Jumat, 28 Agustus 2009

huku ndo kunogewa na mziki au?

AFANDA SELE

Michael Jackson 'aliuawa', afisa aeleza


Afisa mchunguzi wa vifo huko Los Angeles nchini Marekani ametangaza rasmi kuwa kifo cha Michael Jackson kilisababishwa na mtu mwingine, Jackson alifariki mwishoni mwa mwezi Juni.

Alieleza kuwa kifo chake kilisababishwa na kupewa dawa ya ganzi aina ya propofol, na nyingine ya kutuliza maumivu aina ya lorazepam.

Chembe chembe za dawa nyingine aina nne tofauti pia zilikutwa katika mwili wa mwanamuziki huyo.

Mwandishi wa BBC aliyeko Los Angeles anasema hitimisho hilo linaongeza uwezekano wa kufunguliwa mashtaka ya uhalifu dhidi ya madaktari waliokuwa wakimpatia Michael Jackson madawa hayo.

Kwa mujibu wa nyaraka zilizotolewa hivi karibuni na ofisa huyo mchunguzi wa vifo, daktari binafsi Conrad Murray, aliyekuwa akimtibu Bw Jackson, aliwaeleza polisi alimpatia mwanamuziki huyo dawa aina ya propofol kumsaidia apate usingizi. Dr Murray amekana madai ya uhalifu.

Mazishi ya mwanamuziki huyo yamepangwa kufanyika Septemba 3 katika eneo la Forest Lawn Memorial Park huko Glendale, kitongoji cha Los Angeles, katika shughuli itakayokuwa ya faragha.

Mazishi hayo awali yalipangwa kufanyika tarehe 29 Agosti - siku ambayo angekuwa hai angetimiza umri wa miaka 51.

CCM ana kwa ana na maaskofu Katoliki

Atarajiwa kupoza mtafaruku wa Waraka

Kanisa lasita kumwalika kuwa mgeni rasmi wa hafla

WAKATI mjadala kuhusu waraka uliotolewa na Kanisa Katoliki ukipamba moto, Rais Jakaya Kikwete, leo Jumatano, anatarajiwa kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Mwanza Mhashamu Anthony Petro Mayala (69) atakapokutana uso kwa uso na Maaskofu wote wa Kanisa hilo ambao ndio waliobariki waraka huo.

KINGUNGE Ngombale Mwiru amekuwa mwepesi kuzungumzia waraka wa Kanisa Katoliki kuhusu jinsi ya kuchagua viongozi katika uchaguzi ujao kila mara alipotakiwa kufanya hivyo, na wakati mwingine aliita waandishi wa habari ili atoe msimamo wake, lakini jana alimudu kusema maneno mawili tu; "no comment".

Mbali na Kingunge, katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye Halmashauri Kuu ya chama chake ilipendekeza kuwa viongozi wa dini wakutane na viongozi wa kisiasa kabla ya kutoa nyaraka zake, alitoa kauli kama ya Kingunge, hali kadhalika Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Sera, Uratibu na Bunge) Philip Marmo.

Mwananchi ilikuwa imetaka maoni yao kuhusu tamko la Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kuwa kanisa halitapokea maagizo wala maelekezo wakati wa kuandika nyaraka zake.

Waraka huo ambao umesambazwa na kuuzwa nchi nzima, unaelekeza waumini wa kanisa hilo kuchagua viongozi waadilifu, wapenda amani na wenye kujali zaidi maslahi ya wananchi.

Lakini baadhi ya watu, wakiongozwa na Kingunge wamekuwa

wakiupinga kwa madai kuwa unaweza kuwa hatari kwa amani.

Akiongoza ibada ya mazishi ya Askofu Anthony Mayalla juzi, Kardinali Pengo alieleza bayana kuwa si jukumu la viongozi wa kidini kupokea maagizo na maelekezo ya na wanasiasa wakati wa kutekeleza majukumu yake kwa sababu kufanya hivyo ni kukiuka misingi na maelekezo ya kanisa.

Kardinali Pengo alikwenda mbali zaidi alipotoa maneno yaliyoonekana kumlenga moja kwa moja Kingunge aliposema "wakomunisti siku zote wako mbali na Mungu, afadhali hata ya mapebari wanaamini kuwa Mungu yupo".

Kingunge anajulikana kama mmoja wa waumini wakubwa wa siasa za Kikomunisti na hula kiapo kwa kunyoosha mkono juu tofauti na wanasiasa wengine ambao hushika vitabu vitakatifu vya dini zao wakati wanapoapa.

Mwananchi ilipowasiliana na Kingunge jana kupata maoni yake kuhusu msimamo wa Pengo, alikiri kuwa hana hoja tena katika suala hilo.

"No comment (sina la kusema)," alijibu Kingunge na kukata simu. Kingune amekuwa akisisitiza kuwa waraka huo wa Kanisa Katoliki haufai na kulitaka kanisa liufute.

Na hata kanisa lilipomtaka aeleze ubaya wa waraka huo, aliendelea kusema haufai na kusababisha alaumiwe na viongozi wengi wa dini pamoja na wadau wengine wa masuala ya dini na demokrasia.

Kauli kama ya Kingunge ilitolewa na katibu mkuu wa CCM, Makamba."Sina lolote la kusema katika hilo. Wewe niulize ya CCM.

Kuna kura za maoni za kuwachagua wagombea wa serikali za mitaa," alisema Makamba, ambaye chama chake kiliratibu mkutano na waandishi wa habari ambao Kingunge aliutumia kusisitiza msimamo wake dhidi ya waraka wa Katoliki.

Baadaye Makamba alipozungumza tena na gazeti dada la Mwananchi The Citezen alisema: ÒNdugu yangu kila mtu amemsikia baba askofu, sasa unataka mimi niseme nini? Mimi sibishani naye hata kidogo na siwezi kusema abadilishe msimamo.

''Kimsingi, Mwadhama Pengo ni kiongozi mkubwa sana katika Kanisa Katoliki, siwezi kubishana naye hata kidogo.''

Hoja za kupinga na hata kuunga mkono waraka wa Kanisa Katoliki, zilianzia Bungeni Julai Mwaka huu.

Mjadala huo pia ulijadiliwa kwa hisia tofauti na wanasiasa, wasomi, viongozi wa dini na hata wananchi wa kawaida.

Mzee Kingunge, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na kada anayeheshimika sana ndani ya CCM baada ya kufanya kazi kwa karibu na marais wa awamu zote nne, alionekana kutoa hoja nzito zaidi na hasa alipobeba msimamo wa chama hicho kutaka waraka huo uondolewe.

Kama hiyo haitoshi, CCM kupitia Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec), hivi karibuni, ilitoa azimio la kuwataka viongozi wa dini kukaa na viongozi wa dini ili kushauriana katika suala zima la utoaji wa waraka, ikiwa ni njia ya kuepuka kuvunja mshikamano wa kitaifa.

Lakini juzi, Kardinali Pengo alisema Kanisa Katoliki litaendelea kutoa nyaraka zake bila kuomba baraka kwa serikali na hata chama kwa sababu huo ni wajibu waokatika kufanya kazi ya Mungu.

"Waacheni maaskofu wafanye kazi zao na wasifundishwe kazi kwa maana kuandika waraka ni mamlaka kutoka kwa Mungu na si kwa uwezo wao.

Vyama visilazimishe kwamba ni lazima vitoe ushauri," alisema Pengo katika ibada hiyo iliyohudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete, mawaziri, wabunge na marais wastaafu.

Kardinalo Pengo pia alikemea wale ambao wanaonekana kuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi wakati hata ingekuwa wao ndio walio katika nafasi hizo, wangefanya vitendo hivyo vya wizi wa lami za umma.

Kuhusu kauli hiyo ya Kardinali Pengo dhidi ya vinara wa vita dhidi ya ufisadi, mmoja wa wabunge walio mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya ufisadi, Aloyce Kimaro (Vunjo-CCM) alisema binafsi hana uhakika juu ya suala hilo lakini anajifahamu kuwa moyo wake ni safi.

Lakini alimwelezea Kardinali Pengo kama mmoja wa watu mahiri na wanaohitajika sana katika kuendeleza vita itakayowezesha kuwaangamiza mafisadi ili mali za Watanzania zibaki salama.

Senin, 24 Agustus 2009

Nitapambana na mafisadi hadi kifo

PIKA wa Bunge, Samuel Sitta amesema kamwe hawezi kutetereka katika maamuzi yake, kwa kuwa anaamini kuwa Mungu yuko naye katika kila jambo jema analolifanya.

Akizungumza katika mkutano mkubwa wa hadhara ulioandaliwa na wenyeviti wa makanisa ya Mkoa wa Tabora, katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora jana, Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Magharibi, alisema hatatetereka katika maamuzi yake kwa kuwa anaamini anayatekeleza kwa nia njema.

"Katika maamuzi ninayochukua daima ninaamini kuwa ni mambo mema na ninajua kuwa Mungu peke yake ndiye anayenilinda, kwa hivyo sitatetereka hata kidogo,"alisema Spika Sitta ambaye siku za nyuma aliapa kupambana na mafisadi hadi ushidi upatikane.

Alisema hivi sasa kumeibuka tabia ya baadhi ya watu nchini, kulazimisha yale wanayoyafanya wao yaonekane kuwa ndiyo ya ukweli kabisa hata kama wanayoyafanya ni ya uongo.

"Katika nchi yetu kumeibuka tabia ya waovu wanaosambaza uongo uliopakwa asali, hugeuza uongo huo kuwa ukweli na ukweli kuwa uongo, siwezi kukubaliana nao sababu ni waovu,"alisisitiza kauli ambayo imetafsiriwa kuwa anawalenga wale ambao walitaka avuliwe uanachama wa CCM katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho.

Kauli hiyo iliungwa mkono na mkewe ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Margaret Sitta, ambaye alinukuu kauli ya Askofu Norbert Mtega wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Songea, ambaye alisema kuwa maisha ni mpito na kifo ni faida, alipokuwa akizungumza katika msiba wa baba wa Mbunge wa Peramiho, Jenister Mhagama.

"Kauli ile ya Askofu Mtega tunaichukua na sasa tunaifanya kuwa falsafa ya maisha yetu, kwa maana hiyo kwetu sisi sasa maisha ni mpito tu na kifo kwetu ni faida,"alisema waziri huyo.

Kwa upande wake mume wake (Sitta) alisema taifa linaelekea kubaya kwa sababu baadhi ya watu wanajaribu kulazimisha yale wanayoona kuwa ni sawa na kwamba wanatumia gharama kubwa kufanya hivyo.

Mwenyekiti wa umoja wa makanisa mkoani Tabora, William Lusito, alisema umoja huo umetokana na azimio kuwa nyuma ya Spika na kwamba, hawatakubali kumuona akiyumbishwa na kundi la aina yoyote.

Spika huyo pia alielezea kusikitishwa kwake juu ya hatua ya baadhi ya watu, kusambaza maeneo yasiyokuwa na ukweli kuhusu yeye, wakidai kuwa aliomba radhi kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC).

Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki, aliyasema hayo jana nyumbani mjini Urambo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, akiwa katika ziara yake aliyoianza rasmi jana.

Mamia ya watu wa jimbo hilo, walijitokeza kwa wingi kumlaki mbunge wao.

"Kwa kuwa mimi niliwekwa katika kikao cha kujieleza, mimi ninarudisha swali kwa hao wanaosambaza hayo, waeleze niliomba radhi kuhusu kipi,"alisema.

Alisema hataki kuzungumzia yaliyotokea ndani ya kikao, lakini kwa kuwa kuna watu wamejitokeza kuzungumzia hayo, kuna haja kwa watu hao kueleza sababu za yeye kuomba radhi katika kikao cha siku mbili cha NEC.

"Ninachokisema ni hivi, kwa kuwa kikao cha NEC kimefikia mwisho na chama chetu kikatoa maamuzi ya kuunda jopo la watu watatu wenye busara wakaangalie hali ya Bunge letu, watawahoji wabunge, wanachama na kisha tutayasikia maamuzi yao Oktoba basi ni bora tusubirie matokeo yao,"alisema.

Alisema yeye kama mtu mwenye subira atakuwa mtu wa ajabu mno, kuzungumzia yaliyotokea ndani ya kikao cha NEC na CC na kwamba, kauli na maelezo yanayotolewa na baadhi ya watu kutaka kubadilisha picha halisi ya kile kilichotokea ni upotoshaji na inasikitisha.

"Nasikitishwa na makao makuu ya CCM Dodoma kwa ambavyo wanavyoshughulikia baadhi ya mambo, kwani ingekuwa kwa mara moja, kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Kapteni John Chilligati, ilitosha kumaliza mambo.

Alisema, hata hivyo, inashangaza kuona mambo hayo yanarudiwa wakati yanapaswa kushughulikiwa na na kamati maalumu.

"Inashangaza kuona mara anazungumza Katibu Mkuu, mara anazungumza mwanachama tu wa CCM, tena mambo ambayo ni dhahiri yanayoonekana kuwa ni tuhuma bila ya kuacha vyombo vilivyoundwa na chama vifanye maamuzi yake," alisisistiza Sitta.

"Nimesikitishwa na wakuu wa chama ambao waliruhusu, Chenge (Andrew) na Lowassa (Edward) wapokelewe, lakini wanazuia katibu na mwenyekiti wasinipokee, ingawa wanachama walijitokeza kunipokea, hii ndiyo inatufanya wanachama tuamini kuwa kuna wanachama wenye haki na wasio na haki, hii si dalili nzuri,"alisema.

Alielezea kushangazwa na hatua ya makao makuu ya CCM ya kuuzuia uongozi wa mkoa wake usimpokee.

Alisema hivi karibuni amesikia kauli zilizotolewa na viongozi wakuu wa CCM zikionyesha kuegemea upande mmoja, jambo ambalo si dawa na linaonekana kutotumika kwa busara katika wakati huu ambapo kikao cha NEC kimemalizika .

Hata hivyo, aliwashukuru wanachama wa CCM wa Jimbo la Urambo Magharibi, waliojitokeza kwa wingi kumlaki na akawataka kutokata tamaa na waendelee na moyo huo.

Kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kuwa amekuwa akiendesha Bunge kwa kuwapanga wabunge, alikanusha na kwamba, utaratibu wa Bunge unafahamika.

"Vikao vya Bunge vinaendeshwa kwa taratibu na kanuni, kila mbunge anayetaka kuchangia anapitisha hoja zake kwanza kwa Katibu wa Bunge na au kutoa taarifa kwa katibu huyo, hivyo hakuna ukweli wowote kwamba nimekuwa nikipanga mambo,"alisema.

Spika Sitta juzi huko Urambo alipata mapokezi makubwa baada ya kuwasili jimboni humo ikiwa ni mara ya kwanza tangu apate msukosuko kutoka kwenye vikao vya chama chake.

Mwandishi wetu aliyekuwa huko, alisema Sitta alipokelewa na wapigakura wake wakiwa na pikipiki zaidi ya 100 na kutembea naye kwa maandamano kwa umbali wa kilometa moja.

Kamis, 20 Agustus 2009

Mambo ya bajaji....spare mkononi..

muda ni pesa, kwa hali hii bongo hatuendelei ng'o

Oooh God, Swine flue imeingia Tanzania, I'm scared

Tanzania was yesterday on fresh health alert following confirmed cases of students with the dreaded swine flu at a Dar es Salaam school. The Dar es Salaam Regional Medical Officer (RMO), Dr Judith Kahama, told ‘Daily News’ that six students and two teaching assistants at the International School of Tanganyika in the city had tested positive and treated at the school’s clinic.

She said that the students and the teaching assistants had a recent international travelling history, meaning that they could have been infected on their recent travel from holidays outside Tanzania. She said: “It has only been a week since the students resumed school from holiday and they could have been infected on their recent travel out of the country.”

She added that four of the patients had since been treated and discharged. She, however, did not give the countries to which the students had been but confirmed that they are all foreign students studying at IST.

Dr Kahama said after a closed door meeting discussing the issue with health ministry officials following the reports as they attempted to review the reporting system of those infected and how to strengthen the government’s response to the disease. She said the health ministry officials were to roll out countrywide training on response to the disease.

The Director of the school, Dr David Shawver, stated on the school’s website yesterday that H1N1 flu cases had been mild (similar to the normal flu and not life threatening).

However, the Muhimbili National Hospital Director of clinical services, Prof Andrew Swai, told this paper yesterday, that they had not received any patients, save for three people, a Korean and two British students who were treated and discharged early last month. “We have not received any patients, but we remain on the alert and the quarantine wards are still in service,” said Prof Swai.

According to Dr Shawver, the H1N1 Response Team met yesterday morning to review the situation with medical doctors and an epidemiologist from the Centre for Disease Control. He noted that the doctors advised that the school would remain open.

“H1N1 flu cases have been mild (similar to the normal flu and not life threatening),” he stated. But he informed that some parts of the school’s full programme have been suspended for the moment in order to increase social distancing (avoiding the congregation of students/community members in a confined space).

“School assemblies and the ES Open House scheduled for this week have been postponed or cancelled.” he said. Caution was raised that anyone with a fever should not enter the school’s campus and should seek medical attention immediately.

This latest development could mean that the Government could move from trying to contain the disease to treatment. This means the disease could move from the phase where it can be contained to a level where treatment is the only option.

The school’s Director urged the public not to panic because the H1N1 strain reported was the mild type which clears without treatment. He assured that the IST’s H1N1 Response Team was in control of the situation.

At the same time, he urged students to uphold high standards of hygiene like frequent washing of hands with soap, covering mouth and nose with disposable tissue when coughing or sneezing and avoiding touching eyes, nose and mouth.

The Dar es Salaam city Chief Medical Officer, Deo Mutasiwa, recently said the country was well prepared for the epidemic, that stocks of Tamiflu were satisfactory and that doses had recently been sent out to Zanzibar as well.

The first confirmed case involved a 17-year-old British student who was hospitalised earlier in July in the company of 15 others, detected at Julius Kambarage International Airport and later taken into a quarantine at Muhimbili hospital. He was treated and discharged.

Hali si nzuri ndani ya NEC


Amweka kwenye kipindi cha majaribio
Mengi naye aguswa ndani ya NEC
Ya Mkapa yawatisha wajumbe

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM) amemtega Spika Samuel Sitta ambaye ana muda hadi Novemba mwaka huu kujirekebisha, Raia Mwema imeambiwa.

Mtego huo ambao kwa upande mmoja unapalilia zaidi mpasuko wa ndani baina ya kundi la Sitta na jingine ambalo yeye amekuwa akidai linamtafuta, ulihitimishwa juzi pale Sitta alipotakiwa kujitetea ili asinyang’anywe kadi ya uanachama hatua ambayo dhahiri ingeshusha kila aina ya ndoto aliyonayo.

Baadhi ya wana CCM waliozungumza na Raia Mwema wakirejea Mkutano wa Halmashauri Kuu ya chama hicho ulioanza mwishoni mwa wiki iliyopita wanasema mbali na kumpatiliza Sitta, Kikwete pia aliruhusu kutikiswa kwa mtu wa karibu na Sitta, mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi, ambaye kama Sitta, amekuwa akisema kwamba yumo katika vita dhidi ya ufisadi ili kumsaidia Rais Kikwete anayeiongoza.

Habari za ndani ya CCM kutoka katika vikao rasmi na visivyo rasmi, zinaeleza kwamba Rais Kikwete ameamua, kutumia mtindo wa “kuuma na kupuliza” kwa marafiki zake, Sitta na Mengi kwa kuruhusu mjadala kwenda katika mpangilio ulioandaliwa mahususi kwa ajili ya ‘kuwashughulikia’ Sitta na Mengi, na kwa maana hiyo kundi la wabunge ambalo limekuwa likijitambulisha na Sitta.

Taarifa za ndani zinasema, katika kikao hicho, mbali ya Sitta kujadiliwa, mmoja wa wabunge alibanwa kwa kumshirikisha Mengi katika shughuli za CCM ikidaiwa kwamba mfanyabisahara huyo si mwana CCM.

Hata hivyo, habari zinasema kwamba pamoja na Mengi kuwa mwana CCM na mtu anayekisaidia chama hicho kwa muda mrefu, mfanyabiashara huyo amekuwa karibu na Rais Kikwete na amekuwa akimtaja na kumsifia Rais hadharani.

“Karibu wajumbe 40 walizungumza dhidi ya Sitta. Walikuwa wakitoa wito afukuzwe kwa jinsi anavyoliendesha Bunge ambalo katika siku za karibuni limekuwa likiibana sana Serikali.

“Aliomba sana msamaha, lakini dhahiri hakuna hata mmoja aliyekuwa akimsikiliza, hata wachache waliojaribu kumuunga mkono walizomewa wasiweze kuendelea kusema lolote.

“Kwa hiyo kwa sasa ni kama Sitta yupo katika kipindi cha majaribio. Hatima yake itategemeana na jinsi anavyoliendesha Bunge kati ya sasa na Novemba. Hiyo kamati iliyoundwa imepewa mwanya wa kuitisha kikao cha dharura kama itaona kuwa anakwenda ndivyo sivyo,” anasema mmoja wa wajumbe wa NEC aliyezungumza na Raia Mwema kwa masharti ya kuwa hatajwi kama chanzo cha habari hii.

Mjumbe mwingine aliiambia Raia Mwema kwamba pengine msumari wa mwisho katika jeneza la Sitta utakuwa umepigiliwa na mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru ambaye alimsema Sitta kwamba japo amekuwa akidai kwamba anaendesha Bunge kwa mtindo wa Uingereza (Jumuiya ya Madola), uendeshaji wake haukuwa sawa na huo wa Uingereza.

“Kwanza Ngombale alichanachana Waraka wa Wakatoliki akidai ni ilani ya kisiasa na kwamba haiwezekani nchi ikawa na ilani zaidi ya moja kwa wakati mmoja, kisha akamrukia Sitta.

Yalizungumzwa mengi, pamoja na kumtetea Mkapa (Benjamin) na wapo walioonya kwamba kwa kuruhusu Mkapa kukwaruzwa, Kikwete alikuwa anaandaa kaburi lake mwenyewe,” anasema mjumbe huyo.

Lakini mjumbe mwingine, mfuasi wa kundi moja kati ya makubwa yanayopingana kwa sasa ndani ya CCM ameiambia Raia Mwema hata hivyo kwamba msimamo wa Kikwete katika suala la Sitta unaweza usiwe na maslahi makubwa kwa chama siku za usoni.

“Kikwete anaonekana hataki kuwaudhi marafiki zake wote wakiwamo hata wale ambao alionekana kuwatosa kutokana na kuhusishwa kwao na kashfa mbalimbali ambazo Sitta na kundi lake wamekuwa wakizisemea. Nadhani alipaswa kuwa na msimamo wa wazi katika hili maana linahusu mustakabali wake kisiasa na wa chama chetu.

“Sasa wananchi wana uelewa kuliko wakati mwingine wowote na kwamba mwaka mmoja si mbali kuelekea kwenye uchaguzi mwingine na hii ni hatari sana kama hakutatokea jambo lolote zito,” alisema mwanasiasa huyo katika mazungumzo ya simu kutoka Dodoma alikokuwa akihudhuria vikao hivyo.

Katika vikao vyake vya juu mjini Dodoma vilivyomalizika juzi, CCM imeunda timu ya viongozi wake ndani ya Kamati Kuu yake kuchunguza mwenendo wa uhusiano kati ya chama hicho, Serikali na Bunge, mambo ambayo ndiyo msingi wa tuhuma dhidi ya Spika Sitta na watu walio karibu naye.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Spika za zamani ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na waziri wa zamani, Abdulrahman Kinana ndio wanaounda timu ya kufuatilia mwenendo wa Sitta.

Mkakati uliotumika katika kumjadili Sitta unashabihiana kwa staili na ambayo amekuwa akiitumia Spika huyo kujadili mambo nyeti ndani ya Bunge kwa kuwapanga wabunge anaowaamini, kuzungumza. Haikuweza kufahamika mara moja orodha hiyo ya wazungumzaji iliandaliwa na nani.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa baadaye Sitta alipewa “ushauri wa busara” ili aombe radhi wajumbe hao, ikielezwa kuwa ni hatua ambayo ilikuwa ikiungwa mkono na Rais Kikwete. Kikwete anadaiwa kuunga mkono Sitta kuomba radhi kwa vile hakuwa “tayari kupoteza Spika katika kipindi hiki, na wala CCM haiwezi kupoteza mbunge wakati huu”.

Taarifa zaidi zinasema huu si mwisho wa suala la Sitta na chochote kinaweza kutokea siku za baadaye, huku taarifa nyingine zikieleza kuwa Rais Jakaya Kikwete amekuwa na kikosi kazi cha siri kinachochunguza mwenendo wa kundi hilo.

Inadaiwa kuwa moja ya kazi zilizokwishafanywa na kikosi kazi hicho ni pamoja na kupima upepo wa kisiasa katika Jimbo la Urambo Mashariki, linaloongozwa na Sitta. Kikosi kazi hicho kilipewa jukumu la kukusanya taarifa huru kuhusu Sitta na wale wanaodaiwa kumwandamana kwa mbinu chafu, na kati ya mambo yanayodaiwa yamepatikana ni kutumiwa kwa mmoja wa mawaziri kufanikisha mbinu hizo zinazodaiwa ni chafu.

Sitta ambaye amekuwa akijigamba kwa wanasiasa wenzake akiwataka wawe na ngozi ngumu ya kuhimili mikikiki ya siasa, mikakati iliyosukwa safari hii ndani ya NEC imedhihirika kumtoa jasho na hata kumweka katika mtazamo mpya kuwa anayo kazi kubwa ya kufanya dhidi ya mikakati mingine ijayo.

“Kwa kweli tukubali kuwa hali si nzuri katika chama chetu, si nzuri kwa sababu zimejitokeza hoja za kupingana…hapana hata kidogo, ni kwamba si nzuri kwa sababu nguvu ya fedha imeteka busara za baadhi ya wajumbe wa vikao muhimu kama NEC. Na kama Watanzania wataamua vinginevyo basi vikao hivi vya NEC na hata CC vitazidi kupoteza maana.

“Itakapofikia hivyo, itakuwa hatari zaidi kwa CCM kwani vikao kama hivyo ndivyo vinavyopitisha majina ya wagombea nafasi za ubunge, na urais. Watu wakipoteza imani na wajumbe wa NEC, inayopitisha mgombea urais maana yake chama ndiyo kinang’oka madarakani,” alisema mjumbe mmoja wa CCM, ambaye hakutaka kutajwa jina kuelezea kwa ujumla mazingira ya NEC ya wiki iliyopita.

Kabla ya kuanza kwa vikao vya CC na NEC, ambayo safari hii Rais mstaafu Benjamin Mkapa alihudhuria, miongoni mwa wanachama wa CCM walioonyesha mtazamo wao wa kutaka Sitta ang’oke ni pamoja na Mbunge wa Ukonga, Dk. Makongoro Mahanga, ambaye si tu alimlenga Sitta, bali pamoja na wabunge wengine wanaodaiwa kupiga vita ufisadi.

Siku chache baada ya Bunge kumalizika, viongozi wa wakuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Mwenyekiti Hamadi Yusuf Masauni na Katibu Mkuu, Martin Shigela, walikutana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuwaeleza mambo mbalimbali likiwamo suala la kuwapo baadhi ya viongozi kujipatia umaarufu kwa kudai kupinga ufisadi na kusisitiza kuwa kinara wa vita dhidi ya ufisadi ni Rais Jakaya Kikwete.

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa mjini Dodoma wanaamini kuwa tishio la sasa dhidi ya Sitta linalenga kuzima makali ya Bunge katika mkutano wake ujao, ambako Serikali itapaswa kutoa taarifa kadhaa ikiwamo ya kuhitimisha sakata la Richmond.

Katika mkutano uliopita wa Bunge, taarifa ya Richmond ilikataliwa na Bunge kwa madai kuwa ililenga kuwasafisha watuhumiwa badala ya kutekeleza maazimo ya mhimili huo wa taifa.

Sabtu, 15 Agustus 2009

Kanisa Katoliki sasa lamkabili Kingunge

KIONGOZI WA KANISA KATOLIKI NCHINI TANZANIA Polycarp Kardinali Pengo

KANISA Katoliki nchini limekataa rai iliyotolewa na mwanasiasa mkongwe na Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale-Mwiru (CCM) ya kulitaka limuombe radhi kwa madai ya kumkashifu kwa kumwita fisadi.
Msimamo huo ulitangazwa jana na Msemaji wa Baraza la Maaskofu Kanisa Katoliki (TEC), Padre Modest Katonto wakati alipofanya mahojiano ya ana kwa ana na waandishi wa habari wa gazeti hili. Baraza hilo linaongozwa na Askofu Yuda Thadei Ruwaich.
Padre Katonto alikanusha madai yaliyotolewa na Kingunge wakati akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam juzi kuwa, kanisa lilipata kumwita fisadi kutokana na msimamo wake wa kuupinga waraka wao unaohimiza waumini wake kuchagua viongozi waadilifu.
Badala yake kiongozi huyo alimtaka Kingunge kuchukua uamuzi wa kwenda mahakamani iwapo anao ushahidi na anaamini kwa dhati kuwa, kanisa lilipata wakati wowote kumkashifu.
“Waraka umejieleza wazi wazi kuwa kiongozi atakayechaguliwa, anatakiwa kuwa mwadilifu, bila kujali itikadi ya chama wala dini. Tulichosema anayepinga kuchaguliwa kwa kiongozi mwadilifu na mkweli ana harufu ya ufisadi. Iwapo Kingunge anaona amekashifiwa na ana ushahidi, basi anayo haki ya kushitaki,” alisema padre huyo kwa kujiamini.
Aliendelea kueleza kuwa, kanisa haliwezi kunyamazishwa na mtu au taasisi yoyote kama lisivyotaka kumnyamazisha mtu mwingine yeyote kutoa maoni yake.
“Siasa ni ‘property’ (mali) ya nani? Na ipo kwa ajili ya nani? Haya ndiyo maswali ambayo najiuliza, huku ni kuwanyamazisha watu wengine wasizungumze.
“Ukishaanza kusema wewe usizungumze, yule asiongee, ni kuvunja katiba ya nchi, unapoanza kuwanyima baadhi ya watu wasijishughulishe na siasa, maana yake unafikiri kuwa siasa ni mtaji au ni kwa ajili ya watu fulani au kwa ajili ya viongozi. Hayo ni makosa,” alisema Padre Katonto.
Mbali ya kusisitiza kwamba, hawataki kuingia katika malumbano na mwanasiasa huyo mkongwe au mtu mwingine yeyote, padri huyo alisema, kanisa haliwezi kamwe kutishwa na kauli za wananasiasa kwani kanisa ni jamii, na jamii inaongozwa na katiba ya nchi.
“Waraka umeshatoka, ni jukumu la watu kuusoma na kujadili, ni kama changamoto. Watu wapo huru kutoa maoni kama watakavyo kama wanavyoutazama, na hilo ndilo lengo letu.
“Nasema tena, hakuna mtu mwenye uwezo wa kumnyamazisha mtu mwingine, huu ni udikteta kutaka kuwanyamazisha watu kwa kutumia nguvu au madaraka. Sioni kama Kingunge ana haki au nguvu ya kuliambia kanisa nyamaza.
“Nikiangalia maneno ya wanasiasa wote waliojitokeza kuupinga waraka pamoja na Kingunge mwenyewe, hakuna mahali ambapo wanaonyesha au kujenga hoja kuwa kuna ubaya wa waraka huu. Ni kelele tu... ni maoni tu ya kutaka kupotosha na kusema waraka ni mbaya,” alisema padri huyo.
Alisema kanisa linamshughulikia mtu mzima kimwili na kiroho, haliwezi kumwacha muumini wake mwenye roho safi akae katika mazingira machafu na ya kuteseka, kwani hata vishawishi vya dhambi vinatokana na maisha kuwa magumu.
“Hakuna kiongozi ambaye yupo tayari kuona watu wake anaowaongoza wakinyanyasika. Huwezi kutenganisha maisha ya kiroho na ya kimwili, huwezi, ni lazima vitu vyote viende pamoja,” alisema msemaji huyo wa TEC.
Alisema kanisa limeshangazwa na kelele za baadhi ya wanasiasa wa wakati huu, wanaojitokeza kuupinga waraka huo wakati limekuwa likitoa nyaraka kadhaa mara kwa mara.
“Tumetoa huduma nyingi za kimwili kwa Watanzania bila kujali itikadi na imani zao, sambamba na nyaraka na miongozo inayoongoza huduma hizo, mfano afya, elimu, maji, upatikanaji wa haki kisheria na mengine, lakini utashangaa hakuna kiongozi aliyekuwa akipinga wala kusema kuwa kanisa kutoa huduma hizo ni kuingilia siasa za nchi, lakini tunapotoa waraka wa kumwelimisha mwananchi namna ya kudai haki zake, vita inakuja hapo,” alisema.
Aidha, alipinga madai mengine ya Kingunge kuwa, waraka wao unalenga kuwadhibiti na kuwalazimisha Watanzania kuwachagua viongozi fulani akisema, hakuna mahali penye msisitizo wa namna hiyo.
Alisema badala yake, waraka huo unalenga kuwapa raia wenyewe nguvu za kumhoji, kumuuliza hata kumwajibisha kiongozi wao kwa yale aliyoahidi na ambayo hakuyatekeleza.
“Nia ya maaskofu ni kuwapa raia wenyewe nguvu ya kuwahoji watawala wao, juu ya utekelezaji wa ahadi zao. Watu watakuwa na uwezo wa kuwadhibiti watu kwa kutoa elimu ya uraia na si kwa kutumia jeshi na vifaru,” alisema.
Aliongeza kuwa, kwa sasa kanisa linaona kama hoja hiyo ya waraka imegeuzwa na baadhi ya watu na kufanywa ya kulijadili kanisa, jambo alilosema si zuri.
Majibu hayo ya kanisa yamekuja baada ya Kingunge, kulitaka kanisa kumuomba radhi, ikiwa ni pamoja na kupinga hatua ya kuandaa waraka huo, akisema uamuzi huo unaweza kuliingiza taifa katika mgawanyiko wa kidini, na hivyo kuharibu misingi ya umoja na mshikamano iliyojengwa na waasisi wa taifa hili.
Kingunge ambaye mwenyewe alitamba kuwa miongoni mwa watu walioijenga misingi hiyo iliyokuwa ikizuia masuala ya dini kuhusishwa na siasa, alilitaka Kanisa Katoliki kutafakari upya uamuzi wake huo na akayaasa madhehebu na watu wa imani tofauti kutofuata mkondo huo.

Canada kuchangia bil. 201/- kuendeleza elimu

SERIKALI ya Canada inakusudia kuendeleza sekta ya elimu nchini kwa kuchangia sh bilioni 201 katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo katika Ubalozi wa Canada nchini Tanzania, Sam Landon, alisema hayo juzi jijini Dar es Salaam wakati wa utoaji wa tuzo ya fasihi ya Kiafrika ya Burt kwa waandishi wa hadithi za watoto.

Makamba apata pigo jingine

USHAHIDI uliowasilishwa katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, na Mbunge Halima Mdee, kuthibitisha tuhuma dhidi ya Yusuf Makamba kwamba amekuwa akimlinda Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Salum Londa, katika tuhuma za ufisadi ikiwamo ugawaji viwanja eneo la Kawe, Dar es Salaam, msingi wake ni mpasuko wa madiwani wasioridhishwa na mwenendo wa meya huyo, Raia Mwema imebaini.
Imebainika kuwa, madiwani hao waliwahi kumwandikia barua Katibu wa CCM, Wilaya ya Kinondoni na nakala yake kufikishwa kwa Katibu Mkuu wa CCM- Taifa, Yusuf Makamba. Barua hiyo ni yenye kumbukumbu namba MAD/MK/01/08, ya Januari 24, mwaka 2008, inatoa ufafanuzi wa tuhuma za ubadhirifu na uongozi mbovu wa Manispaa ya Kinondoni, ikierejea barua ya awali, yenye kumbukumbu namba MAD/MK/01/08.
Inaelezwa kuwa baada ya madiwani kuchoshwa na kile kinachoelezwa kuwa ni "kumlinda" Meya Londa kwa gharama za walipa kodi wa manispaa, barua hiyo ambayo Raia Mwema imepata nakala yake, iliainisha tuhuma 10 dhidi ya Londa na kuhitimishwa kwa maelezo makali: "Kwa haya machache yanathibitisha kwamba Mstahiki Londa ameshindwa kusimamia utawala bora ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni."
Barua hiyo pia inaeleza ari ya madiwani hao kutaka kuitwa kwa Katibu wa CCM - wilaya na ngazi ya taifa ili kueleza kwa kina madhambi ya Londa ikisema; "Mheshimiwa Katibu utambue kuwa tunayo ya kuzungumza katika kikao ambacho chama mtatuita, lakini kwa haya machache yanathibitisha nani mbabaishaji."
Miongoni mwa tuhuma zilizoelezwa katika barua hiyo ni kuhusu kile kilichoelezwa kuwa; "Madiwani kugundua Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni imegubikwa na wizi wa mali unaotokana na vitendo vya kughushi nyaraka za malipo (payment vouchers).
"Juni, 2007, kwenye kikao cha bajeti tulipitisha kasma (fungu) ya kununua matrela 25 ya kubebea taka kwa thamani ya Sh milioni nane, kila moja baada ya zabuni kutangazwa na mshindi kupatikana. Lakini watendaji wa manispaa wakiwa na baraka za Mstahiki Londa walighushi nyaraka na kuongeza bei kutoka milioni nane hadi milioni 12. Matrekta hayo yakaagizwa tena kwa Sh milioni 15.5.
"Katika kikao cha kamati ya madiwani ya chama (CCM) Januari 7, mwaka 2008, Londa alitetea malipo hayo akidai walipwaji walisahau kuweka Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) walipowasilisha zabuni yao. Swali la kujiuliza hapa ni je, tangu lini VAT ikawa asilimia 50?''
Tuhuma nyingine inahusu ununuzi wa magari, ikidaiwa kuwa magari 15 aina ya Suzuki yalinunuliwa bila kuzingatia taratibu za ununuzi zinazotaka zabuni itangazwe kwanza na kuwa na profoma zaidi ya tatu.
Sehemu nyingine ya tuhuma katika barua hiyo inahusu uuzaji wa mali chakavu ya Manispaa ya Kinondoni na barua hiyo inaeleza; ''Mstahiki Londa aliamuru gari alilokuwa akitumia aina ya Toyota Land Cruiser GX ambalo lilikuwa kwenye orodha ya kupigwa mnada, likarabatiwe kwa kiwango cha juu kwa fedha za Manispaa na matengenezo yaligharimu Sh milioni 9, baada ya matengenezo hayo alilazimisha auziwe gari hilo kwa sh milioni 3.
''Ingawa ameshindwa kununua gari hilo baada ya madiwani kuja juu na kuzima njama zake, ameitia hasara Manispaa ya Kinondoni ya kiwango hicho cha pesa (sh milioni 9) wakati akijua mali chakavu zinazotakiwa kuuzwa hazistahili kukarabatiwa upya kwa fedha za umma''.
Kuhusu mgogoro wa kiwanja namba 695 na 696 ambao ndio umemhusisha Makamba baada ya Mbunge Mdee kudai kuwa amekuwa akimlinda Meya Londa tangu akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, madiwani hao wanasema; ''Mgogoro huu ulijitokeza katika eneo hilo ambalo liliuzwa na Mstahiki Salum Londa kwa Ishik, ilibainika kuwa kiwanja hicho ambacho kimemegwa na kupewa Ishik kilikuwa mali ya Manispaa ya Kinondoni.
''Ishik ilibidi alipe kwa kujenga madarasa kwa kulipa fidia hiyo kwa Manispaa, lakini zimekuwapo taarifa chafu zinazohusisha mchezo mchafu katika kummegea Ishik kiwanja hicho mali ya Manispaa, mchezo unaomhusisha Londa moja kwa moja''.
Mwishoni mwa mkutano uliopita wa Bunge, Spika Samuel Sitta alitoa uamuzi unaomtaka Mbunge Halima Mdee kutomwomba radhi Makamba na Londa kwa matamshi yake yanayoashiria kuwa wamekuwa wakilinda na kushirikiana kwenye mchezo mchafu wa utoaji viwanja namba 695 na 696.
Kwa mujibu wa madiwani wa Manispaa ya Kinondoni, wengi wao wameonyesha kufurahia 'hukumu' hiyo wakibainisha kuwa imewasilisha kilio na malalamiko yao ya muda mrefu.
Katika madai yake, Mdee alidai kuwa Makamba akiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, alimlinda Mstahiki Meya Salum Londa kwenye sakata la uuzaji wa viwanja namba 695 na 696 vilivyopo eneo la Kawe Ukwamani.
Alidai kuwa Yusuf Makamba, ambaye kwa sasa ni Mbunge na Katibu Mkuu wa CCM na Mstahiki Meya Salum Londa walishiriki kwenye vitendo vya kuhusiana na uuzaji wa viwanja hivyo na watendaji wa halmashauri walihamasishwa ili kuficha ukweli wa mambo hayo.
Kutokana na madai hayo, Makamba na Londa waliwasilisha malalamiko kwa Spika licha ya kukanusha wakitaka Spika achukue hatua ili Halima Mdee athibitishe madai yake.
Alisema Spika kuhusu suala hilo : '' Malalamiko yalipelekwa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge. Desemba 31, 2008, kabla ya kamati haijaanza kazi ya kusikiliza shauri hili, nilipokea barua kutoka kwa Makamba akiomba kuyaondoa malalamiko yake na kutoa sababu kuwa amekwisha kuyasahau machungu aliyoyapata kutokana na kauli ya Mdee''.
Mara baada ya Makamba kutoa malalamiko yake, siku kadhaa baadaye Londa naye aliondoa malalamiko yake na hivyo Spika kuamua kuwa aliyelalamikiwa (Mdee) hana sababu ya kuomba radhi na matamshi yake yabaki kama alivyotamka ndani ya Bunge.
Habari za ndani ya CCM zinaeleza kwamba, Makamba na Londa walibaini mapema kwamba watabwagwa na Mdee katika kesi hiyo kutokana na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kuongozwa na Mbunge Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, ambaye amejijengea heshima kubwa kupambana na ufisadi.
Mbali ya kamati hiyo kuongozwa na Kilango, ushahidi ambao kina Makamba walibaini kuwa umewasilishwa katika kamati hiyo, ulikuwa na nguvu na hivyo kuamua kuondoa shauri hilo haraka kuepuka kudhalilishwa zaidi ikiwa kesi hiyo ingesikilizwa.
Wajumbe wengine wa Kamati ni Christopher ole Sendeka (CCM-Simanjiro), Ali Ameir Mohammed (CCM-Donge –Unguja), Abdulkarim Shaha (CCM-Mafia).
Wengine ni William Kusila (CCM-Bahi), Charles Keenja (CCM-Ubungo), Fatma Fereji (CUF-Baraza la Wawakilishi), Maulida Komu (Viti Maalum-CHADEMA) na Fatuma Maghimbi (CUF-Chakechake-Pemba).
Maamuzi yaliyotolewa na Bunge yameelezwa kulenga kurudisha imani ya wananchi kwa CCM, baada ya wana CCM wengi kusema kwamba chama hicho kitakuwa kinafanya mzaha mtupu kujieleza kwa umma kuwa kinapiga vita ufisadi wakati kivitendo inalinda mafisadi.

Sabtu, 08 Agustus 2009

Marekani na Afrika Kusini zakubaliana kufanya mageuzi Zimbabwe


Marekani na Afrika Kusini zakubaliana kufanya mageuzi Zimbabwe


Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, Hillary Clinton
Makubaliano hayo yamefikiwa leo kati ya Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani na mwenzake wa Afrika Kusini, Maite Nkoana-Mashabane.


Marekani na Afrika Kusini zimekubaliana kufanya juhudi za pamoja kubadilisha demokrasia, uhuru na ustawi wa Zimbabwe. Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, Hillary Clinton katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Pretoria uliohudhuriwa pia na Wanziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Afrika Kusini, Maite Nkoana-Mashabane.
Bibi Clinton amesema nchi hizo mbili zinafanya kazi pamoja kuhakikisha kuwa mfumo wa kidemokrasia wa Zimbabwe unafanyiwa mageuzi. Ahadi hiyo ya kufanya kazi pamoja inaonyesha dalili nzuri baina ya Marekani na Afrika Kusini, baada ya kutokuwepo mahusiano mazuri katika miaka ya hivi karibuni wakati wa utawala wa Thabo Mbeki, kutokana na makubaliano ya Zimbabwe, kupiga vita ugonjwa wa Ukimwi na kitendo cha Marekani kuivamia Iraq.
Marekani imekuwa mkosoaji mkubwa wa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, huku ikishinikiza kufanyika mageuzi kadhaa chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ambayo waziri wake mkuu, Morgan Tsvangirai, ni kiongozi wa zamani wa upinzani. Kwa pamoja Marekani na Umoja wa Ulaya zimemuwekea Rais Mugabe vizuizi vya kusafiri kwenda katika nchi hizo na kutaka kuzuiwa kwa mali zake.
Bibi Clinton amesema kuwa wanakusudia kuwalenga viongozi wa Zimbabwe kwa kuwawekea vikwazo ambavyo havitawaathiri wananchi wake. Ameongeza kuwa kabla ya vikwazo hivyo havijaondolewa na kuruhusu kupelekwa kwa misaada, Marekani inataka kuona kuwa Zimbabwe inafanya mageuzi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Waziri huyo wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani, amesema kuwa Afrika Kusini inafahamu vizuri changamoto zilizosababishwa na mzozo wa kisiasa nchini Zimbabwe, kwa sababu Afrika Kusini ina wakimbizi milioni 3 wa Zimbabwe. Msimamo wa rais mpya wa Afrika Kusini, Jacob Zuma umeonyesha matumaini ya kuwepo kwa uhusiano imara baina ya nchi hizo mbili na Bibi Clinton kesho anatarajia kukutana na Rais Zuma.
Aidha, Bibi Clinton amesema kuwa Rais Barack Obama wa Marekani, amekuwa na hamu kubwa ya kufanya kazi kwa karibu na Zuma pamoja na Afrika Kusini kwa ujumla. Akizungumzia uhusiano uliopita baina ya utawala wa George W. Bush na Mbeki, Waziri Nkoana-Mashabane, amesema kuwa nchi hizo zimekubaliana kuimarisha uhusiano wao katika masuala mbalimbali kitu ambacho hakikufanyika miaka minane iliyopita.
Baadaye leo, Bibi Clinton atamtembelea Rais wa Zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na kutembelea kituo cha mradi wa Ukimwi. Bibi Clinton yuko Afrika Kusini katika kituo chake cha pili cha ziara yake ya mataifa saba ya Afrika akitokea nchini Kenya na anatarajiwa kuondoka nchini humo keshokutwa Jumapili, na kuendelea na ziara yake katika nchi za Angola, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Nigeria, Liberia na Cape Verde. Ziara hii ya siku 11 ni ziara ndefu kufanywa na Bibi Clinton tangu achaguliwe kushika wadhifa wake huo.

Rabu, 05 Agustus 2009

Mambo ya maji....




Mahasimu wa kisiasa Madagascar kukutana uso kwa uso

Viongozi hao, Rais wa muda Andry Rajoelina na Marc Ravalomanana, wanakutana kwa mazungumzo nchini Msumbiji.

Mahasimu wa kisiasa wa Madagascar wanakutana hii leo kwa mara ya kwanza mjini Maputo, Msumbiji, tangu kiongozi wa upinzani nchini humo, Andry Rajoelina alivyochukua madaraka baada ya Rais Marc Ravalomanana kuondolewa madarakani, hivyo kuchochea mkwamo wa kisiasa kwa miezi kadhaa. Ajenda kuu ya mazungumzo hayo ni kuhusu mzozo wa kisiasa katika kisiwa hicho.
Ravalomanana aliyewasili hii leo nchini Msumbiji na Rajoelina aliyewasili jana usiku, hawajazungumza na waandishi wa habari. Mahasimu hao wa kisiasa mapema leo walikutana kila mmoja kwa muda wake na mpatanishi wa mazungumzo hayo Rais wa zamani wa Msumbiji, Joaquim Chissano, ambapo jioni hii watakuwa na mazungumzo ya kwanza ya ana kwa ana. Katika vikao hivyo vya awali, mahasimu hao walitaarifiwa juu ya mkutano wa leo.
Mjumbe wa timu ya wapatanishi wa Umoja wa Mataifa, Tiebele Drame, amesema kitendo cha viongozi hao wa kisiasa kukubali kuhudhuria mazungumzo hayo ni dalili njema na kupongeza hatua hiyo baada ya vikao kama hivyo kuvunjika. Drame, amesema kinachosubiriwa kwa sasa ni kuona kuwa viongozi hao wa Madagascar wanapata suluhu ya mzozo huo wa kisiasa. Mazungumzo hayo ya siku nne yatawahusisha pia marais wa zamani wa Madagascar, Didier Ratsiraka na Albert Zafy. Wanasiasa hao wanaviwakilisha vyama vinne vya kisiasa kisiwani Madagascar kilichokumbwa na mivutano ya kisiasa tangu mwezi Januari mwaka huu.
Akizungumza baada ya kuwasili nchini Msumbiji, Rajoelina amesema kuwa anataka kutafuta muafaka kwa kumaliza mzozo huo, akisema kuwa hayo yatafanyikiwa kwa kufanya kazi pamoja na viongozi watatu wa zamani wa Madagascar.
Zafy aliyeiongoza Madagascar kuanzia mwaka 1993 hadi 1996, amesisitizia umuhimu wa mazungumzo hayo akisema kuwa mzozo huo ni hatari na anatumai mazungumzo hayo yatafanikiwa kwa kupatikana suluhu. Madagascar imekuwa katika mvutano wa kisiasa tangu mwanzoni mwa mwaka huu kutokana na kutoelewana kwa Ravalomanana na Rajoelina, meya wa zamani wa Antananarivo na kiongozi wa upinzani.
Baada ya maandamano yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 100 na Ravalomanana aliondolewa na jeshi lake lililoongoza nchi kabla ya kukabidhi madaraka mara moja kwa Rajoelina, huku kiongozi aliyeondolewa madarakani akiilaumu Ufaransa kuwa na mkono wake katika amatukio hayo, madai ambayo Uafaransa iliyakanusha.
Kawa upande wake Ravalomanana anayeishi uhamishoni Afriaka kusini amekua akiitembelea miji mikuu kadhaa ya nchi za kiafrika kutafuta uungaji mkono , hatua ambayo kwa sehemu ilizaa matunda baada ya umoja wa Afrika kulaani kuondolewa kwake madarakani. Tangu wakati huo, jumuiya ya kimataifa nayo ikaamua kusimamisha baadhi ya misaada yake kwa Madagascar, moja kati ya nchi masikini duniani.
Viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), walimteua Chissano kuwa mpatanishi wa mzozo wa Madagascar, baada ya juhudi za Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa kukwama.

White House Spokesman Changes Tune on Ahmadinejad as "Elected Leader" of Iran

White House Press Secretary Robert Gibbs on Wednesday walked back remarks from a day earlier in which he concluded that Mahmoud Ahmadinejad, the Iranian president sworn in Wednesday for a second term despite allegations of election fraud, is the "elected leader" of the Islamic Republic.
Addressing reporters Tuesday, Gibbs responded to a question about whether the administration recognizes the legitimacy of Ahmadinejad's re-election by saying the debate about Iran's leadership "was ongoing in Iran by Iranians," and that the United States remains committed to the goal of "reaching out in order to ensure that they don't develop a nuclear weapons program."
Asked whether that meant the administration recognizes Ahmadinejad as the legitimate president of Iran, the spokesman replied, "He's the elected leader."
On Wednesday, Gibbs said he wanted to "correct a little bit" of what he said a day ealier.
"I denoted that Mr. Ahmadinejad was the elected leader of Iran. I would say it's not for me to pass judgment on. He's been inaugurated, that's a fact. Whether any election was fair, obviously the Iranian people still have questions about that and we'll let them decide that. But I would simply say he's been inaugurated and we know that is simply a fact," he said.
Despite massive opposition to his return to power and several show trials of hundreds of protest organizers and participants, Ahmadinejad was sworn in for a second term on Wednesday. His inauguration was surrounded by security, including a mile-wide area cordoned off around the Parliament building and 9,000 police, anti-riot and plains-clothed officers.
One woman able to get within earshot of the two-term president was arrested for yelling in support of the opposition candidate Houssein Mir Mousavi.
"Long live Mousavi. Death to the dictator," she shouted.
With security so tight, several others searching for a place to protest headed toward the outdoor bazaar, which instantly shut down upon fear of demonstrations.
Traveling in Kenya on Wednesday, Secretary of State Hillary Clinton urged the Iranian government to "recognize the rights of the people of Iran" and to make democracy "much more than a flawed election as that last one was."
Clinton also addressed Ahmadinejad's return to power by saying the United States doesn't get to choose other countries' leaders.
"For purposes of actions and multilateral organizations like the UN, for other important matters, we don't always get to deal with the government that we want to. It's not our choice, it's the choice of the individual countries as to how they determine their leadership," she said.
Clinton added that the United States still has "engagement" on the table for Tehran, either directly or through a multi-country forum, but has not received any response. She said President Obama intends to re-evaluate Iran's willingness to meet and negotiate this fall, but other considerations are in place.
"On the sanction side there is a great opportunity for the international community to stand up against Iran's nuclear program, and to impose consequences of significance. On the incentives side, we want the Iranians to know, although they are violating international rules and regulations, and though they cannot in our view and the view of majority of the international community become a nuclear weapons power, that under appropriate safeguards, they would be able to have a civil nuclear program," she said.
Asked again whether the United States recognizes Ahmadinejad as the leader of Iran, Gibbs said Wednesday, "It's not for me or for us to denote his legitimacy, except to acknowledge the fact."
He added that he cannot pass judgment on whether the election was fair.
I think that's for the Iranian people to decide, and obviously there are many that still have a lot of questions," he said.