Uingereza  imeahidi   kutoa  paundi  milioni  tano zaidi  kama  msaada  kwa  Zimbabwe  leo  Jumatatu, na  kusifu   hatua   za  maendeleo  zilizofikiwa    na serikali  mpya  ya  umoja  wa  kitaifa,  lakini imehimiza  mageuzi  zaidi  baada  ya  mazungumzo muhimu  kati  ya   viongozi  wa  nchi  hizo  mbili.
Akizungumza  baada  ya  mazungumzo  na  waziri mkuu,  Morgan Tsvangirai , ikiwa  ni  mazungumzo ya  kwanza  ya  aina  hiyo  na  kiongozi  wa Zimbabwe  kwa  muda  wa  miongo  miwili, waziri mkuu,  Gordon  Brown,  ameahidi  msaada  zaidi, iwapo  mpango  wa  mageuzi  utapata  kasi  zaidi.
Fedha  hizo  za  ziada  dola  milioni  8.2  zinafikisha kiasi  cha  paundi  milioni  60, ikiwa  ni  msaada   wa mpito  kwa  serikali  ya  Zimbabwe  mwaka  huu, Brown  amesema , ambaye  serikali  yake  ilikuwa inapingana   na  utawala  wa  rais  Robert  Mugabe kwa  muda  mrefu.
Lakini  katika  ishara  nyingine  ya  kuchukua tahadhari, Brown  amesema   kuwa  msaada  huo  wa ziada  utapitia  katika  mashirika  ya  kutoa  misaada badala  ya   kwenda  katika  serikali  ya  Zimbabwe moja  kwa  moja.
Tidak ada komentar:
Posting Komentar