Rais  wa  Somalia , ambaye  madaraka  yake  yako hatarini  akiwa  katika  jumba  la  rais  mjini Mogadishu, ametangaza  leo  hali  ya  hatari  katika juhudi  za  kupambana  na   mashambulizi  makali ya  wiki  sita  ya  wapiganaji.
Tangazo  hilo  la   rais  Sharif  Sheikh  Ahmed limekuja  huku  kukiweko   majadiliano  juu  ya kuchukuliwa  hatua  mpya  ya  kuingilia  kati kuyaondoa  makundi  ya   wapiganaji  wa  Kiislamu, miezi  sita  tu  baada  ya  majeshi  ya  Ethiopia kufikisha  mwisho  hatua  yao  iliyodumu  miaka miwili  ya  kuingilia  kati.
Wiki  sita  baada  ya  kuzuka  mapigano  makali ambayo  yamesababisha  vifo  vya  zaidi  ya  watu 300, udhibiti  wa  serikali  hiyo  katika  baadhi  ya maeneo  ya  mji  mkuu,  Mogadishu,  unapungua. Akizungumzia  kuhusu  hali  nchini  Somalia makamu  wa  rais  wa  Kenya  Kalonzo  Musyoka amesema.
Umoja  wa  Afrika  umeeleza  tena  leo  wasi  wasi wake  na  kuidhinisha  wito  wa  hapo  kabla uliotolewa  na  Somalia  wa  kuomba  usaidizi  wa kijeshi  kutoka  nje.
Mwenyekiti  wa  halmashauri  ya  Umoja  wa  Afrika, Jean Ping,  amesema   katika  taarifa  kuwa  serikali ya  Somalia  ina  haki  ya  kuomba  msaada  kutoka kwa  mataifa  wanachama  wa  Umoja  wa  Afrika pamoja  na  jumuiya  ya  kimataifa,  kwa  jumla.
Tidak ada komentar:
Posting Komentar