



UFUMBUZI wa mvutano wa uchimbaji wa nishati ya mafuta na gesi asilia visiwani Zanzibar uko katika hatua za mwisho baada ya mshauri mwelekezi kutoka kampuni ya Aupec LTD ya Uingereza kuwasilisha taarifa ya mapendekezo ya namna ya kugawana raslimali hiyo kwa serikali ya Muungano na ya Mapinduzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana juu ya mafaniko na changamoto kwa wizara yake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia mambo ya Muungano, Mohamed Seif Khatib alisema taarifa ya mshauri huyo kwa sasa iko katika hatua nzuri ya utekelezaji wa mapendekezo.
"Baada ya kugombana kwa muda mrefu kuhusu uchimbaji wa nishati hiyo, serikali ilimtafuta mshauri mwelekezi kwa lengo la kutushauri namna ya kugawana raslimali hiyo na kwa sasa tayari amekwishawasilisha taarifa rasmi ya mapendekezo katika serikali zote mbili namna ya kugawana raslimali hiyo," alisema Khatib.
Alisema gharama za kumlipa mshauri huyo zimelipwa na serikali zote mbili yaani serikali ya muungano na serikali ya mapinduzi.
Mbali na taarifa hiyo ya mafuta na gesi asilia, Waziri Khatib alisema serikali zote mbili zimeona umuhimu wa kuratibu shughuli za uvuvi kwa kuunda chombo maalum kwa lengo kuweka utaratibu wa kugawana mapato yanayotokana na uvuvi kwa ajili ya kuzinufaisha serikali zote mbili.
Alisema sheria ya Mamlaka ya Uvuvi katika ukanda wa Bahari Kuu imeainisha mgawanyo wa mapato yanayotokana na shughuli za uvuvi, ikieleza kuwa asilimia 50 hutumika kwa shughuli za uendeshaji wa mamlaka hiyo, wakati Serikali ya Muungano hupata 30 asilimia na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hupata asilimia 20.
Akizungumzia nafasi ya Zanzibar katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Waziri Khatibu alisema ili kufaidi matunda ya ushirikiano huo kwa sasa Zanziba itakuwa na sehemu yake inayotegemea tofauti na awali ilipokuwa ikishiriki kupitia Serikali ya Muungano.
"Kwa sasa Zanzibar imeingiza miradi yake nane ya maendeleo katika umoja huo ambayo utekelezaji wake utaiwezesha kunufaika moja kwa moja na ushirikiano huo," alisema Waziri Khatib.
Pia Waziri Khatib alizungumzia manufaa ya misaada ya kiuchumi na ya maendeleo inayotolewa na wafadhili kwa Serikali ya Muungano akisema umewekwa utaratibu wa kuhakikisha kwamba Zanzibar nayo inapata mgawo wake.
Alitaja mafaniko mengine ya wizara yake kuwa ni kuundwa kwa Tume ya Fedha ya pamoja kwa lengo la kuhakikisha kwamba Zanzibar inachangia na kunufaika na mapato ya taifa.
Alisema tume hiyo imetoa mapendekezo ya namna ya serikali zote zitakavyochangia uendeshaji wa shuguli za Muungano.
Hata hivyo, alisema bado kuna changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja malumbano baina ya viongozi wa serikali zote kwa kutumia vyombo vya habari badala ya kutumia vikao kutatua tofauti zinazojitokeza, akisema jambo hilo linawachanganya wananchi.
Akizungumzia muundo wa Muungano, Waziri Khatib alisisitiza kwamba mfumo wa sasa ndio unaofaa kwa kuwa mekubaliwa na wananchi wengi kwa mujibu wa taarifa ya maoni ya Kamati ya Jaji Kisanga.
May this new year bring many opportunities to your way,
to explore every joy of life
&
may your resolutions for the days ahead stay firm,
turning all your dreams into reality
and all your efforts into great achievements.
Happy New Year to you & your loved ones.
VATICAN CITY – Pope Benedict XVI warned in his Christmas message Thursday that the world was headed toward ruin if selfishness prevails over solidarity during tough economic times for rich and poor nations.
Speaking from the central balcony of St. Peter's Basilica, Benedict said he was trying to inspire hope in the world.
"Brothers and sisters, all you who are listening to my words: this proclamation of hope — the heart of the Christmas message — is meant for all men and women."
The traditional papal Christmas Day message "Urbi et Orbi" — Latin for "to the City and to the World" — usually covers the globe's hot spots, but this year Benedict also addressed the economic conditions worrying many across the planet amid near-daily news of layoffs, failing companies and people losing homes.
Benedict said his Christmas message applied to "wherever an increasingly uncertain future is regarded with apprehension, even in affluent nations."
"In each of these places may the light of Christmas shine forth and encourage all people to do their part in a spirit of authentic solidarity," Benedict said. "If people look only to their own interests, our world will certainly fall apart."
Benedict said he hoped the light of Christmas would radiate to places where "the basics needed for survival are missing."
Wearing a crimson mantle against a damp chill, Benedict told tens of thousands of people in St. Peter's Square that God's saving grace could "alone transform evil into good" and "change human hearts, making them oases of peace."
Benedict dedicated part of his message to Africa, singling out Zimbabwe, where hunger is spreading and deepening. He said that people there were "trapped for too long in a political and social crisis which, sadly, keeps worsening."
International pressure has been mounting for longtime Zimbabwe leader Robert Mugabe to step down, following disputed elections in March. Millions of Zimbabwe's people need food aid, and a cholera epidemic has sharpened problems in a country once considered African's breadbasket.
Suffering also continues in the war-ravaged region of Kivu in the Democratic Republic of Congo, and in Darfur, Sudan, the pope added. In Somalia, people are weighed down with "interminable sufferings" as "the tragic consequences of the lack of stability and peace," he said.
Benedict spoke of violence and tensions in the Middle East, lamenting that "the horizon seems once again bleak for Israelis and Palestinians."
He denounced what he called the "twisted logic of conflict and violence" and said he hoped dialogue and negotiation would prevail to find "just and lasting solutions to the conflicts troubling the region."
Benedict also cited Lebanon and Iraq.
Without naming any particular groups, the pope called for an end to "internecine conflict" dividing ethnic and social groups and disrupting peaceful coexistence. He also denounced terrorism "wherever" it continues to strike.
After reading a litany of the world's woes, the pope added a lighter touch, reciting holiday greetings in 64 languages, including Latin, the Church's official tongue.
The pope had rested for a few hours after celebrating Midnight Mass in St. Peter's Basilica in the early hours of Thursday.
During that ceremony, the pope lamented the suffering of children who are abandoned, living on the streets or forced to serve as soldiers in conflicts.
WASHINGTON – U.S. officials said Monday that they want answers from Russia on whether it is selling advanced surface-to-air missiles to Iran, a move the U.S. insists could threaten American troops in Iraq and Afghanistan. A senior military intelligence official said that while Moscow has sent out conflicting responses to reports on the sale of long-range S-300 missiles, the U.S. believes it is taking place. However, it appears that no equipment has yet been delivered to Iran, said the official, who spoke on condition of anonymity because of the sensitivity of the matter.
Russia's state arms export agency said Monday it is supplying Iran with defensive weapons, including surface-to-air missiles, but did not say whether they include sophisticated long-range S-300 missiles.
State Department spokesman Robert Wood said the U.S. is seeking clarification from Russia.
"We have repeatedly made clear at senior levels of the Russian government that we would strongly oppose the sale of the S-300," Wood said. "As the U.S. government has said before, this is not the time for business as usual with the Iranian government."
Iran currently has an antiquated missile defense system, dating back to the 1960s and 1970s, so the Russian sale would provide Tehran a much longer range, more mobile and lethal capability. With a range of roughly 75 miles, the Russian system would allow Iran to reach coalition forces operating in Iraq and Afghanistan, if the missiles were moved near the borders.
Both the U.S. and Israel have strongly opposed the sale, saying that supplying such an advanced anti-aircraft system to Iran would shift the military balance of power in the Middle East. It also would make any strike at Iran's first nuclear power plant — which Russia is helping to build — more difficult.
There have been indications that Russia intends to supply only defensive weapons to Iran, thus keeping in line with U.N. Security Council resolutions that impose sanctions on Iran for refusing to halt its uranium enrichment and prohibit supplying Iran with materials that could contribute to its nuclear program.
Officials acknowledge that the sale of the S-300 system is not prohibited by the resolution.
Israel and the United States fear that Iran could use the S-300 missiles to protect its uranium enrichment plant at Natanz or the country's first atomic power plant now under construction at Bushehr by Russian contractors.
The U.S. and other nations believe Iran is secretly developing nuclear weapons, but Iran insists its uranium enrichment program is intended solely for civilian energy needs.
While the possibility that the U.S. might launch an attack against Iran's nuclear facilities faded about a year ago, Israel has never ruled out a strike of its own, and is considered the nation most likely to take action.
Iran's president has said that Israel should be "wiped off the map."
The sale of S-300 missiles, said the military intelligence official, presents a decision point for Israel, since once the anti-aircraft system is in place it could deter any strike.
WAKATI Serikali ikitoa masharti magumu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kurejea vyuoni baada ya kugomea Sera ya Uchangiaji Elimu, uchunguzi wa awali uliofanywa na Jeshi la Polisi umeonyesha kuwa migomo na maandamano ya wanafunzi hao hayana uhusiano wowote na siasa.
Vyuo saba vya serikali vimefungwa baada ya wanafunzi kugoma kuingia madarasani wakidai wakiishinikiza serikali kufuta sera ya uchangiaji elimu ambayo wanadai kuwa ina ubaguzi katika utoaji wa mikopo na pia kutaka wpte wapewe mikopo kwa asilimia 100 bila ya kubagua iwapo sera hiyo itaendelea.
Migomo hiyo iliyotapakaa kwa kasi kwenye vyuo hivyo vya serikali ilisababisha baadhi ya menejimenti za vyuo hivyo kudai kuwa kuna vyama vinavyofadhili wanafunzi ili waitingishe serikali.
Lakini matokeo hayo ya awali ya uchunguzi wa polisi yanakata nguvu za menejimenti za vyuo vya elimu ya juu.
Kwa mujibu wa habari za kuaminika kutoka kwa timu hiyo ya polisi inayochunguza migomo na maandamano hayo, tatizo kubwa linalochochea migomo vyuoni ni menejimenti.
Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu matokeo ya uchunguzi huo, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Manumba alisema uchunguzi wa polisi bado unaendelea.
Kamishna Manumba alipouilizwa zaidi nini hasa kimebainika katika uchunguzi wa awali, alisisitiza, "Uchunguzi wa polisi ni mpana."
DCI Manumba aliongeza kwamba katika uchunguzi huo si rahisi kuanza kutoa matokeo sasa kwani uchunguzi bado unaendelea lakini akakiri hadi sasa hawajabaini siasa katika migomo na maandamano ya wanafunzi.
"Unajua uchunguzi wa polisi ni mpana, kusema sasa hivi tumebaini nini si sahihi. Uchunguzi unaendelea," alijibu DCI Manumba kwa kifupi.
"Nafikiri tusubiri matokeo ya uchunguzi kamili, tusianze kutoa majibu ya uchunguzi ambao bado unaendelea. Matokeo yatajulikana tu baada ya muda wa uchunguzi kukamilika."
Wakati Kamishna Manumba akisema hayo, habari za kuaminika zinasema matatizo ambayo wanafunzi wamekuwa wakilalamikia ni pamoja na menejimenti mbovu za vyuo vikuu nchini.
Kwa mujibu wa matokeo hayo ya uchunguzi wa awali tatizo jingine lililobainika ni Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ambayo wanafunzi hawakubaliani nayo.
Matokeo hayo ya uchunguzi wa polisi yatakuwa pigo kwa menejimenti za vyuo vikuu nchini hasa vile vya serikali, ambavyo vimekuwa vikihisi matatizo ya wanafunzi yanatokana na siasa.
Naye Exuper Kachenje anaripoti kuwa wakati Jeshi la Polisi nchini likiashiria kuwa hakuna chama cha siasa kinachojihusisha kufadhili migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu, mwananchi mmoja amejitokeza na kulipia gharama za tangazo la nusu kurasa kwenye gazeti kueleza kuwa siasa ndio chanzo cha migomo hiyo.
Mwananchi huyo ambaye hata hivyo hakutaja jina lake alitoa barua ya wazi kwenda kwa Bodi ya Mikopo na Serikali kupitia gazeti hili toleo la jana ukurasa wa 18, iliyokuwa na kichwa kisemacho "Chanzo cha Migomo Vyuoni /Nini Kifanyike".
Mwananchi huyo aliyejitambulisha kama mfanyakazi wa serikali na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro (SUA) alisema viongozi wa wanafunzi wakishirikiana na viongozi wa vitivo wa kila kozi na wawakilishi wa wanafunzi wamekuwa wakiendesha vikao usiku wa manane na kwamba wana pesa kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo vyama vya siasa.
“Wale viongozi wa wanafunzi wakishirikiana na viongozi wa vitivo vya kila kozi na wawakilishi wa wanafunzi wamekuwa wakiendesha vikao mpaka usiku wa manane. Hawa lazima wanapesa toka sehemu mbalimbali na vyama vya siasa kama ilivyoelezwa kwenye vyombo vya habari,” alieleza
Aliongeza kuwa baada ya vikao hivyo viongozi hao wamekuwa wakiwalazimisha kutii maamuzi yao bila kufikiri na kueleza kuwa asiyetii atachapwa viboko, akiongeza kuwa asilimia 75 ya wanafunzi wa SUA hawakupenda migomo na kwamba aliyehamasisha watu wasiingie madarasani ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu na yupo chuoni hapo.
Ameishauri serikali kutokubali kuburuzwa na iwafukuze viongozi wote waliopo sasa pamoja na kubinafsisha vyuo vyote vya umma ili ibakie na jukumu la ukopeshaji na kuwaelimisha wanavyuo kuwa mkopo si msaada wala haki.
Na Peter Zakhayo Daily News; Thursday,December 18, 2008 @20:00 | |||||
Baada ya kujibiwa hivyo, nilijua nini kimetokea kwa kuwa naelewa kabisa misimamo ya mzee wetu pale yanapojitokeza mambo ya kipuuzi, hasa katika suala la elimu. Kwa maana hiyo basi, nilimwomba atulie ili anieleze vizuri kilichotokea ili nami niweze kumsaidia. Baada ya kutulia, kwa mara nyingine nilimtaka anieleze kilichotokea kinagaubaga naye aliniambia hivi, “Nilimpelekea fomu za kunirejesha chuoni ili azijaze naye amenijibu kwamba ‘nenda kampelekee baba yako mpumbavu kama wewe akakujazie, mimi sishughulikii masuala ya watoto wapumbavu wanaogoma vyuoni”. Kwa upande wangu, sikuona kama uamuzi wa mzee wetu ulikuwa wa busara, hasa ikizingatiwa kwamba tatizo hilo si lake peke yake, bali linawahusu wanafunzi wote, bila kujali kama yeye alishiriki au hakushiriki. Kutokana na ukweli huo, ingawa nilikuwa katika nafasi nzuri ya kumsaidia mdogo wangu, nililazimika kuwasiliana na mzee wetu ili kujua kama kuna lingine lililojitokeza zaidi ya hayo niliyoelezwa ili napate kujua mahali pa kuanzia, naye alinipa majibu yaleyale. Nilipojaribu kumshawishi, mzee alikataa katu na kuniambia nisirudie kumuuliza juu ya suala hilo la kipuuzi na kuongeza kwamba yeye hawezi kumshughulikia mwanafunzi aliyegoma. Alisema hawezi kufanya hivyo kwani yeye hakushiriki kumshawishi agome na wala hakuwahi kumwambia kuwa hana uwezo wa kulipia kiasi cha ada kinachopaswa kukamilishwa na mzazi au mlezi wa mwanafunzi. Baada ya kupata majibu hayo kutoka kwa baba sikuwa na uamuzi mwingine zaidi ya kumsaidia mdogo wangu aweze kurejea chuoni. Nilisoma masharti yaliyopo katika fomu hiyo na kuijaza kisha niliisaini na kumwambia airejeshe chuoni pamoja na fedha anayodaiwa pindi wakati wa kufanya hivyo utakapofika.Ukweli ni kwamba tukio hilo lilinipa fundisho kubwa ndio maana nikaamua kuandika makala haya. Hiyo inatokana na ukweli kwamba wapo wanafunzi wengi ambao wamekumbwa na tatizo kama hilo lakini mpaka sasa hawajapata ufumbuzi. Wapo wanafunzi walioanza kulia kama mdogo wangu alivyokuwa akilia tangu siku ya kwanza baada ya vyuo vikuu kufungwa na mpaka sasa wanalia. Kibaya zaidi ni kwamba hawana la kufanya, kwani hakuna wakuwasaidia mpaka sasa.Ninapowaangalia wanafunzi hawa namkumbuka mwalimu wangu wa masomo ya Sosholojia na Saikolojia, hayati Profesa Samuel Mshana, alipotufundisha kwamba uamuzi utokanao na makundi una madhara makubwa. Alitufundisha kwamba tunapoishi na watu tukiwa kama kundi moja, tunapaswa kuchukua tahadhari kubwa, kwani tunaweza kudhani sote tunafanana, kumbe katika hali halisi hatufanani hata kidogo.Hivyo ndivyo ilivyotokea kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, ambao wakati wakijiandaa kugoma walikuwa wakidhani kuwa ni wamoja, lakini baada ya kufukuzwa, wamebaini kuwa wanatofautiana kwa kiasi kikubwa. Hivi sasa kila mmoja anakufa kivyake. Ukweli ni kwamba baada ya kufukuzwa, kila mwanafunzi ameshika njia yake na kwa bahati mbaya zaidi wale wenzangu na mimi wanaotokea katika familia masikini mambo si shwari kwa upande wao hata kidogo. Hili ni kundi la wanafunzi ambalo kwa sasa hawana nauli ya kurejea makwao, wanahangaika mitaani wakisubiri chuo kifunguliwe ili warudi kwenye neema. Wanafunzi hao sasa wamejifunza kuwa wenzao waliowarubuni kugoma, walikuwa hawana nia njema nao, kwani mwisho wa siku wameachwa peke yao. Walitakiwa kujua ukweli kuhusu hilo, chukua mfano wa mdogo wangu. Ukweli ni kwamba kama ningekuwa naishi mbali, inawezekana kabisa kwamba ndoto ya safari yake ya kupata shahada ya kwanza ingeishia njiani, kutokana na mgomo huo.Anaeleza kwamba hakuwahi kushiriki katika mgomo huo au kuunga mkono hata siku moja, lakini naye amefukuzwa kwa sababu ya mkumbo. Niandikavyo makala haya, wapo wanafunzi wengi ambao wapo tayari kurejea vyuoni kwa masharti yaliyowekwa, lakini hawana pa kuanzia. Hao ni wanafunzi waliokuja Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kujiunga na chuo, kwa nauli za mkopo vijijini kwao. Hao ni wanafunzi ambao kipato cha familia zao, kinatokana na kilimo cha msimu, hivyo baadhi yao wamekutwa na hicho kilichowakuta wakati wazazi wao hawana kitu mfukoni. Baadhi yao ambao wamefanikiwa kurejea makwao kwa nauli zilizotokana na posho kidogo wanayopewa chuoni, hivi sasa wanahaha kupata nauli ya kurejea chuoni. Wakati wao wapo katika hali hiyo, wenzao wanaotoka katika familia za kitajiri waishio Dar es Salaam, wanakwenda na kurudi chuoni kila siku wakitumia magari ya kifahari ya wazazi wao. Kwa wakati huu, wanafunzi hao wanapaswa kutambua kuwa si wamoja hata kidogo. Wanapaswa kutambua kuwa umoja walionao, ambao unasimamiwa na Serikali ya Wanafunzi unaishia katika mipaka ya chuo. Lakini, inapotokea mwanafunzi mmoja mmoja anapatwa na tatizo mtaani, umoja huo hauwasaidii kitu. Ingawa wanafunzi wengi wanalaani hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuwasimamisha masomo mpaka mwezi ujao, kwangu mimi nadhani hilo ni fundisho kubwa kwao kwa siku za baadaye.Wanafunzi wengi sasa wametambua kuwa maisha si lelemama hata kidogo! Wametambua kuwa serikali ikisema haina fedha ya kugharamia asilimia 100 ya masomo yao, maana yake ni nini. Kwa sasa, wanafunzi hao wanajua kazi iliyopo katika kutafuta fedha. Kwa sasa wanatambua serikali ilivyo na majukumu makubwa ya kuwasomesha na kuwapatia fedha za kujikimu. Wanajua kwamba fedha za matumizi, ambazo baadhi yao wamekuwa wakidai kuwa ni kidogo, kwa sasa ni nyingi, kwani upatikanaji wake mwanafunzi akiwa mtaani ni mbinde.Kutokana na ukweli huo, ni wazi kwamba tabia za uamuzi utokanao na mkumbo zitapungua kwa kiasi kikubwa katika vyuo vikuu, hasa vilivyokumbwa na dhahama ya kufungwa. Hiyo inatokana na ukweli kwamba hivi sasa kila mwanafunzi, amebaini kuwa yupo peke yake. Wanafunzi wanapaswa kutambua kuwa huo ndio ukweli, hivyo pindi watakaporejea vyuoni uamuzi wao katika masuala ya kitaaluma, haupaswi kuathiriwa na uchochezi wa makundi fulani. Huo ni ushauri wa bure kwa wanafunzi wanaotokea kwenye familia masikini.Kama hawaamini, wanapaswa kujiuliza kwamba tangu walipoondolewa vyuoni, ni lini uongozi wa Serikali za Wanafunzi uliwatafutia wafadhili wa kuwapatia fedha za kujikimu katika kipindi hiki kigumu? |
Na Jumanne Khasim Daily News; Monday,December 15, 2008 @12:20 | |||||
Katika uchaguzi huo uliofanyika jana kwenye ukumbi wa NSSF waterfront, Tenga alitangazwa mshindi kwa kupata kura 68 dhidi ya kura 39 za Malinzi ambaye alirejeshwa kuwania nafasi hiyo baada ya kushinda rufaa kutokana na kuenguliwa na kamati ya uchaguzi. Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa Tenga alisema " nawashukuru wajumbe kwa kunipa nafasi nyingine ya kumalizia kazi niliyoianza.'Pia alimuhakikishia Mwakilishi wa wa Shirikisho la Soka la Taifa (FIFA) kwenye uchaguzi huo Ashford Mamelodi kuwa kipindi cha miaka mnne ijayo kitakuwa cha kuendeleza maendeleo yaliyokwishafikiwa. Nate Malinzi pamoja na kukubali kushindwa alimuomba Tenga kutokuweka kisasi kwa wale ambao hawakumpigia kura jambo ambalo Tenga alimhakikishia halitakuwapo.Aidha Malinzi aliahidi kumkabidhi ilani yake ya uchaguzi ambayo itakuwa changamoto katika utendaji wake wa kazi. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Henry Tandau alimtangaza athumani Nyamlani kuwa mshindi wa nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa TFF, baada ya kujikusanyia kura 65 kati ya kura 107 zilizopigwa na kura mbili kuharibika. Mwalusako alipata kura 39 na Ali Mwanakatwe aliambulia kura moja. Katika nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais wa TFF ambaye anawakilisha klabu za Ligi Kuu, nafasi hiyo ilikwenda kwa mgombea Ramadhan Nassib aliyemwangusha mpinzani wake wa karibu Damas Ndumbalo aliyepata kura 45. Nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji imechukuliwa na wallace Karia ambaye ni mpinzani wake Abduk Sauko aliyepata kura 26 huku kura moja ikiharibika. Wajumbe wengine wa kamati ya utendaji kupitia kanda 11 za soka ni kama ifuatavyo: Amri Roshan ametetea nafasi yake katika kanda ya Kagera na Shinyanga kwa kumshinda Mbasha Masha kwa kura 88 kwa 19. kanda ya pili inayojumuisha mikoa ya Mara na Mwanza Samuel Nyalla ambayye alikuwa mgombea pekeealipata kura 73, kura 33 za hapana wakati kura tatu ziliharibika na kwa upande wa kanda ya Manyara na Arusha, Khafani Mgonja aliibuka kidedea kwa kupata kura 60 dhidi ya 45 za mpinzani wake Charles Mugodo, kura mbili ziliharibika kwenye uchanguzi huo. kanda ya Kigoma na Tabora, Msafiri Mgoyi alimbwaga Ismail rage kwa kura 75 dhidi ya 32. Akizungumza na alimbwaga Ismail Rage kwa kura 75 dhidi ya 32. Akizungumza na gazeti hili, Rage alisema kuwa: “ Nilikuwa naumwa na jana (juzi) jioni ndipo niliporuhusiwa kutoka hospitali lakini leo (jana) nimeweza kwenda kutumia haki yangu kupiga kura na kurejea nyumbani kupumzika.” Kwa upande wa kanda ya Mbeya na Rukwa Theophil Sikazwe alirejea kwa kupata kura 70 dhidi ya 36 za John Mwangakala na kanda ya Iringa na Ruvuma Eliud Mvella amekuwa mshindi kwa kupata kura 52 na kumbwaga Joseph Mapunda aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo akiwa amepata kura 50 huku John Kiteve akipata kura tano. Katika kanda ya Lindi na Mtwara Shaibu Nampunde alitetea nafasi yake kwa kupata kura 52 na Murtaz Mangungu kura 31, Juma Muruwa kura 19 na Vincent Majili kura tano. Kanda ya Dodoma na Singida Hussein Mwamba aliibuka mshindi kwa kunyakua kura 46 na kuwabwaga Mulami Ng’hambi aliyepata kura 43 na Nassor Kipenzi aliyeambulia kura 18 wakati Kanda ya Pwani na Morogoro ilichukuliwa na Athumani Kambi na kumbwaga Hassan Hassanol kwa kupata kura 57 dhidi ya 50. Wakati kanda ya Kilimanjaro na Tanga Khalid Mohamed alishinda kwa kupata kura 44 na kumwangusha Titus Bandawe aliyepata kura 27 huku Charles Mchau kura 25 na Benedict Macha kura 10. Kanda ya Dar es Salaam, Muhsin Balbhou aliishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 41 na kuwashinda wapinzani wake Omari Abdulkadir aliyepata kura 37 na Lameck Nyambaya aliyepata kura 29. Viongozi waliochaguliwa jana watakuwa madarakani kwa kipindi cha miaka miaka minne na kuongoza kwa jahazi la soka ya Tanzania ambalo limeanza kwenda katika njia sahihi. |
Tottenham Hotspur fight back from two goals down to draw 2-2 at home to Spartak Moscow and qualify for the last 32 of the UEFA Cup. Second-half goals by Luka Modric and Tom Huddlestone cancel out a first-half brace from Artem Dzyuba to ensure Spurs a second-placed finish in Group D.
Mjini London hii leo kunafanyika kongamano la mustakbali wa Visiwa vya Zanzibar lililoitishwa na jumuiya MUWAZA ambayo imesema madhumuni yake ni kuwaleta Wazanzibari pamoja kutoka ndani na nje ya nchi wajadili mambo yanayohusu nchi yao, kama vile Muungano wa Tanzania, haki za Zanzibar na kuiletea Zanzibar maendeleo. Mwenzangu Othman Miraji alizungumza kwa njia ya simu na Dr. Yusuf Saleh Salim, mmoja wa waasisi wa jumuiya ya Mustakbali wa Zanzibar, MUWAZA, kuhusu kongamano hilo: