Senin, 22 Juni 2009

Waziri wa zamani wa rwanda afungwa jela miaka 30.

Mahakama ya umoja wa mataifa inayowahukumu wale waliopanga mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994 imemhukumu kwenda jela miaka 30 waziri wa zamani wa mambo ya ndani anayeshutumiwa kuwadanganya maelfu ya watu kujificha mlimani kabla ya kuuwawa.
Mahakama hiyo ya kimataifa ya uhalifu wa kivita, yenye makao yake nchini Tanzania, imesema callixte Kalimanzira, mshirika wa karibu wa rais na waziri mkuu wakati wa mauaji, alipatikana na hatia ya mauaji ya kimbari na kula njama ya kufanya mauaji.
Wanamgambo wa Kihutu waliwauwa Watutsi walio wachache wapatao 800,000 pamoja na Wahutu waliochukua msimamo wa kati katika siku 100 za mauaji ambayo yaliishtusha Afrika na dunia kwa jumla.

Tidak ada komentar:

Posting Komentar