Sabtu, 30 Mei 2009

mashindano ya 13 ya kombe la africa chuo kikuu cha urafiki lumumba moscow russia. mbabe ni Gabon...












Kijana mwenye asili ya Iraq amegundua kanuni ya hesabu kuchukua nafasi ya Bernoulli equation

Iraq-born teen cracks maths puzzle

STOCKHOLM (AFP) – A 16-year-old Iraqi immigrant living in Sweden has cracked a maths puzzle that has stumped experts for more than 300 years, Swedish media reported on Thursday.

In just four months, Mohamed Altoumaimi has found a formula to explain and simplify the so-called Bernoulli numbers, a sequence of calculations named after the 17th century Swiss mathematician Jacob Bernoulli, the Dagens Nyheter daily said.

Altoumaimi, who came to Sweden six years ago, said teachers at his high school in Falun, central Sweden were not convinced about his work at first.

"When I first showed it to my teachers, none of them thought the formula I had written down really worked," Altoumaimi told the Falu Kuriren newspaper.

He then got in touch with professors at Uppsala University, one of Sweden's top institutions, to ask them to check his work.

After going through his notebooks, the professors found his work was indeed correct and offered him a place in Uppsala.

But for now, Altoumaimi is focusing on his school studies and plans to take summer classes in advanced mathematics and physics this year.

"I wanted to be a researcher in physics or mathematics; I really like those subjects. But I have to improve in English and social sciences," he told the Falu Kuriren.

What happened to Mau U?

Barcelona bingwa mpya barani Ulaya

Mabingwa wapya wa soka barani Ulaya
Barcelona mabingwa wa soka Ulaya
Jaribio la Manchester United kuweka historia ya kuwa klabu ya kwanza kutetea ubingwa wake wa Ulaya, lilikwama baada ya kuchapwa katika uwanja wa Stadio Olimpico, Rome.

Matumaini ya kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson kurudia kile alichofanya dhidi ya Chelsea mwaka jana yaliyeyuka walipofungwa na Barcelona mabao 2-0 huku mshambuliaji wa Argentinas Lionel Messi akisumbua ngome ya Manchester United.

United ilianza pambano hilo kwa kishindo kikubwa, huku dalili zikionekana za kutetea ubingwa wao, huku Cristiano Ronaldo akiisumbua ngome ya Barcelona na kuwafanya Barcelona kubabaika.

Lakini mara tu baada ya Samuel Eto'o kufunga bao la kwanza katika dakika ya 10 kipindi cha kwanza, kwa kumponyoka Nemanja Vidic, hali ya mchezo ikabadilika na Barcelona wakawa wanamiliki mchezo na kufuta matumaini ya Manchester United kuongeza kikombe kingine zaidi ya kile cha Ligi Kuu ya England.

Barcelona walionekana kumiliki kila idara na hasa sehemu ya katikati ambapo Andres Iniesta na Xavi wakitawa.

Ilikuwa ni Barcelona tena walioweza kupachika bao la pili kupitia kwa Lionel Messi kwa kichwa baada ya kuwekewa mpira wa juu na Xavi, katika dakika ya 25 ya kipindi cha pili.

Kwa ushindi huo sasa Barcelona wamejiongezea kikombe cha tatu msimu huu baada ya kushinda ligi ya Uhispania- La Liga pamoja na kombe la Hispania.

Obama avalia njuga uhalifu wa internet

Obama avalia njuga uhalifu wa internet

Rais Obama ametangaza vita dhidi ya uhalifu wa mtandao
Uhalifu wa mtandao wa internet umeigharimu Marekani dola milioni 8
Rais wa Marekani Barack Obama ametangaza mipango ya kukabiliana na uhalifu wa mtandao wa internet nchini Marekani.

Amesema kutoka sasa , mfumo wa kompiuta wa Marekani utathaminiwa kama chombo muhimu cha serikali.

Ametangaza kuundwa kwa ofisi ya Ikulu ya White house itakayohakikisha usalama wa internet , na akasema atateua mtu atakayeshughulika na visa vya uhalifu katika internet.

Serikali ya Marekani pamoja na taasisi za kijeshi zimeripoti kuingiliwa mara kadha na wahalifu wa internet katika miaka ya hivi karibuni.

Bwana Obama amesema kundi la al Qaeda na makundi mengine yanatatiza makabiliano dhidi ya uhalifu wa mtandao.

Amesema Marekani inategemea sana mifumo ya kompiuta na kwa hivyo uhalifu wa mtandao wa internet ni tishio kubwa nchi yake.

Katika mwaka 2007 pekee , makao makuu ya kijeshi ya Pentagon yaliripoti visa 44,000 vya kile kilichoelezewa kuwa uhalifu wa mtandao uliotekelezwa na wanajeshi wa kigeni , mashirika ya kijasusi na watu binafsi.

Ameeleza kwamba kulingana na utafiti , uhalifu wa mtandao umeigharimu Marekani zaidi ya dola bilioni 8 katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

Amesema ufanisi wa kiuchumi wa Marekani katika karne ya 21 utategemea usalama wa shughuli za mtandao wa internet.

Bomu lingine lalipuka Mbagala, lajeruhi wanajeshi saba

HALI ya usalama kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi (JWTZ), Mbagala Kuu jijini Dar es salaam na maeneo ya jirani, bado haijawa shwari baada ya bomu moja kulipuka jana na kujeruhi wanajeshi saba, mmoja kati yao akiwa mahututi.

Habari kutoka maeneo jirani na kambi hiyo ya Kikosi cha 673 zinasema mabomu yamekuwa yakilipuka mara kwa mara kati ya saa 7:00 usiku na saa 9:00 alfajiri, ingawa la jana lilipuka majira ya saa 4:00 asubuhi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kutoka ndani ya kambi hiyo na kuifikia Mwananchi zinadai kuwa bomu hilo lilijeruhi wanajeshi saba waliokuwa jirani na eneo la bomu kwenye kambi hiyo ambayo ilikumbwa na milipuko ya mabomu Aprili 29.

Habari zinasema wakati bomu hilo linalipuka, askari hao hawakuwa na taarifa yoyote.

"Ni kweli kuna bomu lililolipuka leo saa 4:00 asubuhi hapa kambini na kujeruhi wenzetu saba, mmoja kati yao yuko mahututi," alisema mwanajeshi mmoja aliyeomba jina lake lisitajwe.

"Hata sisi hali hii inazidi kutupa wasiwasi, kwa sababu hatufahamu maeneo sahihi ambayo mabomu yapo."

Kauli yake inalingana na ya mwanajeshi mwingine aliyefika kwenye ofisi za Mwananchi jana asubuhi kutoa taarifa ya mlipuko huo na kueleza kuwa takriban watu saba walijeruhiwa kwenye kambi hiyo na kukimbizwa hospitalini.

Alisema hali hiyo ya wasiwasi inasababisha washindwe kukamilisha zoezi la kufanya usafi na kazi ya kutafuta mabaki ya mabomu katika maeneo ya kambi hiyo kuwa ngumu.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema bomu lililolipuka jana lilisababisha hofu kubwa kwa baadhi ya raia wa eneo hilo, ambao wengi wao walipoteza ndugu na nyumba zao wakati wa milipuko ya kwanza iliyochukua maisha ya watu zaidi ya 26, kubomoa nyuma zaidi ya 800 na kusababisha watu zaidi ya 8,000 kukosa makazi.

Grace Songo, aliyedai kupata matatizo ya moyo kutokana milipuko hiyo, alisema: "Ingawa mlipuko huu wa leo haujasababisha madhara makubwa kwa raia, ni hatari kwa sababu tunapata mshtukuko mkubwa."

Plasda Njimbari, 35, alisema mbali na kulipuka kwa bomu, milipuko mingine zaidi ya mitatu husikika kati ya saa 9:00 usiku na saa 10:00 alfajiri kila siku.

"He! We uko dunia gani hapa. Siku hizi hapaitwi Mbagala, hii ni Baghdad kwa sababu kila siku ni milipuko kwa kwenda mbele," alisema Njibari.

Alisema: "Utaratibu huu ambao wanajeshi wameuanzisha wa kulipua mabomu usiku ni hatari zaidi kuliko mchana kwa sababu baadhi yetu tunaishi kwenye nyumba zenye nyufa na ziko kwenye hatari ya kuanguka hivyo ipo siku wataongeza maafa."

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alikiri kuwepo kwa mlipuko wa bomu la jana na kusema kuwa hayakuwa na madhara makubwa katika eneo hilo.

"Ni kweli kuna bomu limelipuka, lakini kwa muujibu wa taarifa za kijeshi walizonipa wao wenyewe, hilo lilikuwa ni kiwashio tu na sio bomu na hakikuwa na madhara makubwa," alisema Lukuvi.

"Hata kama kilipuka chenyewe, hakiwezi kuwa na madhara makubwa kwa sababu hakina uwezo wa kusafiri zaidi ya kilomita moja".

Kuhusu majeruhi, Lukuvi alisema: "Mimi sifahamu kuhusu suala la majeruhi, isipokuwa taarifa niliyopewa na wanajeshi wenyewe ni kwamba kiwashio hicho hakikuleta madhara makubwa".

Lukuvi aliwataka wakazi wa mbagala kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwao.

Ikulu yawabana makatibu wakuu


AWAZUIA KUWA WENYEVITI WA BODI ZA MASHIRIKA


BAADA ya kuwazuia wabunge kuwa wajumbe kwenye taasisi za kifedha, mianya ya ufisadi imezidi kubanwa baada ya Ikulu kuandaa waraka ambao utawaondoa makatibu wakuu wote katika nafasi za uenyekiti wa bodi za mashirika ya umma.

Katikati ya wiki, gavana wa Benki Kuu (BoT), alitoa maagizo kuwa taasisi za kifedha za umma hazitaruhusiwa kuwateua wabunge kuwa wajumbe wa bodi za taasisi hizo ili kuondoa mgongano wa kimaslahi.

Kwa mujibu wa duru za habari za kuaminika, agizo la Ikulu limetolewa na katibu mkuu kiongozi, Philemon Luhanjo. Habari hizo zinasema hatua hiyo imefikiwa ili kuondoa mgongano wa kimaslahi katika utumishi wa umma.

Kaimu msajili wa hazina, Geoffrey Msella alikiri jana kuwa alipata taarifa za waraka huo, lakini akasema hajapata barua rasmi kutoka kwa katibu mkuu kiongozi.

"Nafikiri, inawezekana amewaandikia kwanza makatibu wakuu wenyewe na baadaye anaweza kuleta kwetu, lakini hadi sasa (jana) sijapata taarifa rasmi," alisema Msella.

Alipoulizwa kuhusu waraka huo, Luhanjo alisema hakuwa katika nafasi nzuri kuzungumza. "Siwezi kuzungumza kwa sasa nipo kwenye mkutano," alisema Luhanjo kwa kifupi jana jioni.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe alikiri kupata taarifa hizo alipohojiwa na Mwananchi, lakini akasema si rasmi bali amesikia.

Kutolewa kwa waraka huo wa kudhibiti watendaji hao wakuu wa wizara ni moja ya hatua kubwa za serikali katika kuimarisha utawala bora na kuondoa mgongano wa kimaslahi.

Baadhi ya makatibu wakuu ambao ni wenyeviti wa bodi za mshirika ya umma hadi sasa, ni pamoja na Bliandina Nyoni wa Wizara ya Afya. Kwa sasa, Nyoni ni mwenyekiti wa bodi ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii ( NSSF).

Mwingine ni Ramadhan Kijjah ambaye kwa sasa ni katibu mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi. Kijjah ni mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi wa Pesheni kwa Mashirika ya Umma (PPF) na Mfuko wa Jamii kwa Watumishi wa Serikali (PSPF).

Kwa mantiki hiyo, makatibu wakuu watabaki kuwa wajumbe wa bodi kutokana na mwingiliano wa shughuli za kiutendaji.

Kipanya leo

Sawa Mkuu

Makamu wa Rais Dk. Shein akikabidhi Mwenge wa Uhuru
Image
Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein akimkabidhi Mwenge wa Uhuru, kiongozi wa mbio za mwenge mwaka huu kitaifa Kheir Ahmada Mwawalo kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, baada ya kuuwasha rasmi kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza jana. Kushoto ni Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Prof. Juma Kapuya. (Picha na Amour Nassor).

Mohammed Dewji amkana Juma Kaseja

Mohammed Dewji amkana Juma Kaseja
Kocha mpya wa African Lyon Eduardo Filipe Almeida(katikati) akitambulishwa kwa waandishi wa habari na Mkurugenzi wa timu Mohamed Dewji(kulia) katika halfa fupi jijini jana.
Na Mwandishi Wetu

AFRICAN LYON imemtambulisha kocha wake mpya Mreno Eduardo Filipe Almeida ambaye atainoa timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara huku ikisema imejitoa katika suala la kumtaka Juma Kaseja.

Akimtambulisha kocha huyo kwa waandishi wa habari jana katika ofisi zake jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu, Mohamed Dewji alisema kocha huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja kufundisha klabu hiyo.

Alisema Mreno huyo alishawahi kufundisha kikosi cha vijana wa umri chini ya miaka 13 na 16 katika timu kongwe za Ureno za Benfica na Porto kabla ya kupata mkataba Hongkong. Katika hatua nyingine Dewji amekanusha madai kuwa timu hiyo imemsajili kipa wa Yanga, Juma Kaseja.

Dewji alikiri kufanya mazunguzmzo na kipa huyo lakini hawaafikiana naye kwa madai kuwa dau alilotaka lilikuwa ni kubwa mno.

Dewji alisema kuwa timu yake inahitaji kipa kijana zaidi ambaye wanaweza kumtumia zaidi ya misimu mitatu ya ligi na hivyo umri wa Kaseja pia umekuwa ni kikwazo cha wao kumhihitaji.

" Tunao vijana wengi wa umri mdogo ambao walicheza vizuri wakati wa mechi za kutafuta kupanda daraja. Tulihitaji wachezaji wachahe wenye uzoefu ili kuwapa changamoto vijana wetu wachanga na ndiyo maana tukamfuata Kaseja," alisema Dewji.

Hata hivyo Dewji hakuwa tayari kueleza Kaseji alihitaji kiasi gani ili asajiliwe na klabu hiyo ya African Lyon yenye makazi yake Mbagala wilayani Temeke.

Katika hatua nyinine Dewji alisema kuwa ujenzi wa uwanja wa kisasa katika eneo la Mbagala tayari umeshaanza katika hatua za awali na utakuwa na nyasi za bandia.

Wazungu wamwaga Sh milioni 120 kwa Simba



KLABU ya daraja la kwanza ya Norway imesema ipo tayari kutoa kitita cha dola 120,000 (kama zaidi ya Sh milioni 120) kwa Simba ili kuwasaijili wachezaji wake wawili, Henry Joseph na Emeh Izuchukwu.

Izuchukwu raia wa Nigeria tayari yupo Norway akiendelea kufanya mazoezi na timu hiyo yenye makao yake makuu katika Manispaa ya Kongsvinger IL.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa uongozi wa Kongsvinger upo tayari kutoa kitita cha dola 70,000 kwa Izuchukwu na dola 50,000 kwa Henry kuwasajili kwa msimu ujao wa ligi.

"Unajua weyewe wameona Emeh bado kijana, hivyo watatoa dola 70,000 na Henry dola 50,000. lakini hata hivyo wametakiwa kusubiri kidogo kwa kuwa Simba walikuwa na makubaliano mengine na klabu ya Molde FK kupitia wakala anayetambulika na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), Mehd Rehmtullah.

"Unajua huenda wale Molde FK wakatoa fedha zaidi, ndio maana uongozi wa Simba unaendelea kuvuta subira, umetoa muda kidogo kuisubiri hiyo timu ya kwanza ili kujua uamuzi wake.

"Hata hii timu nyingine (Kongsvinger) iliwaona wakati wakifanya majaribio na Molde FK ambao wanasubiri kuanza kwa kipindi cha usajili ili waseme wanatoa kiasi gani halafu Simba itaamua," kilieleza chanzo.

Imeelezwa kuwa wakala, Rehtmtullah ndiye aliyewashauri Simba kuwapa nafasi Emeh na Henry kwenda kufanya mazoezi na Kongsvinger ili ikiwezekana watoe dau au kama hata si wao, klabu nyingine za Norway ziwaone kama ambavyo waliweza kuonekana wakiwa na Molde FK.

"Kweli nilishauri iwe hivyo kwa kuwa watu hao wameonyesha nia ya kutaka kuwasajili kama itakuwa inawezekana. Nikaona ni wazo zuri ndiyo maana tumetoa nafasi kwa Henry amalize majukumu ya taifa halafu akaungane na Emeh," alisema Rehmtullah alipozungumza na Mwanaspoti.

Lakini alipoulizwa suala la ofa waliota Wanorway hao alisema; "ameonyesha kweli wanawataka, wametoa ofa naweza kusema si mbaya kwa kuanzia lakini hili si suala langu na wanaoweza kulizungumzia ni Simba wenyewe," alisema wakala huyo.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji alisema wanafanya mambo yote kwa wakati mmoja. Tunazungumza na timu ya sasa na pia tunasubiri ile ya awali.

"Kuna wakala na tunashulikia mambo yote kupitia yeye, hivyo tusingependa kuchanganya mambo kwanza kwa kuwa bado kuna mazungumzo. Tukijua kila kitu kwa uhakika basi mara moja tutawaeleza," alisema Dewji.

Timu ya Kongsvinger, si timu kubwa sana na inatokea kwenye manispaa ndogo ya Kongsvinger iliyo Kusini Mashariki mwa Norway. Ilianzishwa Januari 31 mwaka 1892 na inatumia jezi za rangi nyekundu na nyeupe ikiwa nyumbani au bluu tupu ukiwa ugenini.

Haijawahi kutwaa ubingwa wa Norway zaidi ya kushika nafasi ya pili na ya tatu na miaka kadhaa haijawahi kuwa na wachezaji kutoka Afrika, badala yake mwaka huu kikosi chake kinaundwa na wachezaji wengi wenyeji na wageni wachache kutoka nchi jirani za Sweden, Luxembourg na Colombia kutoka Amerika Kusini.

Kocha mkuu wa Simba Phiri kuhamia Yanga?

Phiri: Mimi Yanga? Acheni masihala

KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Phiri amesema anaendelea kusaka wachezaji kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake, lakini ameshangazwa na habari kuwa atajiunga na Yanga na ameziita habari hizo kuwa ni masihala makubwa.

"Yanga! Kwa nini? Kwani kocha wao (Dusan Kondic) ameondoka? Nani kasema? Kila mtu anaweza kusema lake ila mimi nina mkataba na Simba na wala sijazungumza na Yanga.

Nakuhakikishia naelekeza nguvu zangu Simba na kila kitu ninafanya kwa ajili ya Simba kwa kipindi hiki,� alisema Phiri jana Ijumaa alipozungumza na Mwanaspoti kwa simu kutoka Zambia.

Phiri raia wa Zambia alisema hawezi kufanya kitu ambacho kitachanganya mipango yake; "Waambie niko Simba na hata huku ninafanya kazi za Simba," alisisitiza kocha huyo mpole.
Wakati Phiri akisema hivyo, Kocha Mkuu wa Yanga, Dusan Kondic aliiambia Mwanaspoti jana Ijumaa kuwa kama viongozi wa Yanga watakuwa wameamua hivyo, atamkaribisha Phiri.

"Suala hili wanaweza kulizungumzia viongozi, lakini ni kitu kibaya sana ambacho mtu anaweza kujitangazia tu. Mimi nipo Yanga, naendelea na kazi za Yanga kwa ajili ya msimu ujao tena kwa umakini mkubwa. Lakini kama yatatokea mabadiliko mimi ni kocha. Kukaa katika klabu kwa siku kadhaa na kuondoka si kitu kigeni," alisema raia huyo wa Serbia.
Kwa upande wa uongozi wa Yanga, Katibu Mkuu wa klabu hiyo kongwe nchini, Lucas Kisasa alisema hawana mpango wowote na Phiri.

"Tunafikiria vitu vingine kabisa, suala la kocha ni kwamba Dusan Kondic ndiye kocha mkuu wa Yanga. Naomba watendeeni haki wasomaji wenu kwa kuwaandikia habari za kweli. Kwa kifupi hatuna mpango huo," alisema Kisasa.
Mwanaspoti ilipiga mguu hadi kwa Mfadhili wa Yanga, Yusuf Manji ambaye pia alisisitiza kuwa hizo taarifa ni mpya kwake na anazisikia kwa mara ya kwanza.

"Tayari tuna Kondic ambaye ndiye kocha bora Tanzania, amefanya karibu kila kitu na Yanga wanajivunia. Timu imechukua ubingwa ikiwa na mechi mkononi, tumetoa mfungaji bora, tuna wachezaji wanatakiwa Ulaya na kwingine kama China. Hatuna mpango wa kutaka kocha mwingine,' alisema Manji.

Lakini kwa upande wa Simba kupitia mwenyekiti wake wa usajili, Kassim Dewji wamesisitiza kwamba Phiri ana mkataba na klabu hiyo na hakuna mpango wowote wa kumwachia aende Jangwani.

Taarifa ya baadhi ya vyombo vya habari jana zilisema kuwa kocha huyo anataka kujiunga na Yanga jambo ambalo lilizua mjadala sehemu mbalimbali nchini.

Kaseja, Sunguti watemwa Yanga


SIKU saba kabla ya kumalizika kwa mkataba wake wa mwaka mmoja, Kocha wa Yanga, Dusan Kondic amemtema rasmi kipa wake, Juma Kaseja.

Kaseja, aliyesajiliwa na Yanga kwa kitita cha dola 30,000 (Sh milioni 36) msimu uliopita ni miongoni mwa majina matano ambayo Kondic ameyapeleka kwa uongozi kuwa waachwe.

Pamoja na Kaseja, Yanga imewatema washambuliaji wake wawili, Gaudence Mwaikimba na mkongwe, Maurice Sunguti aliyeibuka mfungaji bora na kinara wa mabao misimu miwili iliyopita.

Kondic pia amewatema wachezaji wawili watoro sugu, Laurent Kabanda ambaye alikwenda kwao Congo na Credo Mwaipopo aliyetoka kwenda Sweden kabla ya kurejea miezi kadhaa iliyopita.

Habari za uhakika kutoka Yanga zinasema kuwa kikao cha juzi Alhamisi cha uongozi, kocha Kondic na mfadhili, Yusuf Manji umepitisha uamuzi huo na majina hayo matabo yatatangazwa wakati wowote kuwa wameachwa.

Habari hizo zenye uhakika ni kuwa Yanga imemuacha Kaseja baada ya Kondic raia wa Serbia kumuweka katika orodha ya wachezaji asiowahitaji tena kwa ajili ya msimu ujao na hasa baada ya kupata habari kuwa kipa wake wa Serbia, Obren Curkovic anarejea.

Kondic amefanya hivyo ikiwa ni siku chache baada ya kuiambia Mwanaspoti kuwa kipa namba moja wa Simba, Ally Mustapha 'Barthez' ni bora kuliko Kaseja.

Katika kikao hicho, Mserbia huyo aliueleza uongozi huo kwamba pamoja na ubora wa Kaseja katika mambo mengine lakini kasoro ya umbo na hasa ufupi ndio kimefanya asitake kuendelea naye.

Kondic alisema hakuwahi kumtaka Kaseja na hata msimu uliopita alitua Jangwani kutokana na siasa za Yanga na Simba, lakini halikuwa chaguo lake.

Tayari kocha huyo ameanza mipango ya kuhakikisha wanasajili kipa mwingine hapa nchini lakini ikiwa ni baada ya kurejea kwa kipa Mserbia, Obren Curkovic ambaye aliondoka nchini kwa hofu ya vitisho na kwenda kwao Serbia, baadaye Austria kufanya majaribio ambako anaelezwa ameshindwa.

Kwa upande wa Mwaikimba na Sunguti, Kondic alikieleza kikao hicho kwamba wameshindwa kuonyesha mchango wowote hata pale alipowapa nafasi ya kufanya hivyo, lakini Sunguti ikiwa ni kutokana na umri kumtupa mkono.

Kondic amekieleza kikao hicho kwamba, kitu muhimu kwa Yanga ni kufanya usajili wa wachezaji wachache tu huku akisisitiza kuwa Nurdin Bakari 'Kibajaji', Ben Mwalala na Mike Baraza hawatakwenda popote kwani anawahitaji kwa msimu ujao.

Kondic amewaweka mabeki Yusuf Hamis na Abuu Mtiro na Mkenya, George Owino katika orodha ya wachezaji watakaouzwa kwa kuwa bado wana mkataba na jeshi hilo la Jangwani.

Wengine ambao Kondic amewaweka katika orodha ya kuuzwa nje ya nchi ni Nadir Haroub 'Cannavaro' (Vancouver-Canada), Shadrack Nsajigwa (Ufaransa) na Boniface Ambani (China).

Akizungumza na Mwanaspoti jana Ijumaa, Katibu Mkuu wa Yanga, Lucas Kisasa alikiri kuwa na kikao hicho na kusema kilihusu mambo ya Yanga na si kwa ajili ya taarifa kwenye vyombo vya habari.

"Kweli tumekutana, lakini ilihusu mambo ya Yanga na tusingependa yazungumziwe hadharani. Tukiwa tayari tutawaita na kuwaeleza," alisema Kisasa.

Lakini kwa upande wa Kondic alisisitiza kwamba, usajili mpya hautakuwa na mabadiliko makubwa kama wengi wanavyofikiri.

"Kweli tulikutana, lakini ni mambo yetu ya ndani ukiwamo usajili. Tumejadili mengi ukiwamo usajili, kweli kuna ambao wataachwa, wengine watauzwa na wengine tunawasiliana nao kwa ajili ya usajili.

Ila hatutakuwa na mabadiliko makubwa kwa kuwa tuna wachezaji wa kutosha na kumbuka kuna Joseph Shokokoti na John Njoroge ambao wako Tusker kwa mkopo. Pia tuna chipukizi wetu ambao tuliwapandisha mwaka jana. Hivyo ni sehemu chache tutaongeza.

Mwanaspoti ilimsaka mfadhili Mkuu wa Yanga, Yusuf Manji ambaye alimsajili Kaseja mwaka jana na kuweka rekodi ya usajili kwa wachezaji wandani ikiwa ni pamoja na kumpa mshahara wa Sh milioni moja ambaye alisema suala hilo ameachiwa Kondic.

"Tunaweza kusajili mchezaji yeyote kama anaweza kuisaidia Yanga hata kama itakuwa Sh milioni 50, lakini kocha ndiye anatuelekeza wapi twende kwenye hili. Hivyo kama kumbakiza au kumuacha mchezaji ni suala la kocha," alisema Manji.

Akizungumza jana kuhusu hilo, Kaseja alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kirefu kwa kuwa ameelekeza nguvu zake kwenye mechi ya leo Jumamosi ya fainali ya Kombe la Taifa.

"Mkataba haujaisha nitakuwa nimeachwa vipi, hapo sielewi lakini naomba mnipe muda kwa kuwa nikiamua kuzungumza nitakuwa na mengi tu. Ila naelekeza nguvu zangu katika mechi ya kesho (leo Jumamosi) ya Taifa Cup baada ya hapo naweza kuzungumza vizuri," alisema Kaseja ambaye ndiye kipa bora namba moja nchini.

Senin, 25 Mei 2009

The force of the nuclear blast was 10 to 20 kilotons, Russian Defense Ministry spokesman Alexander Drobyshevsky told the state-run RIA-Novosti news


NKorea says it conducted 2nd nuclear test

Visitors stand near the mock North Korean Scud-B missile, standing at center in background, and other South Korean missiles on display at Korea War Memorial Museum in Seoul, South Korea, Monday, May 25, 2009. North Korea announced Monday that it successfully carried out an underground nuclear test, weeks after threatening to restart its rogue atomic program

SEOUL, South Korea – North Korea defiantly declared Monday that it carried out a powerful underground nuclear test — reportedly many times larger than a 2006 test — in a major provocation in the escalating international standoff over its rogue nuclear and missile programs.

The regime also test-fired a short-range, ground-to-air missile Monday from the same northeastern site where it controversially launched a rocket last month, the Yonhap news agency reported, citing unnamed sources. That liftoff, widely believed to be a cover for a test of its long-range missile technology, drew censure from the U.N. Security Council.

North Korea, incensed by the condemnation of the April 5 rocket launch, had warned last month that it would restart it rogue nuclear program, conduct an atomic test and carry out long-range missile tests.

On Monday, the country's official Korean Central News Agency said the regime "successfully conducted one more underground nuclear test on May 25 as part of measures to bolster its nuclear deterrent for self-defense."

Defense officials in Russia, which shares a short border with North Korea, confirmed a nuclear test in northeastern North Korea, the ITAR-Tass news agency said.

President Barack Obama said a nuclear test would constitute an act of "blatant defiance" of the U.N. Security Council and a violation of international law.

"These actions, while not a surprise given its statements and actions to date, are a matter of grave concern to all nations," he said, calling for international action in a statement from Washington. "North Korea's attempts to develop nuclear weapons, as well as its ballistic missile program, constitute a threat to international peace and security."

"If North Korea carried out a nuclear test, it would clearly violate U.N. Security Council resolutions," chief government spokesman Takeo Kawamura told reporters in Tokyo. "We will definitely not tolerate it."

Japan will request an emergency U.N. Security Council meeting to discuss North Korea, Vice Foreign Minister Mitoji Yabunaka said, according to the Kyodo news agency.

North Korea did not say where or when the test took place. But seismologists from the U.S., South Korea and Japan reported activity shortly after 9:50 a.m. in a northeastern area where North Korea conducted its first nuclear test in 2006.

An emergency siren sounded in the Chinese border city of Yanji, 130 miles (200 kilometers) northwest from the test site. A receptionist at Yanji's International Hotel said she and several hotel guests felt the ground tremble.

The Japan Meteorological Agency measured the seismic activity at magnitude-5.3, quake expert Gen Aoki said. The Korea Institute of Geoscience and Mineral Resources in Seoul reported seismic activity in Kilju in North Hamgyong Province — the same area where North Korea carried out a nuclear test in October 2006.

North Korea boasted that Monday's test was conducted "on a new higher level in terms of its explosive power and technology of its control" than one carried out in 2006.

The force of the nuclear blast was 10 to 20 kilotons, Russian Defense Ministry spokesman Alexander Drobyshevsky told the state-run RIA-Novosti news agency.

An explosion of that size would be many times more than North Korea managed in 2006. U.S. intelligence officials said the 2006 test measured less than a kiloton; one kiloton is equal to the force produced by 1,000 tons of TNT.

Radiation levels, tested after the blast, were normal, RIA-Novosti cited a spokeswoman for the meteorological official in the Primorye region as saying.

The reported test-fire of the short-range missile took place at the Musudan-ri launchpad on North Korea's northeast coast, Yonhap said. Sources described it as a ground-to-air missile with a range of 80 miles (130 kilometers).

Japan's coast guard had said Friday that North Korea warned ships to steer clear of waters off a coastal city near the missile launch site, suggesting Pyongyang was preparing for a missile test. Yonhap also had reported brisk activity along the northeast coast over several days last week.

South Korean troops were on a high alert but there was no sign North Korean soldiers were massing along the heavily fortified border dividing the two nations, according to an official at the Joint Chiefs of Staff who spoke on condition of anonymity, citing agency policy.

The two Koreas technically remain at war because their three-year conflict ended in a truce, not a peace treaty, in 1953.

North Korea is believed to have at least a half-dozen atomic bombs. However, experts say North Korean scientists have not yet mastered the miniaturization technology for mounting a nuclear device onto a long-range missile.

The 2006 test, which drew tough U.N. sanctions, prompted North Korea's neighbors and the U.S. to push for a pact offering Pyongyang energy aid in exchange for dismantling its nuclear program. North Korea signed the accord in February 2007, but the process has been stalled since last July.

___

Associated Press writers Kelly Olsen and Jae-soon Chang in Seoul, Pamela Hess in Washington, Steve Gutterman in Moscow, Shino Yuasa in Tokyo and AP researcher Zhao Liang in Beijing contributed to this report.