisema dunia inahitaji kushirikiana pamoja chini ya misingi ya kuheshimiana na kuvumiliana. akasema wakati wa hotuba tu umekwisha badala yake hatua za kivitendo . Kiongozi huyo wa Marekani alitaja juu ya hatua zilizochukuliwa na utawala wake, ikiwa ni pamoja na kupinga mateso, kulifunga gereza la Guantanamo na kutangaza ratiba ya kuondoa wanajeshi wake nchini Irak.

Kiongozi huyo wa Marekani aliyekua akilihutubia baraza kuu la umoja wa mataifa kwa mara ya kwanza aliwaambia viongozi wenzake kwamba Marekani haiwezi kutatua matatizo yote ya dunia peke yake na badala yake panahitajika ushirikiano zaidi baina ya mataifa kuyakabili matatizo hayo kwa pamoja.

Rais Obama akazungumzia pia haja ya kuzuwia kusambaa kwa silaha za nyuklia . Akasema nchi yake itaendeleza mazungumzo na Urusi kupunguza silaha hizo. Akizungumzia migogoro duniani alisema Marekani itaendeleza juhudi za kupatikana amani kati ya Israel na Wapalestina na haja ya mataifa mawili Israel na Palestina kuishi pamoja na pia amani ya mashariki ya kati kwa jumla .Pia akataja juu ya haja ya kupatikana amani huko Darfur, alakini dunia kwa jumla lazima iamuwe kama kweli imejizatiti kuishi kwa amani.

Hotuba yake pia iligusia juu ya ongezeko la ujoto duniani kufuatia mabadiliko ya hali ya hewa na suala la umaskini na kuongezeka kwa maradhi . Obama akaonya juu ya kitisho kinachoukabili ulimwengu pindi jumuiya ya kimataifa haitashikamana kukabiliana na matatizo hayo.

Hapo awali kikao cha baraza hilo kilifunguliwa na katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon, ambaye alitoa wito mbele ya zaidi ya viongozi 120 akiwataka kuchukua hatua ya dhati na ya pamoja,kuzuwia mabadiliko ya hali ya hewa, kupambana na umasikini duniani na kushinikiza juu ya kupunguzwa silaha za nukliya.Aidha alitoa pia wito wa kumalizwa migogoro duniani,"Tunataka kumaliza umwagaji damu katika Gaza, masuala ya haki na uwajibikaji yanapaswa kushughulikiwa, lazima kufufua mazungumzo juu ya kuwepokwa dola mbili na utaratibu madhubuti wa amani ya Mashariki ya kati."

Kikao cha mwaka huu pia kinahudhuriwa na viongozi wawili ambao kuwepo kawao kumegonga vichwa vya habari. Hao ni rais Mahmoud Ahmadinejad wa Iran na Kiongozi wa Libya ambaye pia ni mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika Kanali Muammar Gaddafi. Baadhi ya wajumbe wa nchi za magharibi ikiwemo Ujerumani wameshtamka kwamba wataondoka kikaoni pindi wakati wa hotuaba yake Rais Ahmadinajed atatoa matamshi ya kukana maangamizi makubwa ya Wayahudi wakati wa vita vya pili vya dunia au matamshi yanayoashiria chuki dhidi ya Wayahudi.

Kwa upande wa Gaddafi atalihutubia baraza kuu kwa mara ya kwanza .Kiongozi habari tayari amekua kivutio kutokana na viroja vinavyohusiana na kuwepo kwake. Kiti chake mkutanoni kimeandikwa " Tuko hapa", na kwa mujibu wa mjumbe mmoja wa Libya maneno hayo yameandikwa kwa lugha ya Kiingereza na Kiarabu.

Tayari jana kulizuka utata mwengine, wakati kanali Gaddafi alipotaka ajengewe hema katika mji wa Bedford na kuwa maskani yake , lakini maafiwa wa mji huo wakazuwia hatua hiyo wakisema inakwenda kinyume na sheria za mji huo.

Hapo kabla maafisa wa Gaaddafi walitaka kujenga hema hilo katika bustani kuu ya jiji la New York na paia katika eneo la ubalozi wa Libya katika kitongoji cha New Jersey lakini matamkwa yote mawili yakazuiwa. Hadi sasa haijulikani Kiongozi huyo wa Libya atakaa wapi wakati wa ziara hii ya Marekani,aya kwanza tangu 1969 alipotwaa madaraka katika mapinduzi yaliomuangusha Mfalme Idris 1969.

Rabu, 16 September 2009

New Brand for USD 250. Price negotiable.

Warning: IT IS NOT THE APPLE IPHONE PRODUCT


descriptions:

Style

Smartphone

Status

UNLOCKED

Languages

English / French / Italian / Arabic / Russian / Viatnamese / Portugues / Spanish / German

Screen

3.5'' screen / 16 million color QVGA / PX : 320*240

Bluetooth

Enabled

Data Transfer bluetooth

Radio

FM radio

Memory

2GB TF for free (INCLUDED IN PHONE) MAX SUPPORT 16GB

Camera

1.3 MP camera for Picture & Video capability, Tested put out biggest size is 640*480

Bandwidth

Quad-band (850/900/1800/1900Mhz)

SIM card Slot

Dual Active SIM (Two active lines operates)

Ring tones

64 chord ring tone / Stereo Loud speaker

Telephone Directories

Music

MP3

Movie

MP4, 3PG (watch movie upto 8hrs)

Messages &
Multimedia Messaging

200 SMS / MMS

Game

Built in games (5 built-in common games)

Functions

Hands free / Voice recorder / self-designed ringtones / photo editor / calculator / otepad / health management / calendar / To do list / Alarm / World Clock / Spot watch

Communication

WAP / GPRS / JAVA

Scheduled Power On/Off

Starting and shutting images as your wish / auto power off

Alarm Clock

MP3 alarm clock / MP3 alarm clock

Keyboard

Touch screen / Handwriting Stylus

WEB

GPRS / WAP

Em@il

POP3 and IMAP

Conversions

Unit conversion / Currency conversion

Warrant

6 months with the company. (3 days check and free shipping to and fro the company USA for maintenance)

Extra features

shake control. forward, rewind music by shaking the phone. also next picture or backward by shaking the phone.

Operating System

Applications

slide to unlock

> Works

Worldwide


> Parameters :

Interface

USB

Stand-by time

7 to 10 days

Talk time

3 to 4 hrs

Dim (l x w x d)

115 x 61 x 11.5 mm

Weight

100 g


> In the Box :

1 x

Celphone full Touch screen smartphone

2 x

Lithium batteries (2 X 1800 mAh)

1 x

Wall charger

1 x

2GB TF memory card

1 x

Earphones

1 x

USB cable

1 x

User manual


1 x

Car charger (1st Gift)