Selasa, 17 November 2009

Askofu wa Kanisa katoliki jimbo la same atimuliwa na Vatican

Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Vatican nchini Italia yamemnyang’anya Jimbo, Askofu wa Same, Jacob Koda, baada ya kubainika kukiuka mafundisho ya imani ya kanisa hilo. Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Joseph Chennoth alithibitisha Dar es Salaam jana kuwa Askofu Koda ametakiwa na kanisa kuacha utume huo mara moja na kupumzika ama kufanya shughuli binafsi za mafunzo.

Hata hivyo, Balozi huyo wa Papa hakufafanua zaidi kiini cha kuondolewa kwa Askofu Koda na ni mafundisho gani ya kanisa aliyokiuka, ingawa taarifa kutoka Same zilizolifikia gazeti hili jana zilidai kuwa amejiingiza katika mafundisho yaliyo kinyume cha imani ya Kikristo na ya Kanisa Katoliki.

Sambamba na kuondolewa Askofu Koda katika jimbo hilo lililoko mkoani Kilimanjaro, pia taarifa ya Askofu Mkuu Chennoth kwa vyombo vya habari jana ilieleza kuwa Baba Mtakatifu Benedicto wa XVI amemteua Padri Rogath Kimaryo kuwa Msimamizi wa Kitume wa jimbo hilo hadi hapo litakapopata askofu mwingine.

Padri Kimaryo kabla ya uteuzi huo alikuwa Paroko wa Parokia ya Kipawa, Jimbo Kuu la Dar es Salaam. “Tumemshauri kuondoka jimboni na Padri Kimaryo ataongoza jimbo hilo kwa muda mpaka hapo Baba Mtakatifu atakapomteua askofu mpya,” alisema Askofu Mkuu Chennoth.

Aidha, taarifa hiyo ya Ubalozi wa Vatican hapa nchini kwa vyombo vya habari iliyotolewa kwa gazeti hili na Katibu Mtendaji wa Habari wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Revocatus Makonge, ilithibitisha uteuzi wa Padri Kimaryo katika jimbo hilo la Same.

“Mwakilishi wa Baba Mtakatifu hapa nchini anayo heshima kutangaza kuwa Baba Mtakatifu Benedicto wa XVI amemteua Padri Rogath Kimaryo (CSSP) ambaye ni Paroko wa Kipawa, Dar es Salaam kuwa Msimamizi wa Kitume mwenye mamlaka kamili na chini ya utii kwa kiti kitakatifu wa Jimbo Katoliki la Same,” ilieleza taarifa hiyo iliyotolewa Mei 30, mwaka huu. Hata hivyo, Padri Makonge alisema TEC haina taarifa zozote za kina kuhusu suala hilo na kueleza kuwa wanachofahamu ni uteuzi wa Padri Kimaryo kupitia taarifa hiyo ya Mwakilishi wa Papa nchini.

Taarifa zaidi kutoka katika ofisi za Ubalozi wa Vatican Dar es Salaam zilieleza kuwa Padri Kimaryo atakabidhiwa jimbo hilo kwa usimamizi rasmi kesho katika Ibada ya Misa itakayoongozwa na Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo katika Kanisa Kuu la Same na kuhudhuriwa na viongozi kadhaa wa kanisa hilo akiwamo Askofu Mkuu Chennoth.

Bila kufafanua zaidi, Askofu Mkuu Chennoth alisema Kanisa Katoliki huwa lina utaratibu wa kumteua Msimamizi wa Jimbo linapotokea hitaji kama hilo hivyo ni kitu cha kawaida ndani ya kanisa pindi panapoonekana umuhimu wa kufanya hivyo.

Askofu Koda aliteuliwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa II kuwa Askofu Mpya wa Same Septemba 1999 kuchukua nafasi ya Askofu Josephat Lebulu aliyehamishiwa katika Jimbo Kuu la Arusha.

Padri Kimaryo ambaye ni Padri wa Shirika la Roho Mtakatifu alitunukiwa Udaktari wa Sheria nchini Roma katika Chuo Kikuu cha Pontifical Gregorian na pia amefanya kazi ya kitume kama mshauri kwa miaka sita katika nyumba yao ya shirika nchini humo.

Kwa utaratibu wa Kanisa Katoliki, Papa humteua Msimamizi wa Jimbo ambaye kikanisa ni kama Mtawala ambaye hufanya kazi hiyo, mara kadhaa hutumikia katika eneo ambalo halijapewa hadhi ya Jimbo au katika Jimbo lisilo na Askofu au tatizo kama lililotokea. Katika sheria za kanisa (Canon Law), utawala wa aina hiyo unampa mamlaka mtawala kufanya kazi zote za kiaskofu isipokuwa kuuza mali yoyote ya jimbo na kutoa daraja la upadrisho.

Si ajabu kuwa Panga la Kikwete likamkumba Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Waziri Mkuu Pinda, panga la Kikwete linamkalia vibaya kutokana na umri wake.

KAMA Rais Jakaya Kikwete atakuwa ametoa kauli thabiti ya kuwaengua wazee iwapo atachaguliwa tena mwaka 2010, basi atawapa kisogo mawaziri wengi wazoefu walio kwenye serikali ya sasa, akiwemo mtendaji wake mkuu, Mizengo Pinda.

Akizungumza katika mkutano wa vijana wa kulea viongozi wa Afrika juzi, Rais Kikwete aliahidi kufanya mabadiliko makubwa kwenye serikali yake ijayo iwapo atashinda uchaguzi wa mwaka 2010, akisema kuwa ataingiza vijana wengi.

Alisema: “Wale viongozi wa rika langu, lazima waanze kuwaachia nafasi vijana. Tunahitaji wakuu wa wilaya vijana zaidi; wakuu wa mikoa vijana zaidi na hata mawaziri vijana zaidi. Ndivyo ilivyotokea kwetu sisi wakati tukiwa vijana.”

Lakini kama atasimamia ahadi yake, Rais Kikwete, ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 59, atalazimika kuachana na Pinda, 61, katika kipindi cha pili cha uongozi wake baada ya serikali ya sasa kuwa mchanganyiko wa wazee waliowahi kushika nyadhifa tangu serikali ya awamu ya kwanza na vijana ambao ndio kwanza wameingia kwenye siasa.

Pinda hakuwa chaguo la kwanza la Kikwete kwa nafasi hiyo ya waziri mkuu wakati aliposhinda kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005.

Lakini mbunge huyo wa Mpanda aliteuliwa na Kikwete mwaka 2008 baada ya Edward Lowassa, ambaye ni rafiki mkubwa wa rais, kujiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu kutokana na kashfa ya utoaji zabuni kwa kampuni ambayo ilibainika kuwa haikuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond Development LLC.

Pinda, ambaye ni muhitimu wa shahada ya Sheria kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam, alikuwa msaidizi wa katibu wa Rais kati ya mwaka 1982 na 1992 na baadaye kuwa karani wa Baraza la Mawaziri kuanzia mwaka 1996 hadi 2000.

Alichaguliwa kuwa mbunge wa Mpanda mwaka 2000 na baadaye kuwa naibu waziri wa Tamisemi na baadaye kuwa waziri kamili mwaka 2006 kabla ya kuteuliwa kuwa waziri mkuu Februari 8, 2008.

Tangu aanze kuwa waziri, Pinda hajawahi kuhusishwa na makundi na wakati wote amekuwa akichukuliwa kama mchapakazi na uteuzi wake ulipitishwa na wabunge 279, huku kura mbili zikimpinga na moja ikiharibika.

Wakati ahadi hiyo ya Kikwete ikionekana kuwa kiashirio kibaya kwa watendaji wake wa sasa, baadhi ya wanasiasa na mawaziri wameiambia Mwananchi kuwa uamuzi huo utachangia maendeleo, huku wengine wakipinga.

Baadhi ambao walihojiwa na Mwananchi kutaka maoni yao walisema ahadi hiyo itasaidia kuisafisha serikali yake kutokana na viongozi kadhaa wenye umri mkubwa wana uzoefu wa kutuhumiwa kwa ufisadi.

“Mambo mengi yameonekana kuwashinda baadhi ya mawaziri wake na kumfanya yeye binafsi kuingilia kati kwa mawazo na hata wakati mwingine kutoa amri,” alisema mmoja wa wabunge wa CCM ambaye hakupenda jina lake litajwe kutokana na nafasi yake ndani ya chama.

Alielezea baadhi ya mawaziri upeo wao umefikia mwisho na kwamba kuendelea kuwaweka kwenye nafasi zao kutawafanya waendeshe mambo kwa mazoea badala ya kwenda na wakati.

“Kwanza ingetakiwa mawaziri na hata wabunge nao wawekewe ukomo. Hii ingesaidia sana... na tusingewasikia waking’ang’ania majimbo kama mbwa anavyong’ang’ania mfupa. Imefika mahali ukionekana unataka kugombea jimbo fulani ndani ya CCM, unaonekana kama mtovu wa nidhamu,” alilalamika.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (Itikadi na Uenezi), John Chiligati alionyesha kuwa na mawazo tofauti kidogo, akieleza alichosema rais ni utekelezaji wa sera za chama hicho.

Alisema ni katika utekelezaji huo kanuni zinaelekeza wazee kupisha vijana katika nafasi mbalimbali za uongozi.

“Hii ni kanuni ya maisha na ndio sera ya CCM. Kama umri umeenda lazima tupishe tu,” alisema Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi.

“CCM imetenga nafasi maalumu kwa vijana kuingia Halmashauri Kuu ya chama na hata katika nafasi za ubunge... ukiachia wabunge wa majimbo, tumetenga nafasi 10 maalumu kwa ajili ya vijana,” aliongeza Chiligati ambaye ana umri wa miaka 59.

Chiligati, ambaye ni mbunge wa Manyoni Mashariki (CCM), alisema: “Sisi tunajiandaa kwenda kupumzika, tunataka vijana wapate nafasi hata kama wazee watakuwamo, lazima vijana waonekane kwa wingi”.

Alisema hiyo ni kwa sababu busara ya wazee katika uongozi ni muhimu sana katika kuhakikisha kwamba taifa linaongozwa vizuri kwa kuwa na maamuzi ya busara na hekima ya hali ya juu.

Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa CCM na mbunge wa Newala, George Mkuchika, 61, aliunga mkono mtazamo wa Rais Kikwete akisema “hiyo ni sawasawa kabisa”.

Mkuchika alisema huo ndio utaratibu walionao CCM na hata katika utamaduni wa jamii ya Tanzania.

“Sio tu kwa Baraza la Mawaziri, bali hata katika nafasi zote za uongozi serikalini na katika chama chetu,” alisema Mkuchika.

“Mawaziri, manaibu, makatibu wakuu na wakurugenzi wa wizara mbalimbali wanazeeka, hivyo lazima vijana washike nafasi hizo kwa maslahi ya maendeleo ya taifa, kwa sababu wao ndio chachu ya maendeleo.”

Alisisitiza kuwa aliyosema rais Kikwete ni sawasawa kabisa, lakini ni kwa vijana ambao wameandaliwa na kupikwa vizuri, ili kupata uzoefu wa kuongoza katika nyadhifa mbalimbali za kitaifa.

“Unajua kuna msemo usemao ‘uzee dawa’ hivyo pamoja na kwamba vijana watakuwa wengi, wazee wachache watakuwamo ili kutoa busara na miongozo yao katika kutoa maamuzi,” alisema Mkuchika.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, ambaye ni waziri kijana zaidi kwenye serikali ya awamu ya nne, aliunga mkono kauli ya rais akisema: “Haya ni mambo ambayo nimekuwa nikiyasema mara nyingi. Vijana wana nafasi na changamoto nyingi za maendeleo katika taifa.”

Mbunge huyo alimsifu Rais Kikwete akisema kwamba hata katika uongozi wake wa sasa amejitahidi kuweka vijana kadhaa kwenye serikali yake.

Hata hivyo, baadhi ya mawaziri ambao waliomba majina yao yasitajwe gazetini, walisema wapo tayari kuwaachia vijana madaraka bila ya wasiwasi wowote.

Mara baada ya Kikwete kushinda kiti cha urais mwaka 2005 aliteua baadhi ya mawaziri ambao walitumikia serikali za awamu zilizomtangulia, wakiwemo Bakari Mwapachu, Basil Mramba, Joseph Mungai na Kingunge Ngombare Mwiru ambaye hata hivyo alimteua kuwa mbunge. Hata hivyo, baada ya kuvunja Baraza la Mawaziri Kikwete hakuwarejesha tena.

‘Zanzibar undeni Serikali ya Mseto’

ZANZIBAR imeshauriwa kuunda Serikali ya Mseto ikilazimika kufanya hivyo, kwa sababu si jambo la aibu, bali ni sehemu ya demokrasia.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Balozi Juma Mwapachu, alisema jana kuwa watu hawatajisikia vibaya kuhusu uundaji wa Serikali ya Mseto kutokana na kuwa sehemu ya kuundwa kwa demokrasia ya kweli.

“Nafikiri rafiki zetu wa Zanzibar wakifikiria kuwa na Serikali ya Umoja si mbaya,” alisema Balozi Mwapachu na kuongeza: “Ingawa wanasiasa wengi katika nchi za Afrika Mashariki hupendelea serikali inayoendeshwa na chama kimoja.”

Alizungumza hayo baada ya kufungua mkutano wa demokrasia katika nchi za Afrika Mashariki ulioandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 10 tangu kuundwa kwa EAC Novemba 1999.

Alisema Serikali ya Mseto imefanikiwa katika nchi nyingine kama za Ujerumani na Italia, huku akiunga mkono makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), akisema ni mwanzo mzuri wa upatikanaji wa amani Zanzibar.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandala, alisema sababu ya watu wachache kujitokeza katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliopita inatokana na wananchi kuamini kuwa viongozi wanaochaguliwa hawaleti tofauti yoyote.

Alisema ni jambo la kawaida duniani uchaguzi unapofanyika kama wa mitaa, unakuwa na matokeo duni mpaka Uchaguzi Mkuu ambao wananchi wanaamini kuwa kura zao zinaweza kuleta mabadiliko.

Profesa Mukandala alishauri katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu ufanyike kwa wakati mmoja ili kuhamasisha wananchi wengi kujitokeza kupiga kura katika kuchagua viongozi wa mitaa.

Kutokana na maombi ya wadau wengi, THE THOMCOM Inc. imeweza kupata picha mbalimbali za marehemu dada Emmy.

Dada Emmy akiwa na Juvenile Mwambi,

Dada emmy katikati akiwa na marafiki zake. kushoto ni dada Gladis raia wa Kenya

Dada Emmy akiwa na Edd Mkali. katikati ni mtoto wa Mr. Edd Mkali


Dada Emmy akitoa hotuba siku ya kuzaliwa kwake iliyofanyika katika kumbi za Ubalozi wa Tanzania Moscow Russia mwaka huu.




Picha mbalimbali za Dada Emmy akiwa katika mapozi mbalimbali


Picha mbalimbali za Dada Emmy akiwa katika mapozi mbalimbali


Picha mbalimbali za Dada Emmy akiwa katika mapozi mbalimbali

Ijue nchi yako ni ya ngapi kwa umasikini duniani? ukimwi n.k.


Tanzania

Facts and Figures

IOM Member since November 1998
Capital: Dodoma (official), Dar es Salaam (commercial)
Population: 38,478,000
Total Area: 945,087 sq km
Major Languages: English, Swahili
Currency: Tanzanian Shilling (TZS)
GDP per Capita PPP: USD 674
HDI Rank: 162 of 177 (HDI value, 0.430)
HPI Rank: 64 of 102 (HPI value, 36.3%)
Remittances: USD 16 million
Net Migration Rate: -1.9 migrants/1,000 population
International Migrants: 2.1%
Women as a Percentage of International Migrants: 52.3%
Population under 15: 44.4%
Adult HIV Prevalence: 6.5%

definition

Tanzania - Sources and Definitions for Country Facts and Figures

Capital, Total Area, Languages and Currency based on data from the BBC News Country Profiles. Tanzania is the largest country in east Africa with a total area of 945,000 sq km, out which 2000 sq km is Zanzibar, 881,000 sq km Mainland, 62,000 sq km water, and 3.35 sq km forest and woodlands. Data from the Tanzania National Website,accessed on 17 May 2007.

Population, 2005, based on data from the United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division's World Population Prospects: the 2006 Revision Population Database. The National Bureau of Statistics Tanzania estimates the population for 2005 at 37,379,000. Data from the National Bureau of Statistics Tanzania Official Website, accessed on 17 May 2007.

Gross Domestic Product (Purchasing Power Parity). The sum value of all final goods and services produced in a country in a given year valued at prices prevailing in the United States of America. GDP Per Capita (PPP), 2004, is Gross Domestic Product on a Purchasing Power Parity basis divided by the population. GDP Per Capita PPP based on data from the United Nations Development Programme's Human Development Report 2006

International Migrants as a Percentage of the Population, 2005. Estimated number of international migrants divided by the total population, expressed as a percentage. The number of international migrants generally represents the number of persons born in a country other than that in which they live. Data from the United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division's World Migrant Stock: The 2005 Revision Population Database.

Additional Resources
International Migration Law Database
National Instruments: Tanzania



Female Migrants as a Percentage of All International Migrants, 2005. The percentage of female migrants among all international migrants. Data from the United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division's World Migrant Stock: The 2005 Revision Population Database.

Percentage of Population Under 15, 2005, refers to the percentage of persons below 15 years old with respect to the total population. Data from the United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division's World Population Prospects: the 2006 Revision Population Database.

Adult HIV Prevalence, 2005, refers to the percentage of adults aged 15 to 49 years old infected with the HIV virus. It is calculated by dividing the number of adults aged 15 to 49 years who have HIV in a given year by the population of adults of the same age group. Data from the UNAIDS Report on the Global AIDS Epidemic 2006.

Human Development Index (HDI). A composite indicator that measures development and human progress based on health, education, and purchasing power. The higher the HDI rank, the higher a country's level of development. HDI Rank, 2004, based on data from the United Nations Development Programme's Human Development Report 2006.

Human Poverty Index for Developing Countries (HPI-1) is a composite indicator that measures deprivations in the three basic dimensions captured in the human development index - a long and healthy life, knowledge and a decent standard of living - and focuses on the proportion of people below a threshold level. The higher the HPI-1 rank, the lower the level of poverty. HPI-1 Rank, 2004, based on data from the United Nations Development Programme's Human Development Report 2006.

Workers' remittances and compensation of employees received (USD), 2004, comprises current transfers by migrant workers and wages and salaries earned by nonresident workers. Data from the World Bank's World Development Indicators database, April 2006.

Net Migration Rate, 2000-2005. The difference between the number of persons entering and leaving a country during the year per 1,000 persons. An excess of persons entering the country is referred to as net immigration (e.g., 3.56 migrants/1,000 population); an excess of persons leaving the country is referred to as net emigration (e.g., -9.26 migrants/1,000 population). Net Migration Rate based on data from the United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division's World Migrant Stock: The 2005 Revision Population Database.


Serikali zikipenda, ubaguzi wa rangi unatokomea kabisa


Leader of Russian anti-fascist skinheads killed in Moscow

Ivan Khutorskoy, one of the leaders of the Russian left-wing skinhead movement was shot dead in Moscow on Monday evening. The victim’s friends and relatives see political motives behind the murder.

Russian daily Komsomolskaya Pravda reports that 26-year-old Khutorskoi was killed with two pistol shots in the back of the head in the stairwell of the apartment building where he lived.

According to several Russian leftist skinhead websites, Ivan Khutorskoy was one of the leaders of the movement in Russia. His activities included providing security at concerts and organizing mixed fights among young leftists and anarchists. Khutorskoy survived three attempts on his life over the past four years. In 2005, several attackers slashed his head with a razor. Later he was repeatedly stabbed in the neck with a screwdriver and beaten with a baseball bat, and he was stabbed in the stomach with a knife in January this year.

The “Collective Action” website wrote on Tuesday that all Khutorskoy’s friends and comrades blamed the murder on Russian neo-Nazi groups.

The website also reminded that this was the sixth time an anti-fascist activist has been killed in Moscow over the past 5 years. Police have solved one such case, after which several activists of right-wing skinhead groups were sentenced to prison terms.

“Al Qaeda iliundwa na CIA...





“Al Qaeda is a kind of CIA Arab legion created during the Soviet presence in Afghanistan,” believes author Webster Tarpley

Iranian President Mahmoud Ahmadinejad has accused the West of being behind the bombings which killed leaders of the Revolutionary Guard. Many people say the allegations are shocking.

The group that claimed responsibility for the attacks is a Sunni separatist group called Jundallah, or Soldiers of God. Reports say they have links to Al Qaeda. How in the world could the US be linked to them? Tarpley doesn’t regard it confusing.

“Al Qaeda itself is a kind of CIA Arab legion created during the Soviet presence in Afghanistan,” he said. “It is an open secret to any regional expert: the Jundallah is controlled and funded by the US and the British.”

Skinhead gang sentenced in Moscow




The Moscow City Court has handed sentences to ten skinheads, found guilty of attacking people of non-Slavic origin. At the time crimes were committed most of the accused were underage.

Seven of the 11 members of the gang were found guilty of three attacks on citizens of Kyrgyzstan, Uzbekistan and China – all in the period between February 12 and March 7, 2008. During the attacks, gang members brutally beat the victims.

While attacking the Kyrgyz citizen, the mastermind behind the gang, Ilya Shutko, 19, stabbed him eight times. This resulted in victim’s death in hospital. Shutko has already been convicted of the murder in a separate case and sentenced to seven and a half years in prison.

Shutko received 10 years in a a standard regime penal colony, as the judge had taken into consideration his earlier sentence. The other gang leader Evgenia Zhikhareva received eight years in a juvenile correction centre .

Ruslan Pertz, Oleg Levshin and Oleg Sinodov have received 38 months, 42 months and 48 months suspended sentences respectively, with five years’ probation. This means they can’t change their residence or school without prior notification of authorities. Sergey Gordeev will spend the next five years in a juvenile correction centre.

Yury Matyukhov was sentenced to 7.5 years in a standard regime penal colony, with 8.5-year sentences handed to Pavel Sokolov and Marat Zhuchkov. The toughest sentence – 10 years in a maximum security prison – was handed to Aleksandr Efimov.

The sentences can be appealed in the Supreme Court within 10 days. Meanwhile, prosecutors said the punishment that the accused received is lighter than it should be.

“We insisted all the accused receive a custodial sentence. Because of the nature of the crimes they committed, they are dangers to society,” said prosecutor Galina Karpova.“But because of their young age, the court decided to hand down a lighter punishment.”

Two members of the gang did not appear in court today, as they are awaiting new charges – including terrorism – to be pressed against them

THE THOMCOM Inc. INAOMBA KWA YEYOTE MWENYE PICHA ZAIDI ZA MAREHEMU DADA EMMY AZITUME

KUTOKANA NA WADAU WENGI KUOMBA KUONA PICHA ZINAZOMUONESHA MAREHEMU VIZURI, THE THOMCOM Inc INAOMBA KWA YEYOTE MWENYE PICHA NZURI ZA MAREHEMU AZITUME KWA BARUA PEPE boni_russia@yahoo.com aksanteni sana. R.I.P

China na Marekani zatofautiana kuhusu Israel

zakubaliana kuhusu mambo kadhaa

Bado lakini viongozi hao wanatofautiana juu ya suala la haki za binadamu miongoni mwa mengine

Rais wa Marekani Barack Obama na mwenyeji wake rais wa China Hu Jintao wamekubaliana juu ya kuimarisha uhusiano wao zaidi katika suala masuala ya uchumi,mabadiliko ya hali ya hewa,nishati na vitisho vya kinuklia kutoka nchi za Iran na Korea Kaskazini. Hata hivyo viongozi hao wawili wameonekana bado wanatofautina katika masuala ya uchumi,usalama na haki za binadamu,masuala ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakiutatiza uhusiano wa mataifa hayo mawili yenye nguvu. Obama ni rais wa kwanza wa Marekani kuitembelea China katika kipindi cha miaka 12.

Viongozi hao wawili wameafikiana juu ya kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili na kutilia mkazo katika masuala ya uchumi,mabadiliko ya hali ya hewa nishati na Nuklia. Lakini kutokana na mazungumzo yao imedhihirika kwamba pande hizo mbili bado zinatofautiana jambo ambalo limeonyesha kwamba itakuwa vigumu kwa ziara hiyo ya kwanza ya rais Obama nchini China kumaliza mvutano na taifa hilo.Rais Obama amesema kwamba serikali ya mjini Tehran itachukuliwa hatua zinazostahili ikiwa haitothibitisha kwamba mpango wake wa kinuklia ni kwa ajili ya matumizi ya amani na kuwa wazi kuhusu mpango huo.Obama amesema Marekani na China zitashirikiana kukikabili kitisho cha Iran ikiwa itamiliki silaha za kinuklia.Pia amesema baraza la usalama la Umoja wa mataifa linazungumza kwa kauli moja dhidi ya mpango huo wa Iran.

Kwa upande wake rais Hu Jintao wa China amezungumzia zaidi juu ya diplomasia katika suala hilo la Iran ili kuimarisha usalama katika eneo la mashariki ya kati. Kuhusu Korea Kaskazini nchi zote mbili zinataka mazungumzo ya pande sita yaanze haraka iwezekanavyo.Akizungumzia hilo rais wa China alisema-

''Tumeafikiana kwa pamoja kubakia katika lengo la kuutatua mzozo wa nuklia wa Korea kaszini kupitia mazungumzo,na hatua hiyo itatuwezesha sote tunaohusika katika suala hilo kufikia lengo letu.Pande zote mbili zitafanya kazi pamoja na wahusika wengine kuendelea na mpango wa kuishawishi Korea kaskazini kuchana na harakati zake na kurudi kwenye mazungumzo ya pande sita ili kuimarisha amani na usalama katika eneo la kaskazini mashariki mwa Asia''

mkutano wa rais Obama Chinamkutano wa rais Obama Chinalengo la pande hizo mbili katika mkutano wa Copenhagen sio kupata makubaliano ya kupendelea upande fulani au azimio la kisiasa bali wana nia ya kufikia makubaliano yatakayojumuisha masuala yote na ambayo yatatekelezwa.Akaongeza kusema kwamba-

''Nchi zetu kama watumiaji wakubwa na watoaji wa nishati hakuwezi kupatikana suluhisho katika changamoto hii bila ya juhudi zetu na ndio sababu tumekubaliana juu ya mipango kadhaa ikiwa ni pamoja na kuunda kituo cha utafiti wa nishati na kuafikiana kuhusu matumizi ya nishati isiyoharibu mazingira na pia kushirikiana kufikia mafanikio katika mkutano wa Copenhagen''

Ama kuhusu suala la Uchumi rais Obama ameitaka China kushirikiana na Marekani katika kuuongoza ulimwengu kujikwamua kutokana na mgogoro wa kiuchumi unaoendelea lakini juu ya hilo pia wamekubaliana kufuatilia ahadi zilizotolewa katika mkutano wa G20 mjini Pittsburg na kutafuta mkakati wa kuimarisha uchumi.

Hata hivyo rais wa China ameitaka Marekani kuacha mtindo wa kujipendelea katika kulinda nafasi zake za kazi, pamoja na kukataa kuitambua China kama soko kamili la kiuchumi na kudhibiti biashara ya technologia ya juu.

''Nimemsisitizia rais Obama kwamba katika hali ya hivi sasa ya kiuchumi nchi zateu zinabidi kupinga kwa dhati mtindo wa kulinda nafasi za kazi katika maeneo yote''

Na hatimae katika suala la haki za binadamu rais Obama alionekana kuchokoza nyuki aliposema kwamba makundi ya waliowachache nchini China wanabidi kupewa haki za binadamu na kuitolea mwito nchi hiyo kurudi katika meza ya mazungumzo na wajumbe wa kiongozi wa kidini wa Tibet Dalai Lama anayeishi uhamishoni. Matamshi hayo yalijibiwa kwa sauti kali na rais Hu Jintao akisema pande zote mbili zimehakikishiana juu ya msingi wa kuheshimiana na kuheshimu uhuru wa mamlaka ya kila upande Kutokana na hilo China itaendelea kuchukua hatua ya kudumisha usawa,kuheshimiana,na kutoingilia kati masuala ya ndani ya upande wa pili.

Kikwete ajiandaa kupangua safu yake ya uongozi. hata hivyo amechelewa sana

Kukumba pia wakuu wa mikoa na wilaya
Ni njia ya kutoa fursa vijana mwakani
Wenye umri kama wake watakiwa wapishe
Rais Jakaya Kikwete.

Rais Jakaya Kikwete ameahidi kuwa kama akijaliwa kupata kipindi cha pili cha kuiongoza Tanzania, atafanya jitihada kubwa kuubadilisha uongozi kuwa wa vijana.

Akizungumza na vijana kutoka nchi kadhaa za Afrika juzi jijini Dar es Salaam, Rais Kikwete pia alisema vijana ndiyo Tanzania ya kesho, na kama nchi haitawekeza vya kutosha kwa vijana na maendeleo yao, basi itakuwa haiwekezi katika hali yake ya baadaye.

Katika mkutano huo wa Mpango wa Kulea Uongozi wa Afrika ambao unadhaminiwa na Askofu Mkuu mstaafu wa Kanisa Anglikana wa Afrika Kusini, Desmond Tutu, Rais Kikwete alisema anauthamini mpango huo na kusisitiza kwamba kadri miaka inavyokwenda ni lazima rika la wazee lipishe lile la vijana.

“Kwenye uchaguzi mkuu ujao kama nitajaliwa na nikapata bahati ya kuchaguliwa tena, nitahakikisha kuwa naubadilisha uongozi wa Tanzania kwa kuufanya uongozi wa vijana zaidi," alisema.

Aliongeza: “Wale viongozi wa rika langu, lazima waanze kuwaachia nafasi vijana. Tunahitaji wakuu wa wilaya vijana zaidi, wakuu wa mikoa vijana zaidi, na hata mawaziri vijana zaidi. Ndivyo ilivyotokea kwetu sisi wakati tukiwa vijana.”

“Vijana ndiyo matumaini ya nchi hii katika miaka ijayo na kama hatukuwekeza kwa vijana wetu, basi ni dhahiri kuwa hatuwekezi ipasavyo katika miaka ijayo ya taifa letu,” alisisitiza.

Baraza la Mawaziri la sasa la Rais Kikwete lina jumla ya mawaziri na manaibu mawaziri 51.

Katika baraza hilo, mawaziri wenye umri kuanzia miaka 60 na kuendelea ni 14 wakati wenye umri kati ya miaka 50 hadi 59 ni 25. Mawaziri na manaibu mawaziri wenye umri chini ya miaka 50 ni 12.

Waziri mwenye umri mkubwa kuliko wote ana miaka 67 akifutiwa na mwenye umri wa miaka 66.

Akijibu maswali ya vijana hao kutoka nchi mbalimbali za Afrika zikiwamo Tanzania, Nigeria, Kenya, Afrika Kusini na Uganda, Rais Kikwete aliwaeleza vijana hao jinsi gani alivyojikuta anaingia katika siasa.

Akijibu swali kuhusu maendeleo ya karibuni katika siasa za Zanzibar, Rais Kikwete alisema ni jambo la kufurahisha kwamba vyama vya siasa Zanzibar vimeamua kuachana na siasa na mazoea ya zamani na kuanza ukurasa mpya.

“Nawatakia heri sana katika mwelekeo mpya na sahihi kabisa katika uendeshaji wa siasa. Ni mwelekeo ambao sote tumekuwa tunautafuta kwa muda mrefu,” alisema.

Katika siku za karibuni, Chama cha Wananchi (CUF) kimeamua kumtabua Rais Amani Abeid Karume kama Rais halali wa Zanzibar, hatua ambayo imefungua kila aina ya uwezekano wa kupatikana maelewano na mwafaka Tanzania Visiwani.

Senin, 16 November 2009

Dada Emmy ametutoka, Mungu Ametoa na Yeye ametwaa, Jina la Bwana Lihimidiwe...



Habari zilizoifikia THE THOMCOM Inc. zinasema kuwa Dada Emiliana M. Mwidunda ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa nne (4) ambaye alitarajia kuwa daktari wa upasuaji ameaga dunia asubuhi ya leo jumatatu tarehe 16.11.2009. Familia ya Dada Emiliana M. Mwidunda na wanafunzi watanzania wanaosoma Chuo Kikuu Cha Urafiki Moscow Russia wako kwenye majonzi makubwa baada ya kuondokewa kwa mpendwa huyo. THE THOMCOM Inc. inapenda kuchukua nafasi hii kupeleka salamu za rambirambi kwa familia ya Dada Emmy, ndugu, jamaa na marafiki na kwa watanzania wote waishio moscow katika wakati huu mgumu wa kimaisha. Mungu ametoa na Mungu ametwaa. Jina la Mungu lihimidiwe






Picha mbalimbali akiwemo Dada Emmy. mojawapo ni maeneo ya kanisa moja lililoko Moscow Russia, picha iliyopigwa mara baada ya Ibada ya Misa. Picha hii ilipigwa mwaka 2006..

Minggu, 15 November 2009

Walokole wazidiwa na Mganga wa Kienyeji

Eneo la Kinyerezi, Tabata jijini Dar es Salaam, Novemba 12 mwaka huu lilikumbwa na tukio la aina yake kufuatia vita kubwa kuzuka kati ya baadhi ya watu wanaojiita walokole kutoka Kanisa la International Pentecoste Hollyness Church Ebenezer na watu wanaojihusisha na nguvu za giza ‘wachawi’ kupambana uso kwa uso mtaani mchana kweupe.

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa, walishuhudia vitu vya ajabu vikiruka angani huku nyoka waubwa na wadogo wakitoka katika nyumba ya kijana mmoja aitwaye Kafumu Moto ambaye inadaiwa ni mganga wa jadi tishio katika eneo hilo.
Walisema, tukio hilo lilianza majira ya mchana wakati kundi la walokole zaidi ya 18 likiongozwa na mhubiri maarufu katika eneo hilo aliyetajwa kwa jina moja la Kefa ambaye amepachikwa jina la Jesus, waliposambaa mtaani na kuanza kupiga injili ambayo ililenga kuangamiza uchawi, mapepo na kuleta wokovu katika eneo hilo.

Mashuhuda hao walisema kuwa, pitapita hizo za walokole, ziliishia katika nyumba ya Kafumu Moto ambapo walianza kupiga neno la mungu kisawasawa kitendo kilichomkera mganga huyo kijana na kumfanya naye kuingia ndani na kuvaa magwanda yake ya kazi ya kichawi, kisha kuchukua silaha zake za uchawi wakiwemo nyoka wakubwa na wadogo kisha kutoka nje akiwa na wapambe wake na kuanza kushambuliana na walokole hao.

Inadaiwa kuwa, Kafumu Moto aliamrisha majoka yake kuwashambulia walokole, ambao walitimua mbio na kutawanyika mtaani, huku baadhi yao wakienda kuweka kambi katika kilima kimoja porini kuendelea na maombi yao kwa sauti ya juu.

Mtandao huu ulifika eneo la tukio na kukuta mtafutano kati ya walokole na kundi la mganga huyo ukiendelea vichakani, huku watu wengine wakitimua mbio kuponya nafsi zao .

Hatimaye wahubiri watatu wakiongozwa na Kefa walikutana uso kwa uso na Kafumu ambaye alikuwa amevirigwa na nyoka mdogo shingoni huku akiwa amesheheni silaha zake ambazo ilidaiwa ni tunguli na hirizi.

Walokole walikuwa wakikemea kwa nguvu huku Mganga Kafumu naye akikemea kwa kutaja mizimu yake akiiomba iwaangamize kabisa walokole wale ambao yeye aliwaita ni wachawi wanaotumia neno la Mungu kumuangamiza.

Katika hali ya kushangaza mlokole mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Lazaro Daniel alianza kufuka moshi mkubwa ulioanzia kwenye mifuko yake ya suruali ambapo alianza kupiga kelele na kuvua suruali hiyo kisha kubakia na nguo yake ya ndani.

Baada ya Kefa kuona mwenzake akiwaka, alitimua mbio akifuatiwa na Daniel ambaye alikuwa na ‘kufuli’ aina ya Boxer huku akiomba msaada kwa watu ambao nao walianza kukimbia kuokoa nafasi zao.

Waandishi wetu walifanya jitihada za kuongea na Daniel ambaye alisitiriwa kwa kufungwa shati kwa chini, ambapo alikiri suruali yake kushika moto kimiujiza na kueleza kwamba huenda Kafumu alimwekea kiberiti.

TUKIO LENYEWE LILIKUWA HIVI.
MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Kefa (kushoto) akiwa na Daniel juu ya kilima wakipiga injili

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Mganga wa jadi Kafumu Moto akiwasili eneo la maombi kilimani.

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Mganga Kafumu Moto akimwekea hirizi Daniel mfukoni.

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Baada ya kuweka hirizi mfukoni kwa Daniel Mganga aliomba aombewe ili aokoke ikiwa ni hatua ya kupima uwezo wa wahubiri hao ambao walihisiwa kuwa ‘Feki’.

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Ghafla Suruali ya Daniel ikaanza kuungua

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Danieli akiwa amepagawa ilibidi avue suruali yake, wakati huo mganga alikuwa akiendelea kumuombea dua ya mashetani ili azidi kukolea moto. Kushoto anayeonekana ni Mhubiri Kefa a.k.a Jesus akitimua mbio baada ya mwenzake kuanza kuwaka moto.
MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Baada ya wahubiri kutimua mbio , kilima kitakatifu cha maombi kikatekwa na kigagula Kafumu Moto.

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Danieli (katikati) akiwa amejisitiri kwa kujifunga shati la mhubiri Kefa baada ya ‘kutoka nduki’. Kulia ni raia mmoja akiwa amekaa juu ya tofali mkao wa kujihami.

MGANGA WA JADI AWAZULIA TIMBWILI WALOKOLE
Kafumu Moto akiendelea kuchimba biti mtaani

MGANGA HUYO AKITOA MAELEZO BAADA YA KUMALIZIKA KWA MCHAKATO HUO (bofya hapa)


WALOKOLE WAKITOA MAELEZO YAO BAADA YA MCHAKATO HUO (bofya hapa)


PICHA:CHRISTOPHER LISSA NA ISMAIL MANG’OLA

Ukiwa Kiongozi Bwana, unaweza ukaitwa mtaaluma wa sayansi na technolojia hata kama hujui 1+1=2.

Je kama desturi ya Ulimwengu ukipewa Uprofesa wa Heshima utaenda Chuo Kikuu Kufundisha?

Image
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, Dkt. Salim Ahmed Salim, akimtunuku Shahada ya Heshima ya Uzamifu, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Amani Abeid Karume wakati wa Sherehe ya Mahafali ya saba ya Chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Yusuf Badi).

Sabtu, 14 November 2009

"Russian food and energy will save the world"

chicken fajita food photobeefburger food photored cabbage food photochunky chips food photored cherries food photocoffee bean food photofresh garlic food photostrawberry pancakes food photo

William Wilson, an economist from the Vanguard investment firm in London, told RT about Russia’s impact on the global economy.

Russia's resurgence on the world stage depends on modernizing its economy and freeing up trade. That's the main thrust behind two recent speeches by President Dmitry Medvedev, first in his "State of the Nation" address and again today at the Asia-Pacific Summit

“The world will be facing food shortages, potentially oil and gas shortages, and Russia has a pivotal role there,” Wilson said. “I think the agriculture, the food component, is critically important. Because with the warming of the country and climate change, I expect that Russia will become a major food exporter. Knowledge based, energy and food exporting Russia will play a bigger role in 10 years than it does today.”