Selasa, 27 Oktober 2009

mjadala mkubwa waibuka tena bungeni. safari hii ni kati ya Spika Sitta na Waziri Pinda

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (kushoto) akizungumza na Spika wa Bunge Samweli Sitta (kulia) na Mbunge wa tabora mjini Silaju Kaboyonga nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma jana.

MSUGUANO kati ya mihimili miwili, Bunge na Serikali umejitokeza baada ya Spika Samuel Sitta na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutofautiana kuhusu hatua ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwahoji wabunge kuhusu tuhuma za watunga sheria hao kulipwa posho mara mbili.

Wakati tofauti hizo zikijidhihirisha kwenye kikao cha faragha cha wabunge kilichofanyika ukumbi wa zamani wa Bunge unaojulikana kama Pius Msekwa, mmoja wa vinara wa vita dhidi ya ufisadi, Dk Harrison Mwakyembe aliongea na waandishi wa habari na kushutuma vikali kitendo hicho cha Takukuru akikielezea kuwa ni cha kisasi na kusema kamwe hatakubali kuhojiwa.

Hatua ya Takukuru kuhoji wabunge hao imetokana na malalamiko kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kulalamikia mwenendo wa Kamati za Bunge kudai posho mara mbili kwenye idara na taasisi za serikali. Bunge hugharimia posho kwa ajili ya shughuli za kamati zao zinazosimamia vyombo hivyo, lakini baadhi ya wabunge walidaiwa kuendelea kupokea posho mara mbili, hali ambayo iliilazimisha Takukuru kuanza kuwahoji wanaotuhumiwa kufanya hivyo.

Lakini wabunge, akiwemo Spika Sitta, wamekuwa wakipinga kitendo hicho na jana serikali ilionekana kuunga mkono wabunge kuhojiwa huku Bunge likiendelea kupinga.

Tofauti za watendaji hao wawili wa serikali na Bunge zilizijitokeza jana mchana wakati wabunge walipokutana kwa faragha kupokea taarifa ya agenda zilizopitishwa na Kamati ya Uongozi kwa ajili ya kujadiliwa kwenye mkutano unaoendelea mjini hapa.

Suala la kuhojiwa kwa wabunge lilizua mjadala mkali kiasi kwamba mkutano huo, ambao awali ulikadiriwa kuwa ungechukua takriban saa moja kuanzia saa 5:15 asubuhi, ulimalizika karibu saa 8:00 alasiri.

Katika mjadala huo, mbunge wa Dole, Juma Suleiman N’hunga (CCM) alienda mbali na kusema chombo kilichopaswa kuwahoji wabunge ni Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge na sio Takukuru ambao ni mhimili mwingine wa dola.

Kwa mujibu wa mbunge huyo, kitendo cha Takukuru kuwahoji wabunge ambao ni mhimili wa Bunge ni ukiukwaji wa katiba na akapendekeza Takukuru ikatazwe kuendelea na zoezi lake la kuwahoji wabunge.

Mbunge mwingine aliyechangia mjadala huo mzito alipendekeza Bunge limpigie kura ya kutokuwa na imani na mkurugenzi wa Takukuru, Dk.Edward Hoseah kama ilivyotokea kwa taasisi kama hiyo nchini Kenya.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walitofautiana katika suala hilo, huku baadhi wakihoji sababu za chombo hicho kukaa kimpya wakati Basil Mramba alipohojiwa na kushitakiwa mahakamani.

Mramba, aliyekuwa waziri wa fedha katika serikali ya awamu ya tatu na baadaye waziri wa miundombinu katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete, anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi iliyoiingizia serikali hasara ya mamilioni.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zimedokeza kuwa Mramba alitumia mkutano huo kuelezea kwa kirefu namna alivyohojiwa na Takukuru katika mazingira ya kudhalilisha tena na vijana wadogo ambao hawakustahili kumhoji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shelukindo naye alitumia kikao hicho kuelezea masaibu yaliyomkuta wakati alipoitwa na Takukuru kutoka jimboni kwake hadi Dar es Salaam na kuhojiwa kwa saa nne.

Shelukindo alihoji inakuwaje Takukuru ianzishe uchunguzi huo sasa wakati ambao Bunge linatakiwa kupokea utekelezaji wa maazimio yake ambayo baadhi yanataka DK Hosea awajibishwe.

Pamoja na Spika kueleza kuwa tayari ameandaa mazingira mazuri yatakayotumika kuwahoji wabunge hao ikiwamo kuipatia Takukuru ofisi kwenye jengo la Bunge mjini Dodoma na Dar es Salaam Salaam, bado baadhi ya wabunge walipinga.

Kutokana na michango ya wabunge wengi kuonyesha dhahiri kukerwa na kitendo cha Takukuru, Spika Sitta alitangaza katika kikao hicho kuwa kuanzia hiyo jana mahojiano hayo yamesimamishwa.

Lakini Waziri Mkuu akaonyesha kutokubaliana na maamuzi hayo ya spika na kueleza kuwa uchunguzi huo wa Takukuru utaendelea kwa kuwa ofisi ya Rais Ikulu ndio ambayo imeagiza ufanyike.

Waziri Mkuu Pinda alisisitiza kuwa kinachotakiwa kufanywa si kusitishwa kwa uchunguzi huo bali ufanyike katika maeneo yenye staha na katika mazingira ambayo hayawadhalilishi wabunge.

Mkutano huo haukuelezwa pia kama ni lini ripoti ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge itawasilishwa bungeni katika mkutano huu wa 17 hali ambayo inazidisha usiri na uzito wa mjadala kuhusu kashfa ya Richmond.

Wakati hayo yakiendelea, mbunge wa Kyela, Dk Mwakyembe aliwaambia waandishi wa habari kuwa lengo la Takukuru kuendesha uchunguzi huo ni kuwafunga midomo wabunge wasishikie bango kashfa ya Richmond.

Dk. Mwakyembe, ambaye aliiongoza kamati teuli iliyochunguza kashfa ya Richmond, alisema binafsi hawezi kukubali kile alichodai ni upuuzi wa taasisi hiyo kutaka kuwahoji wabunge katika kipindi hiki tete cha Richmond.

Dk Mwakyembe aliishangaa taasisi hiyo akiitaka ijichunguze kwanza kabla ya kuamua kuwachunguza wabunge kuhusu malipo ya posho mbalimbali, huhusan posho za chakula.

“Takukuru waliponipigia simu kunihitaji, nilikataa kwa sababu kwa mazingira yenyewe hili zoezi linaendeshwa kwa malengo ya kuwafunga midomo wabunge kuhusu sakata la Richmond …mimi nilikataa,” alisema.

Alisema kuwa malipo hayo ya posho yamekuwepo miaka mingi na yamekuwa yakitengewa bajeti katika fungu la kuwakirimu wageni na haoni chembe yoyote ya rushwa katika suala la malipo hayo.

Dk.Mwakyembe alisema alikataa wito huo wa Takukuru kwa kuwa ulikuwa unakwenda kinyume na haki na madaraka ya Bunge na pia ni kinyume cha vifungu 100 na 101 vya katiba ya nchi vinavyotoa uhuru kwa Bunge.

“Sisi wabunge tunasubiri utekelezaji wa maazimio ya Bunge na moja ya maazimio hayo yanataka mtendaji mkuu wa Takukuru awajibishwe kwa kutofanya vizuri kazi yake katika uchunguzi wa Richmond,” alisisitiza Mwakyembe.

“Alisema mchakato bado haujakamilika na wewe unaenda kuwahoji wale wanaokuhoji... hilo halikubaliki na ni kinyume cha utawala wa sheria…mimi ni mwanasheria mwalimu wa sheria siwezi kukubali upuuzi huu.”

Dk. Mwakyembe aliitaka Takukuru kumpeleka mahakamani kama ana makosa na kutamba kuwa hata ikifanya hivyo ataibwaga mahakamani na kusisitiza mafisadi wasitumie vyombo vya habari kumchafua.

“Tukiaanza kuongelea mambo ya posho Takukuru wenyewe ndio vinara wa kutoa posho…wametufanyia semina mara mbili mimi; naishi Dar es salaam, wanatulipa posho ya kulala wajichunguze wao wenyewe kwanza,” alisema.

Mwanasiasa huyo aliitaka Takukuru kuacha kukimbilia vitu vidogovidogo na badala yake ishughulikie mambo makubwa yenye maslahi kwa nchi.

Senin, 26 Oktober 2009

We must honor him, not only Tanzania but also the whole Africa as well...

“The Africa that we must create must be an Africa which the outside world will look at and say: If you really want to see free people who live up to their ideals of human society, go to Africa. That is the continent of hope for the human race.”
-Mwalimu Julius K. Nyerere, Wellesley College, 1960


The Embassy of the United Republic of Tanzania, in collaboration with the Institute of African Studies of the Russian Academy of Sciences organize Memorial Symposium of the Tenth Anniversary of the First President of the United Republic of Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere which will take place at the Russian Academy of science Institute for African Studies Moscow Ruusia on 28/10/2009 from noon.

Many experts who know Mwalimu Nyerere will take the stage including:

  • Prof. Alexei Vassiliev , Director of the Institute for African Studies, Corresponding Member RAS
  • H.E. Jaka M. Mwambi, Ambassador Extraordinary and Plenipotentiary of the United Republic of Tanzania to the Russian Federation
  • Svetlana Shlyonskaya , Senior Research Fellow, Institute of African Studies, RAS - “Julius Nyerere and His Heritage”
  • Prof. Issa Shivji, Mwalimu Nyerere University Professor of Pan-African Studies, University of Dar es Salaam -Mwalimu Nyerere’s Thought and Practice on: The Village as Site of Development
  • Dr. Adolf Mkenda, Head of Department of Economics, University of Dar es Salaam“ Reflections of Economic Legacy of Mwalimu Julius Kambarage Nyerere”
  • Ambassador Doku Zavgaev, Former Ambassador of the Russian Federation to Tanzania
  • Prof. Vasili Solodovnikov, Corresponding Member RAS
  • Prof. Nelli Gromova, Head of African Department, Institute of Asia and African Studies, MSU
  • Mr. Rifat Pateev, Head of the Department of Asia and Africa, “Roszarubezhtsentr”
  • Ambassador Arkady Glukhov, Former Ambassador of the Russian Federation to Tanzania
  • Dr.Nikolai Kosukhin, Senior Reserarch Fellow, Institute of African Studies, RAS
  • Dr. Vladimir Ovchinnikov, Senior Reserarch Fellow, Moscow Museum of History
  • Mr. Oleg Teterin, Deputy Editor, Journal of Asia and Africa


Minggu, 25 Oktober 2009

Are vaccinations of swine flu really helpful?

is swine flu really that dangerous? Are vaccinations really helpful, or just another source of revenue for drug companies? People on the streets of New York have mixed feelings on the issue.

RT’s “The Resident”, Lori Harfenist, asked them if they want to get vaccinated and why.





Sabtu, 24 Oktober 2009

Obama declares swine flu a national emergency. about 1000 USA citizen died


WASHINGTON – President Barack Obama declared the swine flu outbreak a national emergency, giving his health chief the power to let hospitals move emergency rooms offsite to speed treatment and protect noninfected patients.

The declaration, signed Friday night and announced Saturday, comes with the disease more prevalent than ever in the country and production delays undercutting the government's initial, optimistic estimates that as many as 120 million doses of the vaccine could be available by mid-October.

Health authorities say more than 1,000 people in the United States, including almost 100 children, have died from the strain of flu known as H1N1, and 46 states have widespread flu activity. So far only 11 million doses have gone out to health departments, doctor's offices and other providers, according to the Centers for Disease Control and Prevention officials.

Administration officials said the declaration was a pre-emptive move designed to make decisions easier when they need to be made. Officials said the move was not in response to any single development.

Health and Human Services Secretary Kathleen Sebelius now has authority to bypass federal rules when opening alternative care sites, such as offsite hospital centers at schools or community centers if hospitals seek permission.

Some hospitals have opened drive-thrus and drive-up tent clinics to screen and treat swine flu patients. The idea is to keep infectious people out of regular emergency rooms and away from other sick patients.

Hospitals could modify patient rules — for example, requiring them to give less information during a hectic time — to quicken access to treatment, with government approval, under the declaration.

It also addresses a financial question for hospitals — reimbursement for treating people at sites not typically approved. For instance, federal rules do not allow hospitals to put up treatment tents more than 250 yards away from the doors; if the tents are 300 yards or more away, typically federal dollars won't go to pay for treatment.

Administration officials said those rules might not make sense while fighting the swine flu, especially if the best piece of pavement is in the middle of a parking lot and some medical centers already are putting in place parts of their emergency plans.

"I think the term emergency declaration sounds more dramatic than it really is," said Dr. Peter Hotez, a research professor and chairman of the Department of Microbiology, Immunology and Tropical Medicine atGeorge Washington University. "It's largely an administrative move that's more preemptive ..." He said such a step would give emergency rooms and hospitals the flexibility they need.

The national emergency declaration was the second of two steps needed to give Sebelius extraordinary powers during a crisis.

On April 26, the administration declared swine flu a public health emergency, allowing the shipment of roughly 12 million doses of flu-fighting medications from a federal stockpile to states in case they eventually needed them. At the time, there were 20 confirmed cases in the U.S. of people recovering easily. There was no vaccine against swine flu, but the CDC had taken the initial step necessary for producing one.

"As a nation, we have prepared at all levels of government, and as individuals and communities, taking unprecedented steps to counter the emerging pandemic," Obama wrote in Saturday's declaration.

He said the pandemic keeps evolving, the rates of illness are rising rapidly in many areas and there's a potential "to overburden health care resources."

The government now hopes to have about 50 million doses of swine flu vaccine out by mid-November and 150 million in December. The flu virus has to be grown in chicken eggs, and the yield hasn't been as high as was initially hoped, officials have said.

"Many millions" of Americans have had swine flu so far, according to an estimate that CDC Director Dr. Thomas Frieden gave Friday. The government doesn't test everyone to confirm swine flu so it doesn't have an exact count. He also said there have been more than 20,000 hospitalizations.

Sweeden Lutheran Church yaidhinisha ndoa za jinsia moja

Ndoa ruksa wapenzi jinsia moja Sweden
Kanisa la kilutheri nchini Sweden lenye waumini wengi zaidi nchini humo limekubali kubariki ndoa za wapenzi wa jinsia moja kuanzia mwezi ujao.

Asilimia 70 ya baraza kuu la kanisa hilo lilipigia kura kuunga mkono hatua hiyo. Kanisa la kilutheri limejiunga na imani nyingine chache duniani zinazokubaliana na ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Serikali ya Sweden imepitisha sheria mpya kulinda wapenzi wa jinsia moja. Robo tatu ya raia wa Sweden ni waumini wa Lutheran, japo idadi ya wanaohudhuria ibada imepungua sana.

Mwanyi alipojiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani mwaka 1977

Uadilifu wa Mzee Mwinyi huu hapa

Barua yake ya kujiuzulu yathibitisha
Ni changamoto kwa wanaojiuzulu sasa
Alishinda umakundi, visasi na chuki
Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi.

Wakati Taifa likipita katika kupindi kigumu cha kupima uadilifu wa viongozi, wengine wakijiuzulu na kuendelea kulalamika, Nipashe imefanikiwa kupata barua ya kujiuzulu aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hassan Mwinyi, ikithihibitisha jinsi kiongozi huyo alivyo juu kwa viwango vya utiifu na uadilifu.

Katika barua hiyo ambayo inasambazwa kwenye mitandao kwa sasa, inaonyesha jinsi Mwinyi alivyojiuzulu kwa unyenyekevu Januari 22, 1977 wadhifa wa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Kiongozi huyo ambaye mwaka 1985 alikuja kukwea tena ngazi kuwa Rais wa pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika barua aliyomwandikia Rais wake, Mwalimu Julius Nyerere, anaeleza jinsi binafsi alivyoguswa na mauaji ya watu wanaoshukiwa kuwa wachawi katika mikoa ya Shinyanga na Mwanza mwaka 1975.

Kwa maneno yake Mwinyi alisema: “Kisiasa nakiri kuwa nahusika, siwezi kukwepa kwa sababu dhamana yangu ya uwaziri inaambatana na wajibu unaonitaka nijue yanayotendeka wizarani na pia niweze kudhibiti na kuhakikisha mwenendo mwema wa Jeshi la Polisi.”

Mwinyi alijikuta katika matatizo hayo baada ya Jeshi la Polisi kuendesha operesheni ya kusaka wauaji wa wachawi katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga, na alikiri kwamba:

“…vyombo vinavyohusika na utekelezaji, polisi ikiwemo, vilivuka mipaka ya wajibu wao na vikajipa madaraka ya kuogelea katika vitendo viovu vya kishenzi, kinyama na kikatili hata baadhi ya watu waliokamatwa kwa kushukiwa tu kwamba wanahusika wakafa na wengine wakapata vilema vya kudumu.”

Ingawa Mwinyi aliweka bayana kwa bosi wake, Mwalimu Nyerere, kwamba kijinai asingehusika kwani hakushiriki wala kushauri, kuagiza wala kuelekeza mambo hayo yafanywe hivyo, aliandika barua isiyo na kinyongo kabisa na yenye unyenyekevu mkubwa kwa Rais Nyerere.

Kwa unyeyekevu mkubwa, Mwinyi alisema: “Kwa hiyo, Mwalimu, nakuomba mambo matatu. Kwanza naomba radhi mimi nafsi yangu na pia naomba radhi kwa niaba ya askari wote walio wema. Pili, naomba vilevile uelewe sehemu yangu katika kosa hili. Tatu, kwa fedheha hili, naomba unikubalie kujiuzulu.”

Kupatikana kwa barua ya Mwinyi ya kujiuzulu na kuwekwa hadharani inaweka mizania mpya kabisa ya uadilifu katika uwajibikaji wa viongozi wa umma wanapoingia matatani na kutakiwa kujiuzulu.

Miongoni mwa viongozi wakuu waliowahi kujiuzulu katika miaka ya hivi karibuni ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowassa, pamoja na mawaziri wawili waliopata kusimamia Wizara ya Nishati na Madini kwa nyakati tofauti za utawala wa awamu hiyo, Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi.

Viongozi hao, ingawa barua zao za kujiuzulu kwa Rais Jakaya Kikwete hazijapata kuwekwa hadharani, lakini kwa kauli na maelezo yao bungeni wakati wanatangaza kujiuzulu walionyesha kuwa walionewa tu kufikishwa katika hatua hiyo.

Kwa mfano, Lowassa alisema wazi “ameonewa na kudhalilishwa sana” kuhusu suala la mkataba tata wa kuzalisha umeme wa dharura ambao ulitolewa kwa kampuni feki ya Richmond.

Tangu kujiuzulu kwa Lowassa na wenzake wawili, umezuka mpasuko mkubwa miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), vita ikipiganwa kuonyesha kwamba kujiuzulu kwa viongozi hao ulikuwa ni uonevu.

Mivutano hiyo ya wabunge ndiyo ilifanya hata Halmashauri Kuu ya CCM kuunda kamati ya wazee watatu wa busara ikiongozwa na Ali Hassan Mwinyi na wajumbe ni Spika wa zamani wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa, kusaka suluhu ya uhasama huo.

Wakati kamati hiyo ikiendelea na kazi ya kusaka suluhu ya uhasama huo, suala la Richmond ambalo ni chimbuko la kujiuzulu kwa viongozi hao watatu, limezidi kuwa tete kila kukicha, zaidi likijitokeza katika makundi ya wapinga ufisadi na wale wanaolezwa kuutetea.

Kwa barua ya Mwinyi ambayo gazeti hili limeamua kuichapisha ilivyo kwa nia ya kuamsha uadilifu unaofanana na kiongozi huyo wa awamu ya pili, ni fursa nzuri sasa kwa viongozi wote wa umma wanaoachia ngazi si tu kukubali kuachia ngazi, ila kuishi maisha yanaoonyesha kwamba hawana kinyongo na hatua waliyochukua.

Mzee Mwinyi kwa maudhui ya barua yake ya mwaka 1977 haikuwa jambo la ajabu kuja kuwa Rais wa Tanzania miaka minane baadaye, huku akionekana kama kiongozi aliyeshinda vishawishi na kila aina ya hila kwenye uongozi wake.

Rabu, 21 Oktober 2009

Germany worry over 2010 safety

Germany worry over 2010 safety

The German national team
Germany have already qualified for the 2010 World Cup in South Africa

Germany's footballers have been told they may have to wear bullet-proof vests if they leave the team hotel at next year's World Cup in South Africa.

The comments come from the head of security firm BaySecur, who look after the the German Football Federation (DFB) and their guests when the national team play away from home.

BaySecur is one of the firms expected to be employed by the DFB while the team are at the tournament that runs from 11 June until 11 July.

"The possibility for the players of moving outside of the hotel boundaries should be kept to a minimum," BaySecur's Guenter Schnelle told German magazine Sport-Bild.

"Otherwise there must be a full escort: armed security guards and bullet-proof vests for the players."

The DFB is sending its security chief to South Africa to inspect the team's headquarters near Pretoria before deciding if any extra security measures would be needed.

Helmut Spahn, the federation's official in charge of security, will travel to South Africa at the end of this week.

"We will then receive the first security report," DFB spokesman Harald Stenger said Wednesday.

"After a security workshop following the draw on 4 December the federation will receive more information.

"And the will then decide if and what extra security measures it might take on its own to beef up security for the national team and its entourage.

"Any such measures would have to be cleared by Fifa and the South African organizers."

Former German international and the man in charger of team logistic's Oliver Bierhoff says the team will have to get used to certain restrictions.

"We'll have to adjust to a World Cup under different conditions," he said.

"The players won't be able to move so freely as they did 2006 in Germany or 2008 at the European Championship in Austria and Switzerland."


Selasa, 20 Oktober 2009

Hiki ni kituo cha kupiga kura ndani ya jiji la Niamey...Uchaguzi Niger.


Poll worker Reinatou Amadou is handed a voter identity card during voting, in a constitutional referendum that would keep President Mamadou Tandja in power, in Niamey, Niger Tuesday, Aug. 4, 2009. The president of uranium-rich Niger pushed forward Tuesday with a highly controversial referendum on a new constitution that would remove term-limits and grant him another three years in office Ñ this time with increased powers.(AP Photo/Rebecca Blackwell)
Kituo cha kupiga kura mjini Niamey

Wapiga kura wanaitika mwito wa upande wa upinzani na kuususia uchaguzi wa bunge


Uchaguzi wa bunge nchini Niger unaendelea licha ya kususiwa na upande wa upinzani na licha ya miito ya jumuia za kimkoa na kimataifa kumsihi rais Mamadou Tandja aakharishe uchaguzi huo.

Idadi ya wapiga kura ilikua ndogo kabisa vituo vya uchaguzi vilipofunguliwa leo asubuhi.

Uchaguzi huo wa kabla ya wakati umelengwa kuimarisha madaraka ya rais Mamadou Tandja,kanali zamani aliyeingia madarakani kupitia avituo vya upigaji kura mnamo mwaka 1999.

Mhula wa pili wa madaraka ya rais Tandja unamalizika december 22 ijayo,lakini mwanajeshi huyo wa zamani amejifungulia njia ya kusalia madarakani kwa miaka mitatu zaidi baada ya kuitisha kura ya maoni Agosti nne mwaka huu.

Minggu, 18 Oktober 2009

Protect yourselfbefore its too late....

Triage! Will You Be Denied Treatment for Swine Flu?

Swine Flu » 26 August 2009 » In Swine Flu » No Comments


While it may sound like something out of a bad sci-fi movie, it has become our reality. US doctors, in accordance with WHO regulations, have drafted a document deciding who will live and who will be allowed to die when the Swine Flu Pandemic strikes the greater part of North America.

Once Swine Flu has America in its death grip, medical care — including everything from vaccines to respirators to doctors and nurses themselves — will become scarce. So a task force of members from prestigious universities, medical groups, and government agencies (the Department of Homeland Security, the Centers for Disease Control and Prevention, and the Department of Health and Human Services, and World Health Organization) has compiled a list of people who would not be treated.

Those of us most affected by this decision can easily see this as an attempt to “play God” on the part of these doctors who so willingly ignore their Hippocratic oaths, but Dr. Asha Devereaux, a critical care specialist and lead writer of the task force report, called the guidelines a “blueprint for hospitals so that everybody will be thinking in the same way.”

It’s being recommended that every hospital choose a triage team to decide who will get lifesaving treatment and who will not, but the guidelines already spells out those who will be denied care. They include:

People older than 85

People with severe trauma, such as critical injuries from car crashes and shootings

Severely burned patients older than 60

People with severe mental impairment, such as advanced Alzheimer’s disease

People with severe chronic disease, such as advanced heart failure, lung disease or poorly controlled diabetes

Others who are at a high risk of death or have a low chance of long-term survival would also be unlikely to receive medical care.

The guidelines will clearly violate laws against age discrimination and disability discrimination, according to public health law expert Lawrence Gostin of Georgetown University. Gostin also called the report “a political and legal minefield.”

Though most experts acknowledge that health care will, in fact, need to be rationed once Swine Flu infections begin, the current list will basically single out the poor blacks, Mexicans, homosexuals, non-English-speaking peoples and any others who are generally considered as undesirables in America. Because in addition to this list, the triage team will, at its discretion, decide on millions of others who will be arbitrarily denied medical treatment.

As for when the guidelines will be enforced, members of the task force said it’s only a matter of time. Phase Five Pandemic Alert means that a pandemic with millions infected, dead, and dying is imminent. It WILL happen!

According to Secretary Michael O. Leavitt, Department of Health and Human Services:

“Forty million people died when the last major influenza pandemic swept around the world in 1918. We have seen two less severe pandemics since then. We will no doubt see another sometime in the future.

We don’t know when, and we don’t know how bad it will be. But we know it will happen sooner or later and that what we do now will save lives – maybe millions of lives – in the future.”

How did this happen? How did we get to the point where we allowed an engineered virus to be released onto an unsuspecting population – then in the face of imminent death – we are being told that our job is to die.

Don’t allow this fate to happen to your family. The triage experience will not be just about the color of your skin. You may be denied treatment just because someone doesn’t like you or in your haste to get treatment for your loved one, you may become momentarily rude.

Any little thing can mean life or death for someone you love.

Protect your family today before it is too late.

njia 7 zinazoweza kusaidia kuepuk amafua ya nguruwe

This time of year I usually have stopped taking Echinacea, but it is my first port of call to build up my defences and if you can get Echinacea tincture that is the most effective in my opinion. Boots produce their own and there is an excellent one made by Bioforce from helath stores. Take it daily for three weeks then a week off.

2 Next increase the amount of vitamin C you are taking, at least 1 gram a day in two 500mg doses is the most effective. Have as natural and unprocessed diet as you can, and juicing your fruit and vegetables gets you the maximum vitamins from them.

3 Your body requires oxygen for every cell to function properly because viruses can neither survive nor thrive in it. Therefore, the best defence against microbes, germs, harmful bacteria and viruses, such as the swine influenza virus, is to keep the body oxygenated. Add in eggs to your diet as they are excellent for improving your oxygen absorption. See the healthy bites item on eggs below.

4 Are you breathing deeply enough? Shallow breathing will not bring enough oxygen into so your system, and being out in the fresh air every day is a must. Walking at a moderate pace while breathing in for a count of six, and out for a count of six, is one of the simplest ways to do this. If you find a count of six difficult, reduce it to four, or if it becomes easy increase to six or eight.

5 Limit foods and substances that stress the body such as sugar, caffeine, alcohol, smoking, too much red meat and processed foods high in saturated and hydrogenated fats.

6 Increase your intake of green tea, and reduce coffee and tea. Green tea will really help as its antixodants will boost your immune system. Add some lemon to it and you get extra vitamin C as well.

7 Finally, go back to basic hygiene and wash your hands in hot soapy water frequently and carry hand gel when you are out and use it after contact with others such as a handshake – and contact in public places with stair rails, lift buttons and so on.

It may all seem like a nonsense, but people have died from not taking this seriously. The good habits outlined here will help protect you, and if you maintain them you will have a solid barrier to prevent future infection.

Mafua ya nguruwe yaingia Chuo Kikuu cha Urafiki Lumuba.

Mafua ya nguruwe yaingia Chuo Kikuu cha Urafiki Lumuba. wanafunzi zaidi ya 50 wapo hospitali wamelazwa kutokana na athari za ugonjwa huo. kati ya hao wapo watanzania wasiopungua 7 ambao tayari wamelzwa kutokana na ugonjwa huo. tahadhari chuoni bado haijatolewa chuoni hapo kukiwa na uvumi kwamba yeyote atakayetoa taarifa za mlipuko wa ugonjwa huo anaweza kufukuzwa chuo,,,, hali ni mbaya na watu wengi wanatembea wakiwa wamevaa MASK, kutembeleana, makundi makundi inabidi yaepukwe ili kupunguza kasi ya maambukizo

Sumaye atema cheche, aunga mkono vita dhdi ya ufisadi ndani ya CCM

Sumaye ahamasisha wabunge kuendelea kuibua hoja


BAADA ya kimya cha muda mrefu, Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye ameibuka kuunga mkono mijadalaNa inayotokea bungeni na kuwataka wabunge waendelee kuibua hoja zaidi kwa manufaa ya taifa.

Kauli hiyo ya Sumaye imetolewa wakati tayari kuna mgawanyiko miongoni mwa wabunge, huku baadhi wakionekana kuwa mashujaa na wapambanaji wa ufisadi, wengine wakipinga na kutaka wachukuliwe hatua.

Hali hiyo imesababisha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), kuunda kamati ndogo ya watu watatu wenye hekima chini ya Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, kufuatilia mwenendo wa wabunge na wanachama wake wanaoonekana kwenda kinyume na matakwa ya CCM.

Kabla ya kuundwa kwa kamati hiyo katika mkutano wake wa hivi karibuni mjini Dodoma, NEC ilimhoji Spika wa Bunge ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta kwa maelezo kuwa amekuwa akiruhusu mijadala inayoikosoa serikali na CCM.

Spika Sitta amekuwa akitajwa kama kiongozi wa kambi ya wabunge wa CCM bungeni, ambao wamekuwa wakijipambanua kama makamanda wa vita ya ufisadi baada ya matokeo ya Ripoti ya Uchunguzi ya Bunge kuhusu mkataba wa Richmond, ambayo ilimfanya Edward Lowassa, kujiuzulu mwezi Februari mwaka jana.

Wabunge wengine waliopo katika kundi hilo ni Mbunge wa Same Anne Killango, Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Lucas Selelii wa Nzega. Wengine ni Christopher Ole Sendeka wa Simanjiro na James Lembeli wa Kahama.

Hata hivyo, CCM ilieleza kugundua kuwepo kwa chuki miongoni mwa wabunge wake ndani ya bunge na Rais Kikwete akizungumzia hilo kwenye mazungumzo yake ya moja kwa moja na wananchi Septemba, mwaka huu.

CCM imeipa kamati ya Mwinyi ambayo wajumbe wake ni pamoja na Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa kuchunguza kiini cha chuki miongoni mwa wabunge hao.

Akizungunza na Mwananchi Jumapili hivi karibuni, Sumaye alisema mijadala hiyo iendelee na kuwataka wabunge kutoogopa kuibua bungeni mijadala yenye masilahi ya taifa kwa sababu kufanya hivyo ni kukuza demokrasia nchini.

Sumaye alisema kuwa kutokea kwa mgongano wa mawazo baina ya wabunge ni hali ya kawaida na kwamba, hata lingekuwa bunge la chama kimoja, hali hiyo ingeweza kutokea kwa kuwa kila mmoja ana mawazo tofauti na mwingine.

"Mijadala na migongano ya mawazo bungeni ni jambo la kawaida, hata kama lingekuwa bunge la chama kimoja ingeweza kutokea.

Hali ya namna hiyo ni kukua kwa demokrasia hivyo sioni mantiki ya wabunge kuacha kufanya hivyo, nawashauri waendelee," alisema Sumaye.

Mwanasiasa huyo ambaye alishikilia nafasi ya Uwaziri Mkuu kwa kipindi kirefu zaidi ya wote enzi za utawala wa awamu ya tatu wa Rais Benjamin Mkapa, alibainisha kuwa anapoliangalia bunge la Tanzania anaona kuna dalili ya kugawanyika.

"Ninapoliangalia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naona kuna kila dalili ya baadhi ya wabunge kugawanyika," alisema Sumaye.

Alipoulizwa kama anafahamu kuwepo kwa baadhi ya wabunge ndani ya CCM wanaolalamikiwa kwa vitendo vya ufisadi na wananchi wa majimbo yao alisema: "Sifahamu kama kuna wabunge mafisadi walio ndani ya CCM".

Kuhusu kuwepo baadhi ya wabunge wa chama tawala kulalamikiwa kwa kushindwa kuwaletea maendeleo kama walivyoahidi, pia Sumaye alisema haamini kuwepo kwa jambo kama hilo.

Hata hivyo alisema iwapo kuna wabunge wameshindwa kuwaletea maendeleo wananchi, CCM isihusishwe na kushindwa kazi kwa wabunge hao.

Alisema kuwa wabunge wasiotimiza wajibu wao watahukumiwa na wananchi wenyewe kwa njia ya kura na kwamba, CCM bado ni imara katika kila nyanja.

Kama kuna mbunge hajatimiza ahadi zake basi hilo litakuwa tatizo lake na siyo la chama. Chama hakihusiki," alisema Sumaye.

Akizungumzia mustakabali wake kisiasa, Sumaye ambaye alikuwa Mbunge wa Hanang mkoani Manyara alisema tofauti na mawazo ya wengi kuwa yeye anataka kurejea katika siasa, lakini ukweli ni kuwa hatarajii kufanya hivyo.

"Pamoja na uwepo wa minong'ono kuwa nataka kurejea katika siasa na kugombea tena ubunge Jimbo la Hanang, habari hizo siyo za kweli. Sitarajii kuingia tena katika siasa zaidi ya kuwa mshauri endapo nitahitajika kufanya hivyo kwenye CCM," alisema Sumaye.

Alifafanua kuwa yeye alistaafu wakati bado anahitajika na wananchi wa Hanang pamoja na Watanzania kwa ujumla, pia bado ana afya njema itakayomwezesha kuendelea kuwatumikia wananchi na kusisitiza kwamba, hajawahi kufikiria kurejea katika siasa zaidi ya kujikita katika kilimo nyumbani kwake.

Hata hivyo Sumaye aliyekuwa mmoja wa wagombea kumi na moja wa nafasi ya urais mwaka 2005 ndani ya CCM na kuangushwa na Rais wa sasa Jakaya Kikwete alisema: "Si dhambi kwa kiongozi yeyote aliyestaafu kutamani na kurejea tena katika siasa kwani hajavunja sheria za nchi na pia kila mtu ana mtazamo wake katika muktadha wa kisiasa".

"Mimi nimestaafu siasa wakati bado nahitajika na wananchi wa Hanang na Watanzania kwa ujumla, lakini sitarajii kurejea tena katika siasa. Kama nitahitajika kutoa mchango wangu wa mawazo nipo tayari ili kuijenga nchi yetu," alisema Sumaye.


Ndesamburo anunua helkopta mbili za kampeni Chadema

Ndesamburo anunua helkopta mbili za kampeni Chadema
Mbunge wa Moshi Mjini,Philemon Ndesamburo(Chadema), amenunua helikopta mbili za kampeni.

*Zitaanza uchaguzi wa serikali za mitaa

Â

Boniface Meena, Moshi

Â

MBUNGE wa Moshi Mjini,Philemon Ndesamburo(Chadema), amenunua helkopta mbili kwa ajili ya kukisaidia chama hicho katika kampeni za chaguzi mbalimbali hapa nchini.

Â

Moja ya helkopta hizo tayari iko hapa nchini na nyingine itawasili Jumatatu (kesho) na tayari mbunge huyo ameshapata vibali vya kuziruhusu helkopta hizo kutumika hapa nchini.

Â

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Ndesamburo alikiri kuwa amenunua helkopta hizo, ili kukipunguzia chama chao gharama kubwa za kukodi wakati wa kampeni.

Â

Hatua hiyo ni kubwa zaidi kwa Chadema, chama ambacho kimekuwa kikijitahidi kujiimarisha na kuongeza nguvu hasa wakati wa uchaguzi.

Tangu mwaka 2005 wakati wa Uchaguzi Mkuu, Freeman Mbowe alipogombea urais kwa mara ya kwanza, chama hicho kilitumia helkopta ya kukodi.

Hata katika baadhi ya chaguzi ndogo za ubunge zikiwemo za jimbo la Busanda na Tarime, chama hicho kilitumia helkopta za kukodi kwa ajili ya kufanyia kampeni.

Lakini safari hii, chama hicho kimeamua kumiliki helkopta yake huku Ndesamburo akisisitiza: “Vibali vyote nimeshapata kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga na vile vile vya kuitoa hiyo moja Nairobi na kuifikisha hapa Jumatatu”.

Â

Alisema kuwa helkopta hizo zitaanza kufanya kazi katika kampeni za serikali za mitaa katika majimbo yote ya Mkoa wa Kilimanjaro na baadaye katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Â

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana ni kuwa Chadema imesimamisha wagombea zaidi ya robo tatu katika kila jimbo mkoani Kilimanjaro.

Â

Katika Jimbo la Moshi Mjini, chama hicho kimesimamisha wagombea 60Â na Jimbo la Rombo kimesimamisha wagombea 52.

Â

Uchaguzi wa serikali za mitaa unatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo huku idadi ya wapigakura ikiwa ndogo kinyume na matarajio.

Hali hiyo imesababisha baadhi ya vyama kujipanga kikamilifu ili kuhakikisha wanakwepa kile wanachoita hujuma dhidi ya CCM.

Uchaguzi huo ni muhimu kwa vyama vya siasa kujipatia mtaji na kujiimarisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, ambao unatarajiwa kuwa na mchuano mkali.

Viongozi wa serikali za mitaa wana nguvu na ushawishi mkubwa wa kimaamuzi katika uchaguzi mkuu wa wabunge na Rais, kwani wapigakura wengi wako kwenye maeneo yao.

Pia ngazi ya uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu katika maamuzi ya maendeleo ya nchi kutokana na watu wengi kuishi vijijini ambako pamoja na mambo mengine kuna shughuli nyingi muhimu za uchumi hasa kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa taifa.

Sabtu, 17 Oktober 2009

bilionea wa kitanzania kuenda mwezini

Picture of the Day
'Fly our flag to the outer space'
President Jakaya Kikwete placing the National flag to Mr Ashis Thakkar, Uganda-based businessman who is on course to travel to outerspace on board the Virgin Galactic's first flight to space early next year. The 28-year-old millionaire will fly the Tanzania flag on the space shuttle as a tribute to his Tanzanian mother who was born and raised in Mwanza. (Photo by Muhidin Issa Michuzi).
President Jakaya Kikwete placing the National flag to Mr Ashis Thakkar, Uganda-based businessman who is on course to travel to outerspace on board the Virgin Galactic's first flight to space early next year. The 28-year-old millionaire will fly the Tanzania flag on the space shuttle as a tribute to his Tanzanian mother who was born and raised in Mwanza. (Photo by Muhidin Issa Michuzi).

Mtanzania kuandika historia mwezini

ASHISH Thakkar anatarajia kuwa Mtanzania wa kwanza kwenda mwezini wakati atakapofanya safari hiyo mwakani.

Mtanzania huyo, ambaye ni chotara wa Kiingereza alienda Ikulu jijini Dar es salaam jana kumueleza Rais Jakaya KIkwete kuhusu safari yake na kumuaga.

Thakkar, ambaye mama yake ni mzaliwa wa Mwanza na baba Uingereza, alimwambia rais kuwa anajisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika, na hasa Tanzania kwenye safari hiyo ya angani.

"Najisikia vizuri kuwa mwakilishi wa Afrika hasa Tanzania ambako mama yangu alizaliwa, na hii itakuwa nafasi muhimu kwetu kujitangaza duniani kote na kuieleza dunia kuwa Afrika tunaweza na tuna maliasili za pekee,"alisema Takkar alipokuwa akizungumza na Rais Kikwete.

Rais alimweleza Mtanzania huyo anatakiwa apige picha nyingi atakapokwenda mwezini kwa ajili ya kujitangaza zaidi na kuinadi sekta ya utalii kwa juhudi zake zote.

Rais Kikwete alimkabidhi mwanaanga huyo bendera ya Tanzania na kusema watu wenye damu ya Tanzania wapo wengi duniani kote, lakini hawajitokezi kuitangaza nchi kama anavyofanya Thakkar.

"Ni nafasi nzuri kujitangaza kwa kuwa hauwezi kufanikiwa katika utalii bila kujitangaza na tunataraji kupitia Thakkar tutatangaza vyema utalii wetu popote atakapokuwa mwanaanga huyu angani na ardhini,’"alisema Rais Kikwete.

serikali yakataa wito wa Zitto kuitaifisha Dowans

Serikali yampuuza Zitto
Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hoja ya kutaifisha mitambo ya kampuni ya Dowans

YASEMA HAINA SERA NA SHERIA YA UTAIFISHAJI

Na Waandishi Wetu

HOJA ya mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe ya kutaka serikali itaifishe mitambo ya kuzalisha umeme ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, imevuta hisia tofauti huku serikali ikisema haitaweza kuitekeleza kwa kuwa haina sera ya utataifishaji.

Kauli ya serikali imekuja siku moja baada ya Zitto kuwaambia waandishi wa habari kuwa serikali haina budi kufumba macho na kutaifisha mitambo hiyo ya Dowans ili kuiondoa nchi katika janga kubwa la ukosefu wa umeme linaloongeza ugumu wa maisha kwa wananchi na kuiingizia serikali hasara kubwa.

"Mitambo ya Dowans ni mizuri kwa kuwa ukiweka gesi na kuwasha tunapata megawati 120, hivyo ni bora itaifishwe ili tuondokane na giza na kushuka kwa uchumi wetu," alisema Zitto katika mkutano wake na waandishi wa habari juzi jijini Dar es Salaam.

Juzi usiku, Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alisema: "Sijaisoma taarifa yake wala kusikia kwenye televisheni, lakini sisi kama taifa tunaongozwa na sera na sheria.

"Siwezi kufikia hapo; kutaifisha mali si mwongozo na sera yetu. Sisi kama taifa hatuna sera za kutaifisha; huo ndio msingi. Kisera si sera ya CCM na hatuna sheria ya kutaifisha mali za wawekezaji. Sheria zinaeleza kutambua utawala wa sheria na kutatua matatizo au migogoro kwa kutumia sheria."

Ngeleja alifafanua kuwa kimsingi serikali ina matatizo na Dowans ambayo yapo mahakamani na ambayo yanapaswa kumalizwa kwa njia ya sheria, si kwa kutaifisha mitambo hiyo na kuongeza kuwa matatizo ya umeme yaliyopo nchini yanatafutiwa ufumbuzi kwa njia sahihi.

Hata hivyo, alisema Zitto kama Mtanzania yeyote ana uhuru wa kutoa maoni yake na kwamba, yeye (waziri) anayatambua na kuyaheshimu.

"Natambua ni maoni yake; nayaheshimu. Kama kuna lolote tutatue kwa misingi ya sheria," alisema Ngeleja alipozungumza katika hafla ya kampuni ya Songas ya kutimiza miaka mitano iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Serikali ilifanya uamuzi kama huo mwaka 1967 wakati wa Azimio la Arusha, ilipotaifisha mali binafsi na kuziweka chini ya miliki ya umma, uamuzi ambao ulikasirisha wawekezaji wengi ambao waliamua kuondoka nchini.

Mbali na mali za wawekezaji, serikali pia ilitaifisha mali za taasisi mbalimbali za kijamii na kidini.

Ghana mabingwa wa dunia vijana

Ghana mabingwa wa dunia vijana

Timu ya Ghana ikiwa imesalia na wachezaji 10 uwanjani ilifanikiwa kuinyuka Brazil katika fainali ya ubingwa wa dunia wa michuano ya vijana walio chini ya umri wa miaka 20.

Ghana, waliompoteza Daniel Addo aliyetolewa nje kwa kadi nyekundu, walicheza soka maridadi ya kujihami kuwanyima ubingwa Brazil waliokuwa wakipewa nafasi ya kutwaa taji hilo la dunia kwa vijana.

Mechi hiyo iliyofanyika Cairo International Stadium, ilimalizika 0-0 katika muda wa nyongeza na Brazil ilikiona cha moto wakati Alex Teixeira alipokosa goli la wazi.

Emmanuel Agyemang-Badu alifunga goli la ushindi kwa Ghana na kuifanya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kubeba kombe hilo.

Pande zote mbili zilikosa mikwaju miwili ya penati kati ya mitano na kuongeza msisimko wa mechi hiyo, hatimaye ikaingia katika hatua ya mikwaju ya nyongeza ndipo Badu alipoipatia Ghana kile kilichokuwa kikisubiriwa na waafrika wengi.

Jumat, 16 Oktober 2009

CCM bado inatokota














Kamati ya Mzee Mwinyi kumkabili Spika Sitta


KAMATI ndogo ya wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyoundwa chini ya Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, kuchunguza kiini cha chuki miongoni mwa wabunge wake ndani ya bunge , pamoja na mambo mengine inatarajia kumhoji Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Spika Sitta amekuwa kiongozi wa kambi ya wabunge wa CCM bungeni, ambao wamekuwa wakijipambanua kama makamanda wa vita ya ufisadi hasa baada ya matokeo ya Ripoti ya Uchunguzi ya Bunge kuhusu mkataba wa Richmond, ambayo ilimfanya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, kujiuzulu mwezi Februari mwaka jana.

Akizungumza nyumbani kwa mzee Mwinyi, jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo inayoundwa na makada watatu wa CCM, Pius Msekwa, alisema kamati yake itaanza kufanya upelelezi wake baada ya kuanza kwa mkutano wa Bunge, unaotarajiwa kufanyika siku 10 zijazo.

Kauli ya Msekwa inakuja kipindi ambacho pia wabunge wake wanaojiita makamanda wa vita ya ufisadi wameonekana kukaidi onyo la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) , lililotolewa katika mkutano uliofanyika Agosti 16 hadi 17, ambalo liliwataka wasizungumze ovyo nje ya vikao vya chama.

Lakini, licha ya kambi hiyo ya wabunge, makamanda wa ufisadi kuendelea kukaidi amri hiyo na kurusha makombora kwa kambi nyingine ya watuhumiwa wa ufisadi, pia wamekuwa wakijihami kwa kueleza umma kwamba, wanahujumiwa majimboni ili wasirudi mwakani.

Hata hivyo, Msekwa alifafanua zaidi kwamba, baadhi ya wabunge nao wanatarajiwa kuhojiwa na kamati hiyo.

NEC ilipokutana mjini Dodoma, iliunda timu hiyo ili kuchunguza tabia iliyozuka miaka ya karibuni ya baadhi ya wabunge wake, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na viongozi ndani ya chama hicho, kutoa matamshi hadharani yenye mwelekeo wa kuchafuana majina na yanayoashiria kuvunjika kwa umoja na mshikamano ndani ya CCM na serikali.

Wabunge ambao wamekuwa wakijinasibu kupambana na ufisadi, lakini pia wakiwa wa kwanza kulia kwa madai ya kuchezewa mchezo mchafu majimboni ni pamoja na Lucas Selelii (Nzega), Dk Harrison Mwakyembe (Kyela), Beatrice Shelukindo (Kilindi), William Shelukindo (Bumbuli), Fredi Mpendazoe (Kishapu), James Lembeli (Kahama) na Anne Kilango Malecela (Same Mashariki).

Lakini Msekwa alifafanua kwamba, kamati hiyo itaanza kwa kwenda Zanzibar wiki ijayo ambako itawachunguza wajumbe wa kamati ya CCM ya Baraza la Wawakilishi, kupeleleza kiini cha matamshi mengine yenye mwelekeo wa kusababisha mgawanyiko ndani ya chama na serikali juu ya hoja ya mafuta.

Msekwa aliweka bayana kwamba, baada ya kutoka Zanzibar watahamishia majukumu yao kwenye Bunge katika mfumo ambao pia utapitia Kamati ya wabunge wa CCM bungeni.

Alisisitiza zaidi kwamba, mfumo wa utendaji wa kamati hiyo ambayo inaundwa pia na Abdulrahman Kinana, hautekelezi kazi zake kwa siri na miongoni mwa kauli watakazozifanyia kazi, ni juu ya wabunge wake waliodai kuhujumiwa na mafisadi.

"Hatupelelezi kimya kimya. Ndiyo maana tunaweka wazi," alisema Msekwa, bila kutaja jina na kuongeza.

"Watachunguza ukweli wa madai ambayo yalitolewa na wabunge kadhaa bungeni kwamba, mafisadi wanatumia fedha kuwatishia maisha na hata kuwahujumu ili wasichaguliwe tena kwenye majimbo yao."

"Tutatafuta ukweli kujua, hivi kweli ni msingi wa ufisadi," alisema Msekwa ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge kwa muda mrefu.

Hata hivyo, aliweka bayana kwamba, kulingana na mfumo wa CCM, hakuna mbunge mwenye hati miliki kwenye jimbo lake na kila baada ya miaka mitano huwa wazi kwa mwana-CCM yeyote kuliwania.

"Ilionekana hii siyo hali nzuri kwa chama chetu, kwa sababu inavunja mshikamano ndani ya chama na serikali," alieleza Msekwa.

Msekwa ambaye pia alitumia muda kutetea uhalali wa kamati hiyo pamoja na umuhimu wa NEC kuiteua, alisema siyo mara ya kwanza kwa CCM kuwachunguza wabunge baada ya kuona mambo yanaenda shaghalabaghala.

Akitoa mifano ya kihistoria, Msekwa alisema mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 1968 wakati wa enzi za serikali ya awamu ya kwanza chini ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Safari ya pili, alisema ni enzi za Mwinyi akiwa Rais, ambako mwaka 1993 wabunge waliibuka na msimamo wa kutaka kuwa na serikali tatu, Tanganyika, Zanzibar na Muungano.

Mwaka 1993 muungano uliingia katika msukosuko mkubwa baada ya kundi la wabunge maarufu kama G55, kutaka kuvunja muungano wa sasa kipindi ambacho Waziri Mkuu alikuwa ni mzee John Malecela, kitendo ambacho kilimchukiza Mwalimu.

Kuhusu utaratibu huo kuonekana kwamba unawafunga midomo wabunge katika kushughulikia mambo yenye maslahi kwa umma, Msekwa alipinga.

"NEC haiwafungi wabunge midomo. Hili liko wazi. Wabunge wanaruhusiwa kuikosoa serikali kwa kadri wanavyoona inafaa. Na hii imekuwa ikifanyika bila kipingamizi chochote," alisema Msekwa.

Aliongeza kwamba, inachofanya NEC ni kutekeleza jukumu la mfumo wa nchi ambapo chama ndicho kinachosimamia serikali, hivyo kina mamlaka ya kusimamia utendaji wa shughuli zote za serikali yake.

Kuhusu uhuru wa wabunge kama unavyofafanuliwa na Ibara ya 100 ya katiba ya Tanzania wa kujadili mambo yote bila kuhojiwa na chombo chochote, alisema:

"Kifungu hiki kinazuia chombo chochote kuhoji maamuzi ya bunge, lakini hakizuii chama kukosoa mwenendo wa mijadala bungeni."

Akizungumzia hoja ya mafuta, alisema kwenye Baraza la Wawakilishi zilikuwepo lugha za kuzusha mgawanyiko ambao serikali ya Muungano, ilielezewa kama mkoloni anayeinyonya Zanzibar.

Msekwa alisema suala hilo liko wazi ndani ya katiba, kwamba mafuta yanasimamiwa na Serikali ya Muungano.