Chombo   kinachohusika  na  uchaguzi  nchini  Iran , baraza  la  wadhamini, limekiri  kuwapo  na  hitilafu katika  uchaguzi  wa  rais  ambao  umemrejesha  rais Mahmoud  Ahmadinejad  madarakani.
Msemaji  wa  baraza  hilo  ameiambia  televisheni  ya taifa  ya  Iran  kuwa  kura  kadha  zilizopigwa  katika majimbo  50  zimepindukia  idadi  ya  watu  wenye haki  ya  kupiga  kura.
Wagombea  watatu  waliokuwa  wakigombea  kiti hicho  pamoja  na  Ahmadinejad   wanalalamika kuwa  hadi  majimbo  170  kutoka  jumla  ya  majimbo 366  ya  uchaguzi   yamekumbwa  na  hitilafu  hizo.
Wakati  huo  huo , kiongozi  wa   upinzani  nchini Iran,  Mir Kossein  Musavi,  amewataka wanaomuunga  mkono  kuendelea  na  maandamano dhidi  ya   madai  ya  udanganyifu.
Mousavi  amewaambia   wanaomuunga  mkono kuwa  wanapaswa   kupuuzia  marufuku dhidi  ya maandamano, lakini  wanapaswa  kuonyesha uvumilivu  baada  ya  maafisa  kuwakamata  zaidi  ya waandamanaji  450  mwishoni  mwa  juma.
Mapambano  katika  mitaa  ya  Tehran  imesababisha watu  kumi  kuuwawa  na  zaidi  ya   wengine  100 kujeruhiwa  siku  ya  Jumamosi. Serikali  ya  Iran inalaumu  ghasia  hizo  kuwa  zinaungwa  mkono  na mataifa  ya  magharibi.
Tidak ada komentar:
Posting Komentar